Skip to main content

Mpinzani wa Lipumba afukuzwa uanachama

BARAZA Kuu la Uongozi la Chama cha Wananchi (CUF), limemvua uanachama mjumbe wake kutoka Mkoa wa Shinyanga, Chifu Lutayosa Yemba.

Chifu Yemba ambaye pia alikuwa ni mpinzani wa Profesa Ibrahim Lipumba katika kuwania uenyekiti wa CUF kwenye uchaguzi uliofanyika mwaka jana, alivuliwa uanachama kwa tuhuma za ubadhirifu wa fedha za chama pamoja na kutumia vibaya jina la mwenyekiti wa chama hicho.

Chanzo cha kuaminika kutoka ndani ya kikao hicho cha Baraza Kuu kilichoanza vikao vyake jana jijini Dar es Salaam, kimesema kuwa tuhuma za mjumbe huyo zilifikishwa mbele ya kikao hicho na kufikiwa uamuzi huo.

“Kikao cha Baraza Kuu bado kinaendelea hapa na ajenda kubwa ilikuwa ni tuhuma dhidi ya Chifu Yemba ambaye anadaiwa kutumia jina la Mwenyekiti wa chama kuanzisha Saccos na hata kusababisha chama kudaiwa shilingi milioni 12.

“Lakini pia amekuwa akitumia jina la Mwenyekiti wa chama, Profesa Lipumba katika mradi wake huo binafsi ambao anauendesha na hata kusababisha chama kuingia katika mgogoro hasa katika Mkoa wa Shinyanga,” kilisema chanzo hicho.

Chifu Yemba alipambana na Profesa Lipumba katika uchaguzi wa kuwania nafasi ya uenyekiti ambapo alipata kura 30 huku Lipumba akishinda kwa kura 659 na kufanikiwa kukiongoza tena chama hicho.

Chanzo hicho kilisema baada ya kufikiwa kwa uamuzi wa kuvuliwa uanachama kwa Mjumbe huyo wa Baraza Kuu, alitolewa nje ya ukumbi kwa ulinzi maalumu hadi nje ya geti na kuondoka.

Yemba kwa muda amekuwa haelewani na hata kushambuliana katika mitandao ya kijamii na Naibu Mkurugenzi wa Habari na Uenezi, Abdul Kambaya ambaye hivi karibuni alishindwa kura za maoni za kuwania ubunge wa Jimbo la Kinondoni.

Kutokana na kushindwa huko kwa Kambaya, kuliibua hisia mbalimbali miongoni mwa wana CUF hali iliyosababisha baadhi ya kikundi cha watu kuandamana na kwenda Makao Makuu ya CUF kufikisha malalamiko yao kuhusu mwenendo wa uchaguzi Kinondoni.

Alipotafutwa Naibu Mkurugenzi wa Habari wa Uenezi wa CUF, Abdul Kambaya, alithibitisha kuvuliwa uanachama kwa Chifu Yemba na kikao cha Baraza Kuu la Uongozi la CUF.

“Ni kweli tumemfukuza uanachama mjumbe wa Baraza Kuu kutoka Shinyanga kwa tuhuma mbalimbali, tutatoa taarifa rasmi kesho kutwa (kesho) kwa sababu kesho (leo) tunaenda mahakamani,” alisema Kambaya.

Pamoja na kufikiwa kwa uamuzi huo, mwandishi alimtafuta Chifu Yemba ambaye alithibitisha kufukuzwa kwake uanachama ndani ya CUF.

“Tatizo wana shaka na mimi sana, tuhuma zao zote hazina mashiko, katika mashtaka nilikubali moja tu la kutumia nembo ya chama, ni kweli na nikabadilisha sijaelewa jina la Profesa Lipumba nimelitumia vipi, wamepanga kuathiri taasisi na wataniathiri kwa kweli.

“Mimi sina tatizo na CUF, naipenda katika moyo wangu lakini wao hawanipendi na wamefanya maamuzi kikatiba, ila hizi ni hujuma za Kambaya (Abdul) na Sakaya (Magdalena) ambao ndio walipanga kuhakikisha natoka CUF na wamefanikiwa.

