Skip to main content

Zatumwa bil 10/- kulipa walimu wapya

SERIKALI imetuma Sh bilioni 10 katika mikoa mbalimbali nchini kwa ajili ya kuwalipa walimu wapya ambao wameripoti kazini mapema mwezi uliopita.

Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba alisema hayo bungeni jana, alipotoa ufafanuzi kwa Mwongozo kwa Spika ulioombwa na Mbunge wa Tabora Mjini, Ismail Aden Rage (CCM).

Rage katika Mwongozo wake huo, alitaka kusikia kauli ya Serikali kuhusu walimu wapya ambao wamepangwa katika Manispaa ya Tabora na sehemu nyingine nchini kuwa hawajapewa fedha zao na wanaishi katika hali ngumu kwa sasa.

Naibu Waziri alikiri kuwa ni kweli wapo walimu katika baadhi ya halmashauri nchini, hawajalipwa fedha zao baada ya kuripoti kazini kutokana na sababu mbalimbali.

“Ni kweli wapo walimu hawajalipwa fedha zao kama alivyoeleza Mheshimiwa Rage. Yapo maeneo kadhaa nchini na hii imetokana na matatizo kati ya wizara husika na hazina,” alisema Mwigulu na kuongeza: “Ni kama nilivyoeleza hapa juzi kuwa watumishi wanapopangwa ni lazima kila kitu kikamilishwe, sasa hapa kulikuwa na tatizo katika maandalizi yao.

“Lakini jana (juzi) watu wa Hazina wamenihakikishia kuwa shilingi bilioni kumi zimeshapelekwa huko na sasa ni suala tu la kufikishwa kwa wahusika.”

Serikali ilitangaza kuanza kwa ajira za walimu wapya Mei Mosi mwaka huu. Idadi ya walimu wapya walioanza ajira hizo ni 31,056 ambapo kwa walimu wa ngazi ya Cheti ni 11,795, Stashahada 6,596 na wenye Shahada 12,665.

Comments

Popular posts from this blog

Mnyukano urais chama cha walimu

a Gratian Mukoba. MCHUANO mkali umeibuka ndani ya Chama cha Walimu Nchini (CWT) baada ya wagombea 28 kujitosa kuwania Urais wa chama hicho chenye nguvu kutokana na kuundwa na idadi kubwa ya watumishi wa umma. Miongoni mwa wanaogombea ni rais wa sasa wa chama hicho, Gratian Mukoba ambaye pia Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Nchini (TUCTA). Uchaguzi huo unatarajiwa kufanyika Alhamisi wiki hii kwenye Ukumbi wa hoteli ya Ngurdoto, Arumeru mkoani Arusha siku ambayo itakuwa inahitimisha mkutano mkuu wa siku tatu wa chama hicho unaotarajiwa kufunguliwa kesho na Rais Jakata Kikwete. Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya chama hicho, Kanda ya Ziwa imeongoza kwa kutoa wagombea wengi wakiwemo wa mkoa wa Mwanza, Kaliyaya Masunga wa Ilemela, Magesa Kirati wa Kwimba, Marwa D. Marwa wa Nyamagana na Mashauri Benedict kutoka Sengerema. Wengine wa Kanda ya Ziwa ni Charles George wa Geita, Godi Kiduma, Lyangombe Dotto na Malimi Macheyeki kutoka Maswa mkoani Simiyu na Juma Boniface wa Bund...

Aunty Ezekiel ajifungua mtoto wa kike, amuita Cookie

Muigizaji wa filamu za Bongo, Aunty Ezekiel amejifungua mtoto wa kike siku ya Alhamis May 21. Mtoto huyo wa Aunty Ezekiel ambaye baba yake ni dancer wa Diamond aitwaye Mose Iyobo, amepewa jina la Cookie. Aunty ameshare habari hiyo na mashabiki wake wa Instagram: “Amin ktk Mungu ndio Mwisho wa Matatizo yote yaliyotuzunguka Hakuna mganga wala Mchawi pasipo Mungu. "Ahsante Mungu wang kwa kunikabidhi zawadi yang Asubuhi jana tar 21-05-2015 Muache yy atende kwani ndio nguzo yetu sote Nasema Ahsante tena Ahsante kwa zawadi hii kubwa ktk Maisha kwani ilikuwa ni kipindi kigumu chenye majaribu ya kila aina kupitia binaadamu wajizaniao wao ni miungu watu Bac endelea kunyoosha mkono wako ktk paji la kiumbe wako ukiwa kama kinga nami niwe kivuli tuu juu yake Amen Whn Jesus Say Yes Ni body can Say wht!!!!!!!Wlcm Baby Cookie wlcm 2 da world KIBOKO YANG…” Diamond ambaye ni uncle wa Cookie pia amempongeza Aunty na Mose kupitia Instagram: “Hongera sana @auntyezekiel na @...

Tanzanian Irene Kiwia Wins Woman of The Year Africa Award.

Africa Reconnect (http://www.africareconnect.com), a platform for women who have made remarkable contributions to the growth and development of the various nations in Africa has today awarded 11 Africans whose contributions to women empowerment in their countries is outstanding. The award ceremony, which took place in Polokwane, Limpopo South Africa, concluded a two day empowerment conference themed “ Accelerating Positive Change”. The 2015 awards recipient included; Seja Lorraine Semenya for best Cultural Developer in Africa, Dr. K. S Malukele for Best Community Developer in Africa, Mphatheleni Makaulele for Most Inspiring Woman in Africa, all from South Africa. The first lady of Akwibo State for Best Philanthropic in Africa and Irene Kiwia from Tanzania won Woman of the Year Africa award.