Skip to main content

Yanga yamlilia Ngassa

KATIBU Mkuu wa klabu ya Yanga, Jonas Tiboroha amekiri kuondoka kwa mshambuliaji Mrisho Ngassa ni pengo kubwa kwa timu yao, lakini amewataka mashabiki na wanachama wa timu hiyo kuhakikisha wanapambana kumbakiza kiungo Haruna Niyonzima.

Tiboroha alisema ana uhakika watafikia makubaliano na kiungo huyo bora Afrika Mashariki katika siku chache zijazo ili aendelee kuichezea timu yao msimu ujao na kwa kushirikiana na nyota wengine waliopo na watakaowasajili.

Akizungumza na gazeti hili jana, Tiboroha alisema itakuwa wamefanya kosa kubwa endapo watamruhusu nyota huyo kuondoka kwani itakuwa ni pengo jingine baada ya Ngassa kuhamia Free State ya Afrika Kusini kwa mkataba wa miaka minne.

“Bado tupo kwenye mazungumzo na imani yangu kama Katibu Mkuu wa Yanga ni kwamba msimu ujao Niyonzima atabaki kuichezea Yanga kwa sababu mazungumzo yapo kwenye hatua nzuri na hata yeye mwenyewe ameonekana kutaka kubaki,” alisema Tiboroha.

Kiongozi huyo alisema wamekuwa na vikao virefu na viongozi wa juu wa Yanga kwa ajili ya kujadili suala la mchezaji huyo kwa lengo la kumalizana naye kwa kumpa kile alichowaomba kumboreshea katika usajili wake mpya na viongozi wamelipokea na kuahidi kulifanyia kazi haraka iwezekanavyo.

“Sidhani kama kuna kitakachoshindikana kwa sababu pande zote mbili zimeonekana kuelekea kuelewana na kizuri ni kwamba Niyonzima mwenyewe ameonyesha nia ya kutaka kuendelea kubaki Yanga endapo tutamboreshea maslahi yake aliyoyahitaji kwenye mkataba mpya,” alisema.

Alisema mbali na Niyonzima pia wanatarajia kuanza mazungumzo na wachezaji wao wengine waliomaliza mikataba yao ambao wangependa kuendelea nao msimu ujao ili kuwapa mikataba mipya.

Tiboroha alisema baada ya kuondoka kwa Ngassa kocha wao Hans van der Pluijm, aliwataka kufanya kila linalowezekana nyota hao kuwabakisha kwenye kikosi hicho ili kikosi chake kisipoteze uwezo wa kutetea ubingwa wao msimu ujao.

“Kocha Pluijm ametushauri kuhakikisha tunawabakiza baadhi ya nyota wetu waliomaliza muda wao akiwemo Mbuyu Twite, makipa Ally Mustapha ‘Barthez’ Deogratius Munishi ‘Dida’ na Kelvin Yondani ili asipate tabu ya kuanza kujenga upya timu yake na kupata tabu katika mbio za kutetea ubingwa wake,” alisema Tiboroha.

Niyonzima ameonekana kuitikisa klabu ya Yanga akitaka wampe dola 50,000 kama pesa ya usajili ili kusaini mkataba mpya wa kuendelea kuichezea timu hiyo kwa miaka

Comments

Popular posts from this blog

Rais Wa Burundu "Apinduliwa"......Ndege Yake Jana Ilishindwa Kutua Burundi na Kuamua Kurudi Tanzania

Nchini Burundi, aliyekua mkuu wa majeshi Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza Jumatano Mei 13 kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza amepinduliwa madarakani. Meja Generali Niyombareh alisema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza. Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari alisema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa. Wakati  Mapinduzi  hayo  yakitangazwa, Rais Nkurunziza alikuwa  nchini Tanzania kujumuika na viongozi wa kanda  ya Afrika Mashariki kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi tangu Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu. Baada  ya  tangazo  la  kupindulikwa  kwake, Rais  huyo  alipanda  ndege  kurejea  nchini  kwake  licha  ya  tangazo  la  kufungwa  kwa  mipaka  yote  na  viwanja  vya...

Diamond Amuita Jokate Makombo...."Mwacheni Ali Kiba Ajilie Makombo"

Mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ amemuita mpenzi wake wa zamani Jokate Mwegelo kuwa ni makombo na kudai kama zilipendwa huyo anatembea na hasimu wake Ali Kiba, hakuna jipya kwani anakula makombo. Diamond ametoa kauli hiyo Jumatano iliyopita wakati mwanahabari wetu alipotaka kujua anajisikiaje kuona wapenzi wake wa zamani Jokate na Wema Sepetu ‘Madam’ wanamuunga mkono Ali Kiba. Pamoja na kudaiwa kuwa Jokate ana uhusiano wa ‘kimalovee’ na Ali Kiba na mwenyewe kutokubali, ameungana na Wema kuendesha kampeni ya nguvu kwenye mitandao ya kijamii kuhamasisha watu wampigie kura Kiba kwenye Tuzo za Kili 2015 kwa kile kinachoelezwa kuwa ni kampeni ya kuuangusha ufalme wa Diamond kimuziki. Baada ya mwanahabari wetu kuujua ‘mchezo huo’ uliopamba moto kama moto wa kifuu mitandaoni ndipo alipomuuliza Diamond anauzungumziaje ambapo kwanza alikiri kuufahamu na kudai ameudharau maana hauna jipya. “Hamna jipya waache waendelee kumpigia...

Gharama za kupima ardhi kupunguzwa

SERIKALI imesema katika mwaka ujao wa fedha itapunguza gharama za upimaji ardhi kwa zaidi ya nusu ili kuwawezesha wanachi kupima maeneo yao, hali ambayo inaonekana itapunguza migogoro ya ardhi. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi wakati wa ziara mkoani hapa kwa ajili ya kutatua migogoro ya ardhi ambayo imedumu kwa miaka mingi. Akizungumza na watendaji wa sekta mbalimbali wa mkoa wa Tabora, Waziri Lukuvi alisema Wizara itapunguza kwa zaidi ya nusu, gharama za upimaji ardhi ili kila mwananchi aweze kupima eneo lake na kupata hati ya umiliki. Lukuvi aliongeza kuwa serikali pia itaweza kukusanya kwa wingi kodi ya pango la ardhi, hivyo kuongeza mapato ambayo yataisaidia serikali katika kufanikisha shughuli za maendeleo. Pamoja na kupunguza gharama hizo, Lukuvi aliwaonya maofisa ardhi kuacha tabia ya kuendesha shughuli za serikali kwa kukiuka taratibu, akitolea mfano wa maofisa hao kupima viwanja juu ya viwanja suala ambalo limekuwa lina...