“… unajua mimi ni mwanasiasa, natafakari kwa kina hatua za kuchukua baada ya kutokea hili. Na kwa sasa najipanga kuendelea na maisha mengine ya kisiasa nje ya CUF,” alisema Chief Yemba.

Comments

Popular posts from this blog

Mnyukano urais chama cha walimu

a Gratian Mukoba. MCHUANO mkali umeibuka ndani ya Chama cha Walimu Nchini (CWT) baada ya wagombea 28 kujitosa kuwania Urais wa chama hicho chenye nguvu kutokana na kuundwa na idadi kubwa ya watumishi wa umma. Miongoni mwa wanaogombea ni rais wa sasa wa chama hicho, Gratian Mukoba ambaye pia Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Nchini (TUCTA). Uchaguzi huo unatarajiwa kufanyika Alhamisi wiki hii kwenye Ukumbi wa hoteli ya Ngurdoto, Arumeru mkoani Arusha siku ambayo itakuwa inahitimisha mkutano mkuu wa siku tatu wa chama hicho unaotarajiwa kufunguliwa kesho na Rais Jakata Kikwete. Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya chama hicho, Kanda ya Ziwa imeongoza kwa kutoa wagombea wengi wakiwemo wa mkoa wa Mwanza, Kaliyaya Masunga wa Ilemela, Magesa Kirati wa Kwimba, Marwa D. Marwa wa Nyamagana na Mashauri Benedict kutoka Sengerema. Wengine wa Kanda ya Ziwa ni Charles George wa Geita, Godi Kiduma, Lyangombe Dotto na Malimi Macheyeki kutoka Maswa mkoani Simiyu na Juma Boniface wa Bund...

Aunty Ezekiel ajifungua mtoto wa kike, amuita Cookie

Muigizaji wa filamu za Bongo, Aunty Ezekiel amejifungua mtoto wa kike siku ya Alhamis May 21. Mtoto huyo wa Aunty Ezekiel ambaye baba yake ni dancer wa Diamond aitwaye Mose Iyobo, amepewa jina la Cookie. Aunty ameshare habari hiyo na mashabiki wake wa Instagram: “Amin ktk Mungu ndio Mwisho wa Matatizo yote yaliyotuzunguka Hakuna mganga wala Mchawi pasipo Mungu. "Ahsante Mungu wang kwa kunikabidhi zawadi yang Asubuhi jana tar 21-05-2015 Muache yy atende kwani ndio nguzo yetu sote Nasema Ahsante tena Ahsante kwa zawadi hii kubwa ktk Maisha kwani ilikuwa ni kipindi kigumu chenye majaribu ya kila aina kupitia binaadamu wajizaniao wao ni miungu watu Bac endelea kunyoosha mkono wako ktk paji la kiumbe wako ukiwa kama kinga nami niwe kivuli tuu juu yake Amen Whn Jesus Say Yes Ni body can Say wht!!!!!!!Wlcm Baby Cookie wlcm 2 da world KIBOKO YANG…” Diamond ambaye ni uncle wa Cookie pia amempongeza Aunty na Mose kupitia Instagram: “Hongera sana @auntyezekiel na @...

Tanzanian Irene Kiwia Wins Woman of The Year Africa Award.

Africa Reconnect (http://www.africareconnect.com), a platform for women who have made remarkable contributions to the growth and development of the various nations in Africa has today awarded 11 Africans whose contributions to women empowerment in their countries is outstanding. The award ceremony, which took place in Polokwane, Limpopo South Africa, concluded a two day empowerment conference themed “ Accelerating Positive Change”. The 2015 awards recipient included; Seja Lorraine Semenya for best Cultural Developer in Africa, Dr. K. S Malukele for Best Community Developer in Africa, Mphatheleni Makaulele for Most Inspiring Woman in Africa, all from South Africa. The first lady of Akwibo State for Best Philanthropic in Africa and Irene Kiwia from Tanzania won Woman of the Year Africa award.