Mtendaji wa Tume ya Mipango nchini, Dk Philip Mpango ameishauri kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuisisitiza serikali kuongeza mishahara ya watumishi wa umma na kupunguza kodi inayokatwa kwenye mishahara hiyo.
Lengo la hatua hiyo ni kuongeza tija na morali wa utendaji kazi kwa watumishi hao.
Aliyasema hayo jana jijini Dar es Salaam wakati kamati hiyo ikijadili Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa mwaka 2015/16 uliowasilishwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Uhusiano na Uratibu, Dk Mary Nagu mapema wiki iliyopita kwenye kamati ya bunge zima.
Dk Mpango alisema utendaji kazi kwa watumishi wa umma umeshuka na hilo linachangiwa na makato makubwa ya kodi ya (PAYE), ili hali mishahara yao ni midogo ukilinganisha na ile ya sekta binafsi.
“Kama tunataka watumishi wetu wafanye kazi kwa morali na kuwa na utendaji unaoridhisha, ni lazima tuwape mishahara na motisha yenye kuridhisha, vinginevyo utendaji wao utaendelea kushuka kwa kuwa malipo ya mishahara ni kidogo, halafu kodi ni kubwa,”alisema Dk Mpango.
Na kutoa mfano wa nchi ya Singapore ambayo imerekodiwa kuwa na utendaji nzuri kwa watumishi wake wa umma na hiyo imetokana na malipo mazuri ya mishahara wapewayo ukilinganisha na sekta binafsi
Comments
Post a Comment