Skip to main content

‘Sheria ya 1971 inachangia ndoa, mimba za utotoni’

SERIKALI imeombwa kuangalia upya Sheria ya mtoto ya mwaka 1971 kwani imebainika kuwa ndio chanzo kimojawapo kinachoruhusu na kuchangia ndoa za utotoni pamoja na mimba za utotoni.

Akizungumza katika wa kongamano lililoandaliwa na Shirika la Intiative for Youth (INFOY), Mwenyekiti wa Baraza la Watoto Wilaya ya Arusha, Hassani Omary alisema ni wajibu wa serikali kuangalia upya sheria hiyo kwani sheria hii imekuwa ikiwaathiri watoto wengi hapa nchini.

Alisema sheria hiyo imekuwa ikiruhusu watoto hata wenye umri chini ya miaka 18 kuolewa iwapo tu wazazi wake watakapokubali, kitu ambacho kinawaathiri watoto wengi katika masomo yao.

Alisema ikitokea mtu mmoja kupeleka lalamiko lake katika vyombo vya sheria amekuwa akishindwa kutokana na sheria hiyo kuleta mkanganyiko kwani mtoto huyo hata awe mdogo kuolewa mradi tu familia yake iwe imeafiki.

Aidha mbali na sheria hii pia Serikali inatakiwa kutilia mkazo katika mila mbalimbali na desturi kwani mila zingine zimekuwa zikichangia kwa kiasi kikubwa watoto wadogo hasa wa kike kukosa haki zao za msingi kwa kuwalazimisha kuolewa iwapo tu viongozi wa mila zao wakitaka huku akitolea mfano kwa kabila la kimasai ambalo wamekuwa wakisimamia na kulazimisha watoto wao kuolewa pindi atakapovunja ungo. Kwa upande wake Mratibu wa mradi wa kulinda na kutetea haki ya sheria ya mtoto,

Laurent Sabuni alisema ni wajibu wa serikali kuangalia kwa makini sheria hiyo kwani imekuwa ikiwaathiri watoto na kuwakosesha haki zao.

Kwa upande wake, Ofisa Ustawi wa Jamii Manispaa ya Arusha, Saum Kweka alisema katika kipindi hicho ni wajibu wa kila mzazi kuhakikisha anamlinda mtoto wake, anampa elimu mtoto wake kuhusiana na mimba za utotoni.

Comments

Popular posts from this blog

Mnyukano urais chama cha walimu

a Gratian Mukoba. MCHUANO mkali umeibuka ndani ya Chama cha Walimu Nchini (CWT) baada ya wagombea 28 kujitosa kuwania Urais wa chama hicho chenye nguvu kutokana na kuundwa na idadi kubwa ya watumishi wa umma. Miongoni mwa wanaogombea ni rais wa sasa wa chama hicho, Gratian Mukoba ambaye pia Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Nchini (TUCTA). Uchaguzi huo unatarajiwa kufanyika Alhamisi wiki hii kwenye Ukumbi wa hoteli ya Ngurdoto, Arumeru mkoani Arusha siku ambayo itakuwa inahitimisha mkutano mkuu wa siku tatu wa chama hicho unaotarajiwa kufunguliwa kesho na Rais Jakata Kikwete. Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya chama hicho, Kanda ya Ziwa imeongoza kwa kutoa wagombea wengi wakiwemo wa mkoa wa Mwanza, Kaliyaya Masunga wa Ilemela, Magesa Kirati wa Kwimba, Marwa D. Marwa wa Nyamagana na Mashauri Benedict kutoka Sengerema. Wengine wa Kanda ya Ziwa ni Charles George wa Geita, Godi Kiduma, Lyangombe Dotto na Malimi Macheyeki kutoka Maswa mkoani Simiyu na Juma Boniface wa Bund...

Aunty Ezekiel ajifungua mtoto wa kike, amuita Cookie

Muigizaji wa filamu za Bongo, Aunty Ezekiel amejifungua mtoto wa kike siku ya Alhamis May 21. Mtoto huyo wa Aunty Ezekiel ambaye baba yake ni dancer wa Diamond aitwaye Mose Iyobo, amepewa jina la Cookie. Aunty ameshare habari hiyo na mashabiki wake wa Instagram: “Amin ktk Mungu ndio Mwisho wa Matatizo yote yaliyotuzunguka Hakuna mganga wala Mchawi pasipo Mungu. "Ahsante Mungu wang kwa kunikabidhi zawadi yang Asubuhi jana tar 21-05-2015 Muache yy atende kwani ndio nguzo yetu sote Nasema Ahsante tena Ahsante kwa zawadi hii kubwa ktk Maisha kwani ilikuwa ni kipindi kigumu chenye majaribu ya kila aina kupitia binaadamu wajizaniao wao ni miungu watu Bac endelea kunyoosha mkono wako ktk paji la kiumbe wako ukiwa kama kinga nami niwe kivuli tuu juu yake Amen Whn Jesus Say Yes Ni body can Say wht!!!!!!!Wlcm Baby Cookie wlcm 2 da world KIBOKO YANG…” Diamond ambaye ni uncle wa Cookie pia amempongeza Aunty na Mose kupitia Instagram: “Hongera sana @auntyezekiel na @...

Tanzanian Irene Kiwia Wins Woman of The Year Africa Award.

Africa Reconnect (http://www.africareconnect.com), a platform for women who have made remarkable contributions to the growth and development of the various nations in Africa has today awarded 11 Africans whose contributions to women empowerment in their countries is outstanding. The award ceremony, which took place in Polokwane, Limpopo South Africa, concluded a two day empowerment conference themed “ Accelerating Positive Change”. The 2015 awards recipient included; Seja Lorraine Semenya for best Cultural Developer in Africa, Dr. K. S Malukele for Best Community Developer in Africa, Mphatheleni Makaulele for Most Inspiring Woman in Africa, all from South Africa. The first lady of Akwibo State for Best Philanthropic in Africa and Irene Kiwia from Tanzania won Woman of the Year Africa award.