Skip to main content

BRN yapaisha sekta ya elimu

SEKTA ya Elimu imefanikiwa kwa asilimia 81 na kushika nafasi ya kwanza katika utekelezaji wa awamu ya kwanza ya Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (BRN).

Matokeo ya utekelezaji wa mikakati iliyowekwa na BRN ni kupanda kwa ufaulu wa mtihani wa kumaliza Elimu ya Msingi (Darasa la Saba) na kupanda ufaulu wa mtihani wa kumaliza Elimu ya Sekondari (Kidato cha Nne).

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa aliyasema hayo bungeni jana wakati alipowasilisha Bajeti ya Mwaka 2015/16.

Dk Kawambwa alisema, “Kwa mujibu wa taarifa ya mwaka mmoja (2013/14) sekta ya elimu imefanikiwa kwa asilimia 81 na kushika nafasi ya kwanza katika utekelezaji wa awamu ya kwanza ya mikakati hiyo.”

Aliyajata baadhi ya mafanikio ambayo yamehakikiwa na ‘Presidential Delivery Bureau’ ni kutoa tuzo kwa shule na wanafunzi waliofanya vizuri kwenye matokeo ya darasa la saba na kidato cha nne.

Alisema jumla ya tuzo 3,044 zilitolewa kwa shule zilizopata ufaulu uliotukuka na zile zilizopanda kwa ufaulu ikilinganishwa na mwaka 2013.

Pia alisema walimu 4,103 wa masomo ya Sayansi, Hisabati na Lugha walipatiwa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kutambua wanafunzi wenye uwezo mdogo wa kumudu masomo.

Aidha, alisema ujenzi wa miundombinu ya shule 47 za sekondari kati ya 264 zilizolengwa katika awamu ya kwanza ulikamilika. Lengo ni kukamilisha ujenzi wa miundombinu ya shule 1,200 katika awamu tatu.

“Madeni ya shilingi 1,852,162,158.21 ya malimbikizo ya mishahara yalilipwa kwa watumishi 916 wa wizara,” aliongeza Dk Kawambwa.

Alisema matokeo ya utekelezaji wa mikakati hiyo ni kupanda kwa ufaulu wa darasa la saba kutoka asilimia 50.6 mwaka 2013 hadi kufikia asilimia 56.99 mwaka 2014.

“Na kupanda kwa ufaulu wa Mtihani wa kumaliza Elimu ya Sekondari (Kidato cha Nne) kutoka asilimia 57.09 mwaka 2013 hadi kufikia asilimia 69.76 mwaka 2014,” alieleza Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi.

Akizungumzia utungaji wa Sera za Elimu, alisema rasimu ya andiko la uanzishwaji wa Bodi ya Kitaalamu ya Walimu imekamilika, na kuwasilishwa katika mamlaka husika.

Aidha, alisema katika mwaka 2014/15, Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu ilitoa mikopo kwa wanafunzi 99,590 wakiwemo 2,117 wa Stashahada ya Elimu ya Ualimu wa masomo ya Sayansi na Hisabati.

Alisema Bodi hiyo ilikusanya marejesho ya mikopo kiasi cha Sh 15,978,993,320.04 sawa na asilimia 45.5 ya lengo la makusanyo kwa mwaka 2014/15 na hivyo kufikia Sh 75,575,793,215 sawa na asilimia 45.45 ya Sh 165,008,246,475 za madeni yaliyoiva.

Kuhusu changamoto katika mwaka wa fedha uliopita, ilisema mojawapo ilikuwa ni kulipa madeni ya wazabuni na huduma nyingine sasa yanafikia Sh 45,855,370,632.7.

Alisema kati ya hizo, Sh 25,195,672,974.2 ni deni la wazabuni wa vyuo vya ufundi na Sh 5,148,207,930.00 ni deni la posho za wahadhiri.

Akizungumzia vipaumbele kwa mwaka 2015/16, alisema Wizara itasimamia utungaji na utekelezaji wa Sera za Elimu, ithibati ya shule na udhibiti wa ubora wa elimu.

Kwa Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania, alisema itaendelea kuratibu na kusimamia udahili na ukaguzi wa wanafunzi 60,000 ili kufikia lengo la kuwa na wanafunzi 300,000 katika taasisi za elimu ya juu ifikapo mwaka 2016.

