Skip to main content

Padre na Wanafunzi sita Wateteketea Kwa Moto

WANAFUNZI sita wa Sekondari ya CTC Kigonsera inayomilikiwa na Misheni ya Mbinga mkoani Ruvuma na Mkuu wa Shule hiyo, Padre Yazint Kawonga, wamefariki dunia baada ya gari walilokuwa wakisafiria kutumbukia bondeni kisha kuwaka moto na kuiteketeza miili yao.

Akizungumza na Mpekuzi jana shuhuda wa ajali hiyo, Makarius Nchimbi, alisema ilitokea juzi saa tisa alasiri katika mlima uliopo karibu na shule hiyo huku likiwa limewabeba wanafunzi waliokuwa wakitokea shambani kuvuna mahindi ya shule hiyo.

Nchimbi ambaye ni mfanyakazi wa kitengo cha udereva katika misheni hiyo alidai yeye ndiye aliyekuwa dereva wa gari hilo kabla ya kupokelewa na Padre Kawonga aliyemtaka amsaidie kuliendesha kwa kuwarudisha shuleni wanafunzi waliokuwa shamba lililopo Kijiji cha Mkulumus kilichopo Kigonsera.

Alisema gari hilo aina ya Land Rover 110 Station Wagon lenye namba T 306 AYM  lilipofika katika mlima huo lilimshinda Padre Kawonga wakati akitumia gia namba mbili na kuanza kurudi nyuma huku wanafunzi wengine waliokaa juu walifanikiwa kuruka kabla halijatumbukia na baadhi yao 24 waliumia.

Alisema baada ya gari hilo kutumbukia bondeni wao walijitahidi kuingia kwenda kuvunja milango ili waweze kuwaokoa baadhi yao lakini ilishindikana kutokana na nyaya za umeme wa gari kulipuka na kuliunguza huku miili yao ikiwemo ndani  na kusababisha ishindwe kutambulika.

Alisema kutokana na moto kuwaka iliwalazimu watafute mbinu za kuuzima na walitumia maji lakini haikuwezekana na walifanya jitihada ya kuipata winchi iliyoweza kwenda kuliinua gari hilo likiwa limeteketea.

Kwa upande wake, Mganga Mkuu wa Kituo cha Afya cha Kigonsera, Dk. Patrik Mhagama, alisema kituo hicho kilipokea maiti saba na majeruhi wakiwa 24 na kati ya hao wawili wamepekwa Hospitali ya Mbinga kutokana na hali zao kuwa mbaya huku 17 walitibiwa na kuruhusiwa na watano bado wapo kituoni hapo.

Naye Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma, Mihayo Msikihela, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na alisema taratibu za kuyapata majina halisi ya marehemu bado zinaendelea na zikikamilika zitatolewa taarifa.

Aliwataja majeruhi hao kuwa ni Japheth Komba (16), Regobert Mahai (16), Edgar Maseko (16), Luiza Mbunda, Afa Kifaru (15), Nelalfred Nchimbi (16), Teodora Wolfa (16).

Comments

Popular posts from this blog

Mnyukano urais chama cha walimu

a Gratian Mukoba. MCHUANO mkali umeibuka ndani ya Chama cha Walimu Nchini (CWT) baada ya wagombea 28 kujitosa kuwania Urais wa chama hicho chenye nguvu kutokana na kuundwa na idadi kubwa ya watumishi wa umma. Miongoni mwa wanaogombea ni rais wa sasa wa chama hicho, Gratian Mukoba ambaye pia Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Nchini (TUCTA). Uchaguzi huo unatarajiwa kufanyika Alhamisi wiki hii kwenye Ukumbi wa hoteli ya Ngurdoto, Arumeru mkoani Arusha siku ambayo itakuwa inahitimisha mkutano mkuu wa siku tatu wa chama hicho unaotarajiwa kufunguliwa kesho na Rais Jakata Kikwete. Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya chama hicho, Kanda ya Ziwa imeongoza kwa kutoa wagombea wengi wakiwemo wa mkoa wa Mwanza, Kaliyaya Masunga wa Ilemela, Magesa Kirati wa Kwimba, Marwa D. Marwa wa Nyamagana na Mashauri Benedict kutoka Sengerema. Wengine wa Kanda ya Ziwa ni Charles George wa Geita, Godi Kiduma, Lyangombe Dotto na Malimi Macheyeki kutoka Maswa mkoani Simiyu na Juma Boniface wa Bund...

Aunty Ezekiel ajifungua mtoto wa kike, amuita Cookie

Muigizaji wa filamu za Bongo, Aunty Ezekiel amejifungua mtoto wa kike siku ya Alhamis May 21. Mtoto huyo wa Aunty Ezekiel ambaye baba yake ni dancer wa Diamond aitwaye Mose Iyobo, amepewa jina la Cookie. Aunty ameshare habari hiyo na mashabiki wake wa Instagram: “Amin ktk Mungu ndio Mwisho wa Matatizo yote yaliyotuzunguka Hakuna mganga wala Mchawi pasipo Mungu. "Ahsante Mungu wang kwa kunikabidhi zawadi yang Asubuhi jana tar 21-05-2015 Muache yy atende kwani ndio nguzo yetu sote Nasema Ahsante tena Ahsante kwa zawadi hii kubwa ktk Maisha kwani ilikuwa ni kipindi kigumu chenye majaribu ya kila aina kupitia binaadamu wajizaniao wao ni miungu watu Bac endelea kunyoosha mkono wako ktk paji la kiumbe wako ukiwa kama kinga nami niwe kivuli tuu juu yake Amen Whn Jesus Say Yes Ni body can Say wht!!!!!!!Wlcm Baby Cookie wlcm 2 da world KIBOKO YANG…” Diamond ambaye ni uncle wa Cookie pia amempongeza Aunty na Mose kupitia Instagram: “Hongera sana @auntyezekiel na @...

Tanzanian Irene Kiwia Wins Woman of The Year Africa Award.

Africa Reconnect (http://www.africareconnect.com), a platform for women who have made remarkable contributions to the growth and development of the various nations in Africa has today awarded 11 Africans whose contributions to women empowerment in their countries is outstanding. The award ceremony, which took place in Polokwane, Limpopo South Africa, concluded a two day empowerment conference themed “ Accelerating Positive Change”. The 2015 awards recipient included; Seja Lorraine Semenya for best Cultural Developer in Africa, Dr. K. S Malukele for Best Community Developer in Africa, Mphatheleni Makaulele for Most Inspiring Woman in Africa, all from South Africa. The first lady of Akwibo State for Best Philanthropic in Africa and Irene Kiwia from Tanzania won Woman of the Year Africa award.