Skip to main content

ITV kuonesha tuzo za muziki za Kili

WAKATI homa za wasanii mbalimbali juu ya shindano la Kilimanjaro Tanzania Music Awards (KTMA) zikizidi kupanda, wadhamini wa shindano hilo, Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia bia yake ya Kilimanjaro Premium Lager, imeandaa kipindi cha runinga kitakachozungumzia juu ya tuzo hizo.

Hayo yamesemwa Dar es Salaam na Meneja wa bia ya Kilimanajro Premium Lager, Pamela Kikuli, na kueleza kuwa kipindi hichi kitaitwa ‘Kili Chats.’

Alisema sio mara ya kwanza kwa bia hiyo kuandaa kipindi cha aina hii kwani mwaka jana kilirushwa wakati wa msimu wa ‘Nani Mtani Jembe’, kampeni inayowashirikisha wakongwe wa soka hapa nchini Simba na Yanga.

Meneja huyo alisema sasa hivi wameamua kujikita katika muziki kwani ndio msimu wa KTMA kwa hivyo wanataka kusikia kutoka kwa wananchi kuhusu maