Skip to main content

Polisi yakamata kontena la nyaya za milioni 150/-

Maalumu ya Dar es Salaam limekamata kontena likiwa na rola 15 za nyaya za umeme mali ya Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) zenye thamani ya Sh milioni 150.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Kaimu Kamishna wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam Simon Sirro, alisema nyanya hizo ziliibwa Februari 26 zikiwa zinasafirishwa kuelekea mkoani Kagera kwa ajili ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

Alisema baada ya wizi wa kontena hilo, kesi ilifunguliwa katika Kituo cha Polisi Buguruni na watuhumiwa watano kukamatwa na kufikishwa mahakamani.

Aliongeza kuwa wakati upelelezi ukiendelea Mei 25 mwaka huu, polisi walipokea taarifa kutoka kwa msiri kwamba maeneo ya Kibamba mtaa wa Kibengewe kuna kontena katika kiwanda cha kutengenezea matofali.

Alisema askari walifika eneo la tukio na kukuta kontena hilo lenye namba 00LU2876031 na kumhoji mlinzi wa eneo hilo ili kumpata mmiliki wa eneo na kontena hilo.

“Tunashukuru ilipofika saa 5:00 usiku tulifanikiwa kumpata mmiliki wa eneo hilo, Donesia Aidan (40) ambaye ni mfanyabiashara mkazi wa Mbezi makabe,” alisema Sirro.

Alisema taratibu zilikamilika na askari walifungua kontena hilo na zilikutwa rola za nyaya zipatazo 15 kati ya 17 zilizokuwepo katika kontena hilo siku lilipokuwa likisafirishwa.

Pia alisema jeshi la polisi lilifanikiwa kumkamata mtu mwingine anayehusika katika wizi wa kontena hilo, Prosper Mtei (43) ambaye ni mfanyabiashara na upelelezi unaendelea ili aweze kuunganishwa na watuhumiwa wengine katika kesi ya

Comments

Popular posts from this blog

Mnyukano urais chama cha walimu

a Gratian Mukoba. MCHUANO mkali umeibuka ndani ya Chama cha Walimu Nchini (CWT) baada ya wagombea 28 kujitosa kuwania Urais wa chama hicho chenye nguvu kutokana na kuundwa na idadi kubwa ya watumishi wa umma. Miongoni mwa wanaogombea ni rais wa sasa wa chama hicho, Gratian Mukoba ambaye pia Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Nchini (TUCTA). Uchaguzi huo unatarajiwa kufanyika Alhamisi wiki hii kwenye Ukumbi wa hoteli ya Ngurdoto, Arumeru mkoani Arusha siku ambayo itakuwa inahitimisha mkutano mkuu wa siku tatu wa chama hicho unaotarajiwa kufunguliwa kesho na Rais Jakata Kikwete. Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya chama hicho, Kanda ya Ziwa imeongoza kwa kutoa wagombea wengi wakiwemo wa mkoa wa Mwanza, Kaliyaya Masunga wa Ilemela, Magesa Kirati wa Kwimba, Marwa D. Marwa wa Nyamagana na Mashauri Benedict kutoka Sengerema. Wengine wa Kanda ya Ziwa ni Charles George wa Geita, Godi Kiduma, Lyangombe Dotto na Malimi Macheyeki kutoka Maswa mkoani Simiyu na Juma Boniface wa Bund...

Aunty Ezekiel ajifungua mtoto wa kike, amuita Cookie

Muigizaji wa filamu za Bongo, Aunty Ezekiel amejifungua mtoto wa kike siku ya Alhamis May 21. Mtoto huyo wa Aunty Ezekiel ambaye baba yake ni dancer wa Diamond aitwaye Mose Iyobo, amepewa jina la Cookie. Aunty ameshare habari hiyo na mashabiki wake wa Instagram: “Amin ktk Mungu ndio Mwisho wa Matatizo yote yaliyotuzunguka Hakuna mganga wala Mchawi pasipo Mungu. "Ahsante Mungu wang kwa kunikabidhi zawadi yang Asubuhi jana tar 21-05-2015 Muache yy atende kwani ndio nguzo yetu sote Nasema Ahsante tena Ahsante kwa zawadi hii kubwa ktk Maisha kwani ilikuwa ni kipindi kigumu chenye majaribu ya kila aina kupitia binaadamu wajizaniao wao ni miungu watu Bac endelea kunyoosha mkono wako ktk paji la kiumbe wako ukiwa kama kinga nami niwe kivuli tuu juu yake Amen Whn Jesus Say Yes Ni body can Say wht!!!!!!!Wlcm Baby Cookie wlcm 2 da world KIBOKO YANG…” Diamond ambaye ni uncle wa Cookie pia amempongeza Aunty na Mose kupitia Instagram: “Hongera sana @auntyezekiel na @...

Tanzanian Irene Kiwia Wins Woman of The Year Africa Award.

Africa Reconnect (http://www.africareconnect.com), a platform for women who have made remarkable contributions to the growth and development of the various nations in Africa has today awarded 11 Africans whose contributions to women empowerment in their countries is outstanding. The award ceremony, which took place in Polokwane, Limpopo South Africa, concluded a two day empowerment conference themed “ Accelerating Positive Change”. The 2015 awards recipient included; Seja Lorraine Semenya for best Cultural Developer in Africa, Dr. K. S Malukele for Best Community Developer in Africa, Mphatheleni Makaulele for Most Inspiring Woman in Africa, all from South Africa. The first lady of Akwibo State for Best Philanthropic in Africa and Irene Kiwia from Tanzania won Woman of the Year Africa award.