Skip to main content

BRN yapaisha sekta ya elimu

SEKTA ya Elimu imefanikiwa kwa asilimia 81 na kushika nafasi ya kwanza katika utekelezaji wa awamu ya kwanza ya Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (BRN).

Matokeo ya utekelezaji wa mikakati iliyowekwa na BRN ni kupanda kwa ufaulu wa mtihani wa kumaliza Elimu ya Msingi (Darasa la Saba) na kupanda ufaulu wa mtihani wa kumaliza Elimu ya Sekondari (Kidato cha Nne).

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa aliyasema hayo bungeni jana wakati alipowasilisha Bajeti ya Mwaka 2015/16.

Dk Kawambwa alisema, “Kwa mujibu wa taarifa ya mwaka mmoja (2013/14) sekta ya elimu imefanikiwa kwa asilimia 81 na kushika nafasi ya kwanza katika utekelezaji wa awamu ya kwanza ya mikakati hiyo.”

Aliyajata baadhi ya mafanikio ambayo yamehakikiwa na ‘Presidential Delivery Bureau’ ni kutoa tuzo kwa shule na wanafunzi waliofanya vizuri kwenye matokeo ya darasa la saba na kidato cha nne.

Alisema jumla ya tuzo 3,044 zilitolewa kwa shule zilizopata ufaulu uliotukuka na zile zilizopanda kwa ufaulu ikilinganishwa na mwaka 2013.

Pia alisema walimu 4,103 wa masomo ya Sayansi, Hisabati na Lugha walipatiwa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kutambua wanafunzi wenye uwezo mdogo wa kumudu masomo.

Aidha, alisema ujenzi wa miundombinu ya shule 47 za sekondari kati ya 264 zilizolengwa katika awamu ya kwanza ulikamilika. Lengo ni kukamilisha ujenzi wa miundombinu ya shule 1,200 katika awamu tatu.

“Madeni ya shilingi 1,852,162,158.21 ya malimbikizo ya mishahara yalilipwa kwa watumishi 916 wa wizara,” aliongeza Dk Kawambwa.

Alisema matokeo ya utekelezaji wa mikakati hiyo ni kupanda kwa ufaulu wa darasa la saba kutoka asilimia 50.6 mwaka 2013 hadi kufikia asilimia 56.99 mwaka 2014.

“Na kupanda kwa ufaulu wa Mtihani wa kumaliza Elimu ya Sekondari (Kidato cha Nne) kutoka asilimia 57.09 mwaka 2013 hadi kufikia asilimia 69.76 mwaka 2014,” alieleza Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi.

Akizungumzia utungaji wa Sera za Elimu, alisema rasimu ya andiko la uanzishwaji wa Bodi ya Kitaalamu ya Walimu imekamilika, na kuwasilishwa katika mamlaka husika.

Aidha, alisema katika mwaka 2014/15, Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu ilitoa mikopo kwa wanafunzi 99,590 wakiwemo 2,117 wa Stashahada ya Elimu ya Ualimu wa masomo ya Sayansi na Hisabati.

Alisema Bodi hiyo ilikusanya marejesho ya mikopo kiasi cha Sh 15,978,993,320.04 sawa na asilimia 45.5 ya lengo la makusanyo kwa mwaka 2014/15 na hivyo kufikia Sh 75,575,793,215 sawa na asilimia 45.45 ya Sh 165,008,246,475 za madeni yaliyoiva.

Kuhusu changamoto katika mwaka wa fedha uliopita, ilisema mojawapo ilikuwa ni kulipa madeni ya wazabuni na huduma nyingine sasa yanafikia Sh 45,855,370,632.7.

Alisema kati ya hizo, Sh 25,195,672,974.2 ni deni la wazabuni wa vyuo vya ufundi na Sh 5,148,207,930.00 ni deni la posho za wahadhiri.

Akizungumzia vipaumbele kwa mwaka 2015/16, alisema Wizara itasimamia utungaji na utekelezaji wa Sera za Elimu, ithibati ya shule na udhibiti wa ubora wa elimu.

Kwa Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania, alisema itaendelea kuratibu na kusimamia udahili na ukaguzi wa wanafunzi 60,000 ili kufikia lengo la kuwa na wanafunzi 300,000 katika taasisi za elimu ya juu ifikapo mwaka 2016.

Kuhusu Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu, alisema itakusanya Sh 51,001,034,808.24 za marejesho ya mikopo iliyotolewa kati ya mwaka 1994/95 na 2014/15.

Dk Kawambwa aliliomba Bunge liidhinishe bajeti ya Sh 989,552,542,000, ambazo kati ya hizo, Sh 478,675,159,000 ni kwa ajili ya miradi ya maendeleo zikiwamo Sh bilioni 446.578 za ndani ambazo Sh bilioni 348.3 zitatumika wa ajili ya mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu.

Comments

Popular posts from this blog

Rais Wa Burundu "Apinduliwa"......Ndege Yake Jana Ilishindwa Kutua Burundi na Kuamua Kurudi Tanzania

Nchini Burundi, aliyekua mkuu wa majeshi Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza Jumatano Mei 13 kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza amepinduliwa madarakani. Meja Generali Niyombareh alisema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza. Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari alisema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa. Wakati  Mapinduzi  hayo  yakitangazwa, Rais Nkurunziza alikuwa  nchini Tanzania kujumuika na viongozi wa kanda  ya Afrika Mashariki kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi tangu Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu. Baada  ya  tangazo  la  kupindulikwa  kwake, Rais  huyo  alipanda  ndege  kurejea  nchini  kwake  licha  ya  tangazo  la  kufungwa  kwa  mipaka  yote  na  viwanja  vya...

Diamond Amuita Jokate Makombo...."Mwacheni Ali Kiba Ajilie Makombo"

Mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ amemuita mpenzi wake wa zamani Jokate Mwegelo kuwa ni makombo na kudai kama zilipendwa huyo anatembea na hasimu wake Ali Kiba, hakuna jipya kwani anakula makombo. Diamond ametoa kauli hiyo Jumatano iliyopita wakati mwanahabari wetu alipotaka kujua anajisikiaje kuona wapenzi wake wa zamani Jokate na Wema Sepetu ‘Madam’ wanamuunga mkono Ali Kiba. Pamoja na kudaiwa kuwa Jokate ana uhusiano wa ‘kimalovee’ na Ali Kiba na mwenyewe kutokubali, ameungana na Wema kuendesha kampeni ya nguvu kwenye mitandao ya kijamii kuhamasisha watu wampigie kura Kiba kwenye Tuzo za Kili 2015 kwa kile kinachoelezwa kuwa ni kampeni ya kuuangusha ufalme wa Diamond kimuziki. Baada ya mwanahabari wetu kuujua ‘mchezo huo’ uliopamba moto kama moto wa kifuu mitandaoni ndipo alipomuuliza Diamond anauzungumziaje ambapo kwanza alikiri kuufahamu na kudai ameudharau maana hauna jipya. “Hamna jipya waache waendelee kumpigia...

Gharama za kupima ardhi kupunguzwa

SERIKALI imesema katika mwaka ujao wa fedha itapunguza gharama za upimaji ardhi kwa zaidi ya nusu ili kuwawezesha wanachi kupima maeneo yao, hali ambayo inaonekana itapunguza migogoro ya ardhi. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi wakati wa ziara mkoani hapa kwa ajili ya kutatua migogoro ya ardhi ambayo imedumu kwa miaka mingi. Akizungumza na watendaji wa sekta mbalimbali wa mkoa wa Tabora, Waziri Lukuvi alisema Wizara itapunguza kwa zaidi ya nusu, gharama za upimaji ardhi ili kila mwananchi aweze kupima eneo lake na kupata hati ya umiliki. Lukuvi aliongeza kuwa serikali pia itaweza kukusanya kwa wingi kodi ya pango la ardhi, hivyo kuongeza mapato ambayo yataisaidia serikali katika kufanikisha shughuli za maendeleo. Pamoja na kupunguza gharama hizo, Lukuvi aliwaonya maofisa ardhi kuacha tabia ya kuendesha shughuli za serikali kwa kukiuka taratibu, akitolea mfano wa maofisa hao kupima viwanja juu ya viwanja suala ambalo limekuwa lina...