Skip to main content

‘Sheria ya 1971 inachangia ndoa, mimba za utotoni’

SERIKALI imeombwa kuangalia upya Sheria ya mtoto ya mwaka 1971 kwani imebainika kuwa ndio chanzo kimojawapo kinachoruhusu na kuchangia ndoa za utotoni pamoja na mimba za utotoni.

Akizungumza katika wa kongamano lililoandaliwa na Shirika la Intiative for Youth (INFOY), Mwenyekiti wa Baraza la Watoto Wilaya ya Arusha, Hassani Omary alisema ni wajibu wa serikali kuangalia upya sheria hiyo kwani sheria hii imekuwa ikiwaathiri watoto wengi hapa nchini.

Alisema sheria hiyo imekuwa ikiruhusu watoto hata wenye umri chini ya miaka 18 kuolewa iwapo tu wazazi wake watakapokubali, kitu ambacho kinawaathiri watoto wengi katika masomo yao.

Alisema ikitokea mtu mmoja kupeleka lalamiko lake katika vyombo vya sheria amekuwa akishindwa kutokana na sheria hiyo kuleta mkanganyiko kwani mtoto huyo hata awe mdogo kuolewa mradi tu familia yake iwe imeafiki.

Aidha mbali na sheria hii pia Serikali inatakiwa kutilia mkazo katika mila mbalimbali na desturi kwani mila zingine zimekuwa zikichangia kwa kiasi kikubwa watoto wadogo hasa wa kike kukosa haki zao za msingi kwa kuwalazimisha kuolewa iwapo tu viongozi wa mila zao wakitaka huku akitolea mfano kwa kabila la kimasai ambalo wamekuwa wakisimamia na kulazimisha watoto wao kuolewa pindi atakapovunja ungo. Kwa upande wake Mratibu wa mradi wa kulinda na kutetea haki ya sheria ya mtoto,

Laurent Sabuni alisema ni wajibu wa serikali kuangalia kwa makini sheria hiyo kwani imekuwa ikiwaathiri watoto na kuwakosesha haki zao.

Kwa upande wake, Ofisa Ustawi wa Jamii Manispaa ya Arusha, Saum Kweka alisema katika kipindi hicho ni wajibu wa kila mzazi kuhakikisha anamlinda mtoto wake, anampa elimu mtoto wake kuhusiana na mimba za utotoni.

Comments

Popular posts from this blog

Rais Wa Burundu "Apinduliwa"......Ndege Yake Jana Ilishindwa Kutua Burundi na Kuamua Kurudi Tanzania

Nchini Burundi, aliyekua mkuu wa majeshi Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza Jumatano Mei 13 kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza amepinduliwa madarakani. Meja Generali Niyombareh alisema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza. Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari alisema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa. Wakati  Mapinduzi  hayo  yakitangazwa, Rais Nkurunziza alikuwa  nchini Tanzania kujumuika na viongozi wa kanda  ya Afrika Mashariki kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi tangu Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu. Baada  ya  tangazo  la  kupindulikwa  kwake, Rais  huyo  alipanda  ndege  kurejea  nchini  kwake  licha  ya  tangazo  la  kufungwa  kwa  mipaka  yote  na  viwanja  vya...

Diamond Amuita Jokate Makombo...."Mwacheni Ali Kiba Ajilie Makombo"

Mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ amemuita mpenzi wake wa zamani Jokate Mwegelo kuwa ni makombo na kudai kama zilipendwa huyo anatembea na hasimu wake Ali Kiba, hakuna jipya kwani anakula makombo. Diamond ametoa kauli hiyo Jumatano iliyopita wakati mwanahabari wetu alipotaka kujua anajisikiaje kuona wapenzi wake wa zamani Jokate na Wema Sepetu ‘Madam’ wanamuunga mkono Ali Kiba. Pamoja na kudaiwa kuwa Jokate ana uhusiano wa ‘kimalovee’ na Ali Kiba na mwenyewe kutokubali, ameungana na Wema kuendesha kampeni ya nguvu kwenye mitandao ya kijamii kuhamasisha watu wampigie kura Kiba kwenye Tuzo za Kili 2015 kwa kile kinachoelezwa kuwa ni kampeni ya kuuangusha ufalme wa Diamond kimuziki. Baada ya mwanahabari wetu kuujua ‘mchezo huo’ uliopamba moto kama moto wa kifuu mitandaoni ndipo alipomuuliza Diamond anauzungumziaje ambapo kwanza alikiri kuufahamu na kudai ameudharau maana hauna jipya. “Hamna jipya waache waendelee kumpigia...

Aunty Ezekiel ajifungua mtoto wa kike, amuita Cookie

Muigizaji wa filamu za Bongo, Aunty Ezekiel amejifungua mtoto wa kike siku ya Alhamis May 21. Mtoto huyo wa Aunty Ezekiel ambaye baba yake ni dancer wa Diamond aitwaye Mose Iyobo, amepewa jina la Cookie. Aunty ameshare habari hiyo na mashabiki wake wa Instagram: “Amin ktk Mungu ndio Mwisho wa Matatizo yote yaliyotuzunguka Hakuna mganga wala Mchawi pasipo Mungu. "Ahsante Mungu wang kwa kunikabidhi zawadi yang Asubuhi jana tar 21-05-2015 Muache yy atende kwani ndio nguzo yetu sote Nasema Ahsante tena Ahsante kwa zawadi hii kubwa ktk Maisha kwani ilikuwa ni kipindi kigumu chenye majaribu ya kila aina kupitia binaadamu wajizaniao wao ni miungu watu Bac endelea kunyoosha mkono wako ktk paji la kiumbe wako ukiwa kama kinga nami niwe kivuli tuu juu yake Amen Whn Jesus Say Yes Ni body can Say wht!!!!!!!Wlcm Baby Cookie wlcm 2 da world KIBOKO YANG…” Diamond ambaye ni uncle wa Cookie pia amempongeza Aunty na Mose kupitia Instagram: “Hongera sana @auntyezekiel na @...