Skip to main content

Bunge kukaa hadi Jumapili

MKUTANO wa 20 wa Bunge la Bajeti kwa mwaka wa fedha 2015/16, umelazimika kupanga kikao chake kufanyika keshokutwa Jumapili ili kwenda na ratiba.

Kwa mujibu wa ratiba mpya ya Mkutano huo iliyotolewa jana na Ofisi ya Bunge, keshokutwa Wizara ya Fedha itawasilisha bajeti yake kuanzia saa tano asubuhi.

Awali, Wizara ya Fedha ilipangwa kuwasilisha bajeti yake kesho, lakini ratiba ilivurugika Jumanne wiki hii baada ya kifo cha ghafla cha Mbunge wa Jimbo la Ukonga mkoani Dar es Salaam, Eugen Mwaiposa (CCM).

Kutokana na kifo hicho, Bunge liliahirishwa Jumanne mchana ikiwa ni saa chache baada ya kuwasilishwa kwa Bajeti ya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii.

Bunge lilirejea jana kwa kipindi cha Maswali ya Kawaida asubuhi bila kuwapo kwa Maswali ya Papo kwa Hapo kwa Waziri Mkuu na baadaye mjadala wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii uliendelea hadi jioni.

Leo itakuwa zamu ya Wizara ya Maji na kesho itakuwa Wizara ya Nishati na Madini, wizara mbili ambazo hotuba zao zilitakiwa kuwasilishwa Jumatano na Ijumaa.

Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi ambayo hotuba yake ilipangwa kuwasilishwa jana, sasa itawasilishwa Jumatatu wiki ijayo.

Aidha, ratiba hiyo inaonesha kuwa na siku tatu za Serikali na Kamati ya Bajeti kufanya majumuisho kuzingatia hoja zenye maslahi kwa Taifa zilizojitokeza wakati wa kujadili Bajeti za Wizara, sasa zimepunguzwa na kuwa siku mbili, Jumanne na Jumatano ijayo.

Bajeti ya Serikali itasomwa kama ilivyopangwa Alhamisi ijayo ikitanguliwa asubuhi na Taarifa ya Hali ya Uchumi itakayosomwa na Waziri mwenye dhamana ya Mipango.

Comments

Popular posts from this blog

Rais Wa Burundu "Apinduliwa"......Ndege Yake Jana Ilishindwa Kutua Burundi na Kuamua Kurudi Tanzania

Nchini Burundi, aliyekua mkuu wa majeshi Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza Jumatano Mei 13 kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza amepinduliwa madarakani. Meja Generali Niyombareh alisema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza. Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari alisema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa. Wakati  Mapinduzi  hayo  yakitangazwa, Rais Nkurunziza alikuwa  nchini Tanzania kujumuika na viongozi wa kanda  ya Afrika Mashariki kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi tangu Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu. Baada  ya  tangazo  la  kupindulikwa  kwake, Rais  huyo  alipanda  ndege  kurejea  nchini  kwake  licha  ya  tangazo  la  kufungwa  kwa  mipaka  yote  na  viwanja  vya...

Gharama za kupima ardhi kupunguzwa

SERIKALI imesema katika mwaka ujao wa fedha itapunguza gharama za upimaji ardhi kwa zaidi ya nusu ili kuwawezesha wanachi kupima maeneo yao, hali ambayo inaonekana itapunguza migogoro ya ardhi. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi wakati wa ziara mkoani hapa kwa ajili ya kutatua migogoro ya ardhi ambayo imedumu kwa miaka mingi. Akizungumza na watendaji wa sekta mbalimbali wa mkoa wa Tabora, Waziri Lukuvi alisema Wizara itapunguza kwa zaidi ya nusu, gharama za upimaji ardhi ili kila mwananchi aweze kupima eneo lake na kupata hati ya umiliki. Lukuvi aliongeza kuwa serikali pia itaweza kukusanya kwa wingi kodi ya pango la ardhi, hivyo kuongeza mapato ambayo yataisaidia serikali katika kufanikisha shughuli za maendeleo. Pamoja na kupunguza gharama hizo, Lukuvi aliwaonya maofisa ardhi kuacha tabia ya kuendesha shughuli za serikali kwa kukiuka taratibu, akitolea mfano wa maofisa hao kupima viwanja juu ya viwanja suala ambalo limekuwa lina...

Frola Mbasha Ajiunga CHADEMA

MWIMBAJI maarufu wa nyimbo za injili nchini, Frola Mbasha ameijunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema). Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika viwanja vya Tanganyika Packers mjini Dar es Salaam jana, Mbunge wa Kawe, Halima Mdee (Chadema), alisema kuijunga kwa Mbasha katika chama hicho kutasaidia kuhamasisha wasanii wengine ambao wamekuwa wakitumiwa na Chama Chama Mapinduzi (CCM), bila kupata mafanikio. ” Idadi kubwa ya wasanii nchini, wanateseka bila ya kujijua, hii inatokana na kutumiwa na CCM bila kupata mafanikio ya aina yoyote…Frola inabidi uwaelimishe ili waweze kujiunga na chama chetu,”alisema Mdee. Naye Mwenyekiti wa Chadema,Freeman Mbowe alisema siku Serikali itakapowasilisha muswada wa Sheria wa Vyombo vya Habari bungeni, wabunge wa chama hicho na wale wanauounda Umoja wa Katiba ya Wananchi ( Ukawa) watafanya vurugu ili kuhakikisha haupiti. Alisema baadhi ya vipengele vya muswada huo vinakandamiza waandishi na wananchi kupata...