Skip to main content

Nooij asema Stars itang’ara

KOCHA wa timu ya soka Taifa, ‘Taifa Stars’, Mart Nooij amesema watajitahidi kuhakikisha wanafanya vyema katika michuano yote iliyoko mbele yao.

Taifa Stars ipo kwenye harakati za kuwania kufuzu michuano ya Kombe la Mataifa Afrika (AFCON) na ile ya Kombe la Afrika kwa wachezaji wa ndani (CHAN).

Kwa sasa timu hiyo ipo kambini ikitarajiwa kucheza na Misri Juni 14 katika mechi ya kuwania kufuzu Afcon. Akizungumza jana kwenye hafla fupi ya uzinduzi wa jezi na utoaji wa tuzo kwa waliotoa mchango kwenye soka ya Tanzania, Nooij alisema wana kikosi cha wachezaji 41 kambini ambapo baadhi wataondoka leo na wengine watabaki kujiandaa na michuano ya Chan.

“Tutajaribu kufanya vizuri, tuna Afcon na Chan yote ina umuhimu mkubwa kwetu, watakaobaki wataenda Zanzibar kwa maandalizi ya mchezo dhidi ya Uganda,” alisema.

Kwa upande wake nahodha wa Stars, Nadir Haroub alisema uzinduzi wa jezi mpya utawasaidia wao kuzivaa na kwenda kupambana kwa juhudi ili kupata ushindi.

Kocha Nooij leo anatarajiwa kutaja kikosi kitakachoenda Ethiopia kuweka kambi kwa ajili ya maandalizi dhidi ya Misri. Tangu kocha huyo ajiunge na Stars timu hiyo imekuwa haifanyi vizuri kwenye mechi zake mbalimbali, hali iliyopelekea wajumbe wa kamati ya Utendaji ya TFF kumpa mechi tatu za kufanya vizuri, akivurunda atafutwa kazi.

Ofisa Habari wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) ambao ndio wadhamini wa timu hiyo kupitia bia yao ya Kilimanjaro, Dorice Malulu alisema wanaitakia heri Taifa Stars katika maandalizi ya Afcon na kuahidi kutoa bonge la kiburudisho kwa timu hiyo.

Comments

Popular posts from this blog

Rais Wa Burundu "Apinduliwa"......Ndege Yake Jana Ilishindwa Kutua Burundi na Kuamua Kurudi Tanzania

Nchini Burundi, aliyekua mkuu wa majeshi Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza Jumatano Mei 13 kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza amepinduliwa madarakani. Meja Generali Niyombareh alisema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza. Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari alisema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa. Wakati  Mapinduzi  hayo  yakitangazwa, Rais Nkurunziza alikuwa  nchini Tanzania kujumuika na viongozi wa kanda  ya Afrika Mashariki kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi tangu Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu. Baada  ya  tangazo  la  kupindulikwa  kwake, Rais  huyo  alipanda  ndege  kurejea  nchini  kwake  licha  ya  tangazo  la  kufungwa  kwa  mipaka  yote  na  viwanja  vya...

Diamond Amuita Jokate Makombo...."Mwacheni Ali Kiba Ajilie Makombo"

Mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ amemuita mpenzi wake wa zamani Jokate Mwegelo kuwa ni makombo na kudai kama zilipendwa huyo anatembea na hasimu wake Ali Kiba, hakuna jipya kwani anakula makombo. Diamond ametoa kauli hiyo Jumatano iliyopita wakati mwanahabari wetu alipotaka kujua anajisikiaje kuona wapenzi wake wa zamani Jokate na Wema Sepetu ‘Madam’ wanamuunga mkono Ali Kiba. Pamoja na kudaiwa kuwa Jokate ana uhusiano wa ‘kimalovee’ na Ali Kiba na mwenyewe kutokubali, ameungana na Wema kuendesha kampeni ya nguvu kwenye mitandao ya kijamii kuhamasisha watu wampigie kura Kiba kwenye Tuzo za Kili 2015 kwa kile kinachoelezwa kuwa ni kampeni ya kuuangusha ufalme wa Diamond kimuziki. Baada ya mwanahabari wetu kuujua ‘mchezo huo’ uliopamba moto kama moto wa kifuu mitandaoni ndipo alipomuuliza Diamond anauzungumziaje ambapo kwanza alikiri kuufahamu na kudai ameudharau maana hauna jipya. “Hamna jipya waache waendelee kumpigia...

Gharama za kupima ardhi kupunguzwa

SERIKALI imesema katika mwaka ujao wa fedha itapunguza gharama za upimaji ardhi kwa zaidi ya nusu ili kuwawezesha wanachi kupima maeneo yao, hali ambayo inaonekana itapunguza migogoro ya ardhi. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi wakati wa ziara mkoani hapa kwa ajili ya kutatua migogoro ya ardhi ambayo imedumu kwa miaka mingi. Akizungumza na watendaji wa sekta mbalimbali wa mkoa wa Tabora, Waziri Lukuvi alisema Wizara itapunguza kwa zaidi ya nusu, gharama za upimaji ardhi ili kila mwananchi aweze kupima eneo lake na kupata hati ya umiliki. Lukuvi aliongeza kuwa serikali pia itaweza kukusanya kwa wingi kodi ya pango la ardhi, hivyo kuongeza mapato ambayo yataisaidia serikali katika kufanikisha shughuli za maendeleo. Pamoja na kupunguza gharama hizo, Lukuvi aliwaonya maofisa ardhi kuacha tabia ya kuendesha shughuli za serikali kwa kukiuka taratibu, akitolea mfano wa maofisa hao kupima viwanja juu ya viwanja suala ambalo limekuwa lina...