Kuhusu Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu, alisema itakusanya Sh 51,001,034,808.24 za marejesho ya mikopo iliyotolewa kati ya mwaka 1994/95 na 2014/15.

Dk Kawambwa aliliomba Bunge liidhinishe bajeti ya Sh 989,552,542,000, ambazo kati ya hizo, Sh 478,675,159,000 ni kwa ajili ya miradi ya maendeleo zikiwamo Sh bilioni 446.578 za ndani ambazo Sh bilioni 348.3 zitatumika wa ajili ya mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu.

Comments

Popular posts from this blog

Mnyukano urais chama cha walimu

a Gratian Mukoba. MCHUANO mkali umeibuka ndani ya Chama cha Walimu Nchini (CWT) baada ya wagombea 28 kujitosa kuwania Urais wa chama hicho chenye nguvu kutokana na kuundwa na idadi kubwa ya watumishi wa umma. Miongoni mwa wanaogombea ni rais wa sasa wa chama hicho, Gratian Mukoba ambaye pia Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Nchini (TUCTA). Uchaguzi huo unatarajiwa kufanyika Alhamisi wiki hii kwenye Ukumbi wa hoteli ya Ngurdoto, Arumeru mkoani Arusha siku ambayo itakuwa inahitimisha mkutano mkuu wa siku tatu wa chama hicho unaotarajiwa kufunguliwa kesho na Rais Jakata Kikwete. Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya chama hicho, Kanda ya Ziwa imeongoza kwa kutoa wagombea wengi wakiwemo wa mkoa wa Mwanza, Kaliyaya Masunga wa Ilemela, Magesa Kirati wa Kwimba, Marwa D. Marwa wa Nyamagana na Mashauri Benedict kutoka Sengerema. Wengine wa Kanda ya Ziwa ni Charles George wa Geita, Godi Kiduma, Lyangombe Dotto na Malimi Macheyeki kutoka Maswa mkoani Simiyu na Juma Boniface wa Bund...

Aunty Ezekiel ajifungua mtoto wa kike, amuita Cookie

Muigizaji wa filamu za Bongo, Aunty Ezekiel amejifungua mtoto wa kike siku ya Alhamis May 21. Mtoto huyo wa Aunty Ezekiel ambaye baba yake ni dancer wa Diamond aitwaye Mose Iyobo, amepewa jina la Cookie. Aunty ameshare habari hiyo na mashabiki wake wa Instagram: “Amin ktk Mungu ndio Mwisho wa Matatizo yote yaliyotuzunguka Hakuna mganga wala Mchawi pasipo Mungu. "Ahsante Mungu wang kwa kunikabidhi zawadi yang Asubuhi jana tar 21-05-2015 Muache yy atende kwani ndio nguzo yetu sote Nasema Ahsante tena Ahsante kwa zawadi hii kubwa ktk Maisha kwani ilikuwa ni kipindi kigumu chenye majaribu ya kila aina kupitia binaadamu wajizaniao wao ni miungu watu Bac endelea kunyoosha mkono wako ktk paji la kiumbe wako ukiwa kama kinga nami niwe kivuli tuu juu yake Amen Whn Jesus Say Yes Ni body can Say wht!!!!!!!Wlcm Baby Cookie wlcm 2 da world KIBOKO YANG…” Diamond ambaye ni uncle wa Cookie pia amempongeza Aunty na Mose kupitia Instagram: “Hongera sana @auntyezekiel na @...

Tanzanian Irene Kiwia Wins Woman of The Year Africa Award.

Africa Reconnect (http://www.africareconnect.com), a platform for women who have made remarkable contributions to the growth and development of the various nations in Africa has today awarded 11 Africans whose contributions to women empowerment in their countries is outstanding. The award ceremony, which took place in Polokwane, Limpopo South Africa, concluded a two day empowerment conference themed “ Accelerating Positive Change”. The 2015 awards recipient included; Seja Lorraine Semenya for best Cultural Developer in Africa, Dr. K. S Malukele for Best Community Developer in Africa, Mphatheleni Makaulele for Most Inspiring Woman in Africa, all from South Africa. The first lady of Akwibo State for Best Philanthropic in Africa and Irene Kiwia from Tanzania won Woman of the Year Africa award.