Skip to main content

Nooij asema Stars itang’ara

KOCHA wa timu ya soka Taifa, ‘Taifa Stars’, Mart Nooij amesema watajitahidi kuhakikisha wanafanya vyema katika michuano yote iliyoko mbele yao.

Taifa Stars ipo kwenye harakati za kuwania kufuzu michuano ya Kombe la Mataifa Afrika (AFCON) na ile ya Kombe la Afrika kwa wachezaji wa ndani (CHAN).

Kwa sasa timu hiyo ipo kambini ikitarajiwa kucheza na Misri Juni 14 katika mechi ya kuwania kufuzu Afcon. Akizungumza jana kwenye hafla fupi ya uzinduzi wa jezi na utoaji wa tuzo kwa waliotoa mchango kwenye soka ya Tanzania, Nooij alisema wana kikosi cha wachezaji 41 kambini ambapo baadhi wataondoka leo na wengine watabaki kujiandaa na michuano ya Chan.

“Tutajaribu kufanya vizuri, tuna Afcon na Chan yote ina umuhimu mkubwa kwetu, watakaobaki wataenda Zanzibar kwa maandalizi ya mchezo dhidi ya Uganda,” alisema.

Kwa upande wake nahodha wa Stars, Nadir Haroub alisema uzinduzi wa jezi mpya utawasaidia wao kuzivaa na kwenda kupambana kwa juhudi ili kupata ushindi.

Kocha Nooij leo anatarajiwa kutaja kikosi kitakachoenda Ethiopia kuweka kambi kwa ajili ya maandalizi dhidi ya Misri. Tangu kocha huyo ajiunge na Stars timu hiyo imekuwa haifanyi vizuri kwenye mechi zake mbalimbali, hali iliyopelekea wajumbe wa kamati ya Utendaji ya TFF kumpa mechi tatu za kufanya vizuri, akivurunda atafutwa kazi.

Ofisa Habari wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) ambao ndio wadhamini wa timu hiyo kupitia bia yao ya Kilimanjaro, Dorice Malulu alisema wanaitakia heri Taifa Stars katika maandalizi ya Afcon na kuahidi kutoa bonge la kiburudisho kwa timu hiyo.

Comments

Popular posts from this blog

Mnyukano urais chama cha walimu

a Gratian Mukoba. MCHUANO mkali umeibuka ndani ya Chama cha Walimu Nchini (CWT) baada ya wagombea 28 kujitosa kuwania Urais wa chama hicho chenye nguvu kutokana na kuundwa na idadi kubwa ya watumishi wa umma. Miongoni mwa wanaogombea ni rais wa sasa wa chama hicho, Gratian Mukoba ambaye pia Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Nchini (TUCTA). Uchaguzi huo unatarajiwa kufanyika Alhamisi wiki hii kwenye Ukumbi wa hoteli ya Ngurdoto, Arumeru mkoani Arusha siku ambayo itakuwa inahitimisha mkutano mkuu wa siku tatu wa chama hicho unaotarajiwa kufunguliwa kesho na Rais Jakata Kikwete. Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya chama hicho, Kanda ya Ziwa imeongoza kwa kutoa wagombea wengi wakiwemo wa mkoa wa Mwanza, Kaliyaya Masunga wa Ilemela, Magesa Kirati wa Kwimba, Marwa D. Marwa wa Nyamagana na Mashauri Benedict kutoka Sengerema. Wengine wa Kanda ya Ziwa ni Charles George wa Geita, Godi Kiduma, Lyangombe Dotto na Malimi Macheyeki kutoka Maswa mkoani Simiyu na Juma Boniface wa Bund...

Aunty Ezekiel ajifungua mtoto wa kike, amuita Cookie

Muigizaji wa filamu za Bongo, Aunty Ezekiel amejifungua mtoto wa kike siku ya Alhamis May 21. Mtoto huyo wa Aunty Ezekiel ambaye baba yake ni dancer wa Diamond aitwaye Mose Iyobo, amepewa jina la Cookie. Aunty ameshare habari hiyo na mashabiki wake wa Instagram: “Amin ktk Mungu ndio Mwisho wa Matatizo yote yaliyotuzunguka Hakuna mganga wala Mchawi pasipo Mungu. "Ahsante Mungu wang kwa kunikabidhi zawadi yang Asubuhi jana tar 21-05-2015 Muache yy atende kwani ndio nguzo yetu sote Nasema Ahsante tena Ahsante kwa zawadi hii kubwa ktk Maisha kwani ilikuwa ni kipindi kigumu chenye majaribu ya kila aina kupitia binaadamu wajizaniao wao ni miungu watu Bac endelea kunyoosha mkono wako ktk paji la kiumbe wako ukiwa kama kinga nami niwe kivuli tuu juu yake Amen Whn Jesus Say Yes Ni body can Say wht!!!!!!!Wlcm Baby Cookie wlcm 2 da world KIBOKO YANG…” Diamond ambaye ni uncle wa Cookie pia amempongeza Aunty na Mose kupitia Instagram: “Hongera sana @auntyezekiel na @...

Tanzanian Irene Kiwia Wins Woman of The Year Africa Award.

Africa Reconnect (http://www.africareconnect.com), a platform for women who have made remarkable contributions to the growth and development of the various nations in Africa has today awarded 11 Africans whose contributions to women empowerment in their countries is outstanding. The award ceremony, which took place in Polokwane, Limpopo South Africa, concluded a two day empowerment conference themed “ Accelerating Positive Change”. The 2015 awards recipient included; Seja Lorraine Semenya for best Cultural Developer in Africa, Dr. K. S Malukele for Best Community Developer in Africa, Mphatheleni Makaulele for Most Inspiring Woman in Africa, all from South Africa. The first lady of Akwibo State for Best Philanthropic in Africa and Irene Kiwia from Tanzania won Woman of the Year Africa award.