Skip to main content

Nyumba Anayoishi Ali Kiba Yazua Utata..Yadaiwa si yake Bali Kapewa Kuishi tu na Mrembo Amazing Anayeishi Singapore

Musa Mateja
Mjengo anaoishi mkali wa Bongo Fleva anayetamba na ngoma yake ya Chekecha Cheketua, Ali Saleh Kiba uliopo Kunduchi-Mbezi Beach jijini Dar, unadaiwa kuzua utata mkubwa hivyo kulilazimu Risasi Jumamosi kuchimba na kubaini kuwa nyumba hiyo si ya msanii huyo bali amepangisha.

Awali, Kiba alikaririwa akisema kuwa, mjengo huo wa kifahari ni wa ndugu yake aliyepo nje ya nchi ambaye alimpa ili aishi na ndugu zake (wa Kiba) wakati yeye (mmiliki) akiwa hayupo.Siku kadhaa mbele, baada ya Kiba kuvamiwa nyumbani hapo na watu kupora vitu huku akinusurika kuuawa, jamaa huyo alikaririwa redioni na kwenye mitandao ya kijamii akisema kuwa nyumba hiyo ni yake.

Ilidaiwa kwamba, mara tu baada ya Kiba kutangaza kumiliki nyumba hiyo, ilidaiwa kuwa aliibuka mwanamke aliyetajwa kwa jina moja la Mariana ikisemekana eti ndiye mmiliki halali wa nyumba hiyo.Madai mazito yaliendelea kushushwa kwamba, Mariana, akiwa mwandani wa Kiba ndiye aliyemuweka Kiba aishi kwenye nyumba hiyo wakati yeye (Mariana) kwa sasa anaishi nchini Singapore barani Asia.

“Ninyi mnasema ule mjengo ni wa Ali (Kiba)? Acheni hizo, kwa taarifa yenu hiyo nyumba kapewa na mrembo f’lani hivi amazing, anaitwa Mariana, ni Mbongo anayeishi Singapore.

“Muulizeni huyo Kiba awaambie ukweli,” kilisema chanzo chetu kikisisitiza: “Hata Mariana aliposikia eti nyumba ni ya Ali (Kiba) alishangaa na akamaindi ile mbaya hivyo kwa sasa sidhani kama wanaelewana kwa ajili hiyo.”

Baada ya kukutana na mkanganyiko huo, gazeti hili lilimtafuta Kiba ambaye alikiri kwamba kweli nyumba hiyo siyo yake bali amepangisha huku akikana kusema kuwa anaimiliki.Alipoulizwa juu ya madai ya kupewa nyumba hiyo na mwanamke aitwaye Mariana, Kiba alisema hayo ni maneno tu kwani anachojua yeye amepangisha.

“Kwanza hebu nitumie picha nijue ni nyumba gani?” aliomba Kiba ambapo alitumiwa picha kwa WhatsApp ndipo akajibu:
“Okey, kama ni hiyo nimepangisha lakini siyo kwamba sina nyumba

Comments

Popular posts from this blog

Rais Wa Burundu "Apinduliwa"......Ndege Yake Jana Ilishindwa Kutua Burundi na Kuamua Kurudi Tanzania

Nchini Burundi, aliyekua mkuu wa majeshi Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza Jumatano Mei 13 kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza amepinduliwa madarakani. Meja Generali Niyombareh alisema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza. Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari alisema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa. Wakati  Mapinduzi  hayo  yakitangazwa, Rais Nkurunziza alikuwa  nchini Tanzania kujumuika na viongozi wa kanda  ya Afrika Mashariki kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi tangu Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu. Baada  ya  tangazo  la  kupindulikwa  kwake, Rais  huyo  alipanda  ndege  kurejea  nchini  kwake  licha  ya  tangazo  la  kufungwa  kwa  mipaka  yote  na  viwanja  vya...

Diamond Amuita Jokate Makombo...."Mwacheni Ali Kiba Ajilie Makombo"

Mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ amemuita mpenzi wake wa zamani Jokate Mwegelo kuwa ni makombo na kudai kama zilipendwa huyo anatembea na hasimu wake Ali Kiba, hakuna jipya kwani anakula makombo. Diamond ametoa kauli hiyo Jumatano iliyopita wakati mwanahabari wetu alipotaka kujua anajisikiaje kuona wapenzi wake wa zamani Jokate na Wema Sepetu ‘Madam’ wanamuunga mkono Ali Kiba. Pamoja na kudaiwa kuwa Jokate ana uhusiano wa ‘kimalovee’ na Ali Kiba na mwenyewe kutokubali, ameungana na Wema kuendesha kampeni ya nguvu kwenye mitandao ya kijamii kuhamasisha watu wampigie kura Kiba kwenye Tuzo za Kili 2015 kwa kile kinachoelezwa kuwa ni kampeni ya kuuangusha ufalme wa Diamond kimuziki. Baada ya mwanahabari wetu kuujua ‘mchezo huo’ uliopamba moto kama moto wa kifuu mitandaoni ndipo alipomuuliza Diamond anauzungumziaje ambapo kwanza alikiri kuufahamu na kudai ameudharau maana hauna jipya. “Hamna jipya waache waendelee kumpigia...

Gharama za kupima ardhi kupunguzwa

SERIKALI imesema katika mwaka ujao wa fedha itapunguza gharama za upimaji ardhi kwa zaidi ya nusu ili kuwawezesha wanachi kupima maeneo yao, hali ambayo inaonekana itapunguza migogoro ya ardhi. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi wakati wa ziara mkoani hapa kwa ajili ya kutatua migogoro ya ardhi ambayo imedumu kwa miaka mingi. Akizungumza na watendaji wa sekta mbalimbali wa mkoa wa Tabora, Waziri Lukuvi alisema Wizara itapunguza kwa zaidi ya nusu, gharama za upimaji ardhi ili kila mwananchi aweze kupima eneo lake na kupata hati ya umiliki. Lukuvi aliongeza kuwa serikali pia itaweza kukusanya kwa wingi kodi ya pango la ardhi, hivyo kuongeza mapato ambayo yataisaidia serikali katika kufanikisha shughuli za maendeleo. Pamoja na kupunguza gharama hizo, Lukuvi aliwaonya maofisa ardhi kuacha tabia ya kuendesha shughuli za serikali kwa kukiuka taratibu, akitolea mfano wa maofisa hao kupima viwanja juu ya viwanja suala ambalo limekuwa lina...