Skip to main content

Lukuvi afunga ofisi nzima, ageukia wamiliki viwanja

 Kalunde Jamal, Mwananchi kjamal@mwananchi.co.tz
Dar es Salaam. Waziri wa Ardhi, William Lukuvi jana alifunga ofisi za ardhi na masijala za Jiji la Dar es Salaam, akisema anafunga mtambo wa kufyatua migogoro ya ardhi.
Waziri Lukuvi pia amewaonya wamiliki katika Mradi wa Viwanja 20,000 kukaa chonjo kwa kuwa wanaweza kunyang’anywa, huku akiagiza kuanza kwa msako wa watu waliotelekeza hati 6,000 za umiliki wa viwanja zilizotolewa na wizara yake takribani miaka 20 iliyopita.
Lakini, moto ulikuwa ofisi ya ardhi ya Jiji la Dar es Salaam ambako Waziri Lukuvi alitaka maofisa hao wakusanye nyaraka za ofisi yao na kuhamia wizarani kwa kuwa hawana cha kufanya eneo hilo.
“Mnajua kwa muda mrefu nimekuwa nikipambana na migogoro ya ardhi nchini, leo imefika tamati. Nimeshagundua chanzo chake kinatokea hapa. Nazifunga hizi ofisi,” alisema Waziri Lukuvi.
“Hizi ofisi zinatoa hati zisizotambulika kwa kisingizio cha ofa. Mtu yeyote mwenye ofa ya kiwanja na ina muhuri wa jiji haitambuliki. Aende kwa kamishna wa ardhi wa wilaya ilikotolewa ofa hiyo kwa ajili ya maelekezo ya jinsi ya kupata hati halisi, maofisa msipokee tena ofa hizo.”
Lukuvi ambaye alifika ofisi za jiji akiambatana na maofisa wa wizara yake pamoja na waandishi wa habari, alisema jiji halina ardhi, halipangi, halipimi na wala halimilikishi lakini linaendelea kutoa ofa za ardhi ambazo zinaisumbua wizara yake.
Alisema shughuli zote za ardhi zitafanywa na wilaya tano za Dar es Salaam na kanda, hivyo hakukuwa na sababu ya maofisa hao kuwa ofisi ya jiji.
Maofisa hao walijaribu kujitetea, lakini Waziri Lukuvi hakutaka kuwasikiliza akiwaambia watafanya hivyo wizarani.
Mkurugenzi wa Jiji, Spora Liana alisema kumekuwa na matumizi mabaya ya ofa kwa kuwa awali kulikuwa hakuna halmashauri na baada ya kuanzishwa, wajanja wamekuwa wakitumia maofisa ardhi wa jiji kuwatengenezea ofa ambazo huwekwa tarehe za zamani na hivyo kufanikisha umikishwaji usio halali.
Ofa ni nyaraka zilizokuwa zikitolewa kama sehemu ya mchakato wa kumilikishwa ardhi kabla ya kupata hati, lakini ilibainika baadaye zilikuwa zikitumika kumilikisha kinyemela watu walioongea vizuri na maofisa ardhi na kuwapora wanyonge haki zao.
Lukuvi alisema kwa sasa wanaendelea kukusanya taarifa na wakishaingia rasmi kwenye mfumo wa digitali, ofisi za ardhi za mikoa hazitatambulika tena na kuanzia sasa maombi yote yatatoka wilayani kwenda kwa kamishna wa ardhi wa wilaya husika.
“Kuna watu wamekaa mkao wa kula kazi yao kuchapisha ofa za jiji, nilishatoa miaka miwili watu wenye ofa hizi wazibadilishe kupitia kwa maofisa wa ardhi wa wilaya. Kuanzia sasa imekula kwao hatuzitambui tena,” alisema Lukuvi.
“Tunatoa hati moja kwa moja hakuna ofa. Nimeamua kufunga ofisi za ardhi za jiji na watendaji wote wataripoti wizarani.”
Mradi wa viwanja 20,000
Kuhusu walionunua viwanja kwenye Mradi wa Viwanja 20,000, Lukuvi alisema wote ambao hawajaviendeleza mwisho wa kuvimiliki ni Desemba.
Mwezi Juni, wizara hiyo ilitoa wiki mbili kwa walionunua viwanja hivyo kuviendeleza na kwamba ingeanza kukagua ili watakaobainika wachukuliwe hatua.
Jana Lukuvi alisema atawasamehe wale ambao watakuwa angalau wameweka uzio wa matofali na siyo wa maua au waya.
Mradi huo ulihusisha viwanja vilivyoko Bunju, Mpiji, Toangoma, Mwanagati, Kibada, Gezaulole, Mwongozo, Mbweni, Mbweni Malindi, Mbweni JKT na Kibada.
“Nilichogundua baadhi ya viwanja viliwekwa majina bandia, havina wamiliki na wengine wamesahau,” alisema.
“Nimewaita hawa maofisa wa wizara ili niwape maagizo ya mwisho, wafanye uchunguzi kwa yeyote aliyenunua kiwanja hajajenga hata ukuta, taratibu za kuchukua kiwanja chake zianze mara moja.
“Wale wachache waliojenga hawakai kwa raha kuna watu wanawavamia na kuwasumbua, hivyo watakwenda kuvifuatilia na kujua wamiliki ni kina nani. Inawezekana maofisa ardhi walivichukua na kuvitelekeza.”
Katika hatua nyingine, waziri huyo aliagiza msako wa kuwatambua wenye hati 6,000 waliozitelekeza katika wizara hiyo.
Huku akionyesha rundo la hati hizo kwenye makabati wizarani hapo, alisema zipo zilizotelekezwa kwa zaidi ya miaka 20.

Comments

Popular posts from this blog

Rais Wa Burundu "Apinduliwa"......Ndege Yake Jana Ilishindwa Kutua Burundi na Kuamua Kurudi Tanzania

Nchini Burundi, aliyekua mkuu wa majeshi Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza Jumatano Mei 13 kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza amepinduliwa madarakani. Meja Generali Niyombareh alisema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza. Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari alisema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa. Wakati  Mapinduzi  hayo  yakitangazwa, Rais Nkurunziza alikuwa  nchini Tanzania kujumuika na viongozi wa kanda  ya Afrika Mashariki kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi tangu Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu. Baada  ya  tangazo  la  kupindulikwa  kwake, Rais  huyo  alipanda  ndege  kurejea  nchini  kwake  licha  ya  tangazo  la  kufungwa  kwa  mipaka  yote  na  viwanja  vya...

Diamond Amuita Jokate Makombo...."Mwacheni Ali Kiba Ajilie Makombo"

Mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ amemuita mpenzi wake wa zamani Jokate Mwegelo kuwa ni makombo na kudai kama zilipendwa huyo anatembea na hasimu wake Ali Kiba, hakuna jipya kwani anakula makombo. Diamond ametoa kauli hiyo Jumatano iliyopita wakati mwanahabari wetu alipotaka kujua anajisikiaje kuona wapenzi wake wa zamani Jokate na Wema Sepetu ‘Madam’ wanamuunga mkono Ali Kiba. Pamoja na kudaiwa kuwa Jokate ana uhusiano wa ‘kimalovee’ na Ali Kiba na mwenyewe kutokubali, ameungana na Wema kuendesha kampeni ya nguvu kwenye mitandao ya kijamii kuhamasisha watu wampigie kura Kiba kwenye Tuzo za Kili 2015 kwa kile kinachoelezwa kuwa ni kampeni ya kuuangusha ufalme wa Diamond kimuziki. Baada ya mwanahabari wetu kuujua ‘mchezo huo’ uliopamba moto kama moto wa kifuu mitandaoni ndipo alipomuuliza Diamond anauzungumziaje ambapo kwanza alikiri kuufahamu na kudai ameudharau maana hauna jipya. “Hamna jipya waache waendelee kumpigia...

Aunty Ezekiel ajifungua mtoto wa kike, amuita Cookie

Muigizaji wa filamu za Bongo, Aunty Ezekiel amejifungua mtoto wa kike siku ya Alhamis May 21. Mtoto huyo wa Aunty Ezekiel ambaye baba yake ni dancer wa Diamond aitwaye Mose Iyobo, amepewa jina la Cookie. Aunty ameshare habari hiyo na mashabiki wake wa Instagram: “Amin ktk Mungu ndio Mwisho wa Matatizo yote yaliyotuzunguka Hakuna mganga wala Mchawi pasipo Mungu. "Ahsante Mungu wang kwa kunikabidhi zawadi yang Asubuhi jana tar 21-05-2015 Muache yy atende kwani ndio nguzo yetu sote Nasema Ahsante tena Ahsante kwa zawadi hii kubwa ktk Maisha kwani ilikuwa ni kipindi kigumu chenye majaribu ya kila aina kupitia binaadamu wajizaniao wao ni miungu watu Bac endelea kunyoosha mkono wako ktk paji la kiumbe wako ukiwa kama kinga nami niwe kivuli tuu juu yake Amen Whn Jesus Say Yes Ni body can Say wht!!!!!!!Wlcm Baby Cookie wlcm 2 da world KIBOKO YANG…” Diamond ambaye ni uncle wa Cookie pia amempongeza Aunty na Mose kupitia Instagram: “Hongera sana @auntyezekiel na @...