Skip to main content

Serikali yaandaa programu kunufaisha wasanii

Published on Wednesday, 03 June 2015 00:07
Written by Mgaya Kingoba, Dodoma
Hits: 72

SERIKALI inaandaa programu maalumu ya kunasa kazi za wasanii zinazochezwa redioni, kwenye televisheni na katika simu kufahamu kiasi gani kinastahili kulipwa kwa kutumia kazi hizo ili kuongeza mapato ya wasanii na ya serikali.

Aidha, tangu kuanza kwa urasimishaji wa kazi za sanaa, hadi kufikia Mei mwaka huu, CD na DVD 30,984 zimekamatwa kwa kazi za ndani na 45,166 kwa kazi za nje.

Pia Serikali imesema maandalizi ya kurekebisha Sheria ya Hakimiliki na Hakishiriki Namba 7 ya Mwaka 1999 imeanza na rasimu ya kwanza imeshaandaliwa.

Akizungumzia kifaa hicho, Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Janet Mbene alisema imetangazwa zabuni ya kutafuta programu hiyo ya kunasa kazi hizo kwa nia ya kujua kiasi gani anastahili kulipwa msanii na serikali.

Alisema stempu zilizotolewa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) tangu urasimishaji wa sanaa uanze ni 45,570,000 kwa muziki na 18,420,000 kwa filamu, na taarifa kama hizo hazikuwepo kabla ya urasimishaji.

“Mfumo wa pamoja wa kielektroniki wa kushughulikia utoaji wa stempu ya kodi uliozinduliwa tarehe 25, Mei, 2015 utasaidia taarifa kupatikana kwa haraka juu ya utoaji wa stempu na vibali mbalimbali vitakavyotolewa na Cosota, Basata, Bodi ya Filamu na TRA kwa kazi husika,” alieleza Naibu Waziri.

Akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu, Martha Mlata (CCM), Naibu Waziri alisema marekebisho ya Sheria ya Hakimiliki na Hakishiriki, yameanza kwa rasimu ya kwanza kuandaliwa baada ya kupata maoni na mapendekezo kutoka wadau wapatao 22.

Aliwataja wadau hao kuwa ni kutoka katika Ofisi ya Mwendesha Mashitaka Makao Makuu ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai, Mawakili wa Serikali, waigizaji, wachapishaji, mawakala wa kujitegemea na mapromota.

“Aidha, Waraka wa Baraza la Mawaziri umeandaliwa ili kupata maamuzi ya serikali na pindi hatua itakapokamilika muswada husika utawasilishwa bungeni,” alisema Naibu Waziri

Comments

Popular posts from this blog

Mnyukano urais chama cha walimu

a Gratian Mukoba. MCHUANO mkali umeibuka ndani ya Chama cha Walimu Nchini (CWT) baada ya wagombea 28 kujitosa kuwania Urais wa chama hicho chenye nguvu kutokana na kuundwa na idadi kubwa ya watumishi wa umma. Miongoni mwa wanaogombea ni rais wa sasa wa chama hicho, Gratian Mukoba ambaye pia Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Nchini (TUCTA). Uchaguzi huo unatarajiwa kufanyika Alhamisi wiki hii kwenye Ukumbi wa hoteli ya Ngurdoto, Arumeru mkoani Arusha siku ambayo itakuwa inahitimisha mkutano mkuu wa siku tatu wa chama hicho unaotarajiwa kufunguliwa kesho na Rais Jakata Kikwete. Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya chama hicho, Kanda ya Ziwa imeongoza kwa kutoa wagombea wengi wakiwemo wa mkoa wa Mwanza, Kaliyaya Masunga wa Ilemela, Magesa Kirati wa Kwimba, Marwa D. Marwa wa Nyamagana na Mashauri Benedict kutoka Sengerema. Wengine wa Kanda ya Ziwa ni Charles George wa Geita, Godi Kiduma, Lyangombe Dotto na Malimi Macheyeki kutoka Maswa mkoani Simiyu na Juma Boniface wa Bund...

Aunty Ezekiel ajifungua mtoto wa kike, amuita Cookie

Muigizaji wa filamu za Bongo, Aunty Ezekiel amejifungua mtoto wa kike siku ya Alhamis May 21. Mtoto huyo wa Aunty Ezekiel ambaye baba yake ni dancer wa Diamond aitwaye Mose Iyobo, amepewa jina la Cookie. Aunty ameshare habari hiyo na mashabiki wake wa Instagram: “Amin ktk Mungu ndio Mwisho wa Matatizo yote yaliyotuzunguka Hakuna mganga wala Mchawi pasipo Mungu. "Ahsante Mungu wang kwa kunikabidhi zawadi yang Asubuhi jana tar 21-05-2015 Muache yy atende kwani ndio nguzo yetu sote Nasema Ahsante tena Ahsante kwa zawadi hii kubwa ktk Maisha kwani ilikuwa ni kipindi kigumu chenye majaribu ya kila aina kupitia binaadamu wajizaniao wao ni miungu watu Bac endelea kunyoosha mkono wako ktk paji la kiumbe wako ukiwa kama kinga nami niwe kivuli tuu juu yake Amen Whn Jesus Say Yes Ni body can Say wht!!!!!!!Wlcm Baby Cookie wlcm 2 da world KIBOKO YANG…” Diamond ambaye ni uncle wa Cookie pia amempongeza Aunty na Mose kupitia Instagram: “Hongera sana @auntyezekiel na @...

Tanzanian Irene Kiwia Wins Woman of The Year Africa Award.

Africa Reconnect (http://www.africareconnect.com), a platform for women who have made remarkable contributions to the growth and development of the various nations in Africa has today awarded 11 Africans whose contributions to women empowerment in their countries is outstanding. The award ceremony, which took place in Polokwane, Limpopo South Africa, concluded a two day empowerment conference themed “ Accelerating Positive Change”. The 2015 awards recipient included; Seja Lorraine Semenya for best Cultural Developer in Africa, Dr. K. S Malukele for Best Community Developer in Africa, Mphatheleni Makaulele for Most Inspiring Woman in Africa, all from South Africa. The first lady of Akwibo State for Best Philanthropic in Africa and Irene Kiwia from Tanzania won Woman of the Year Africa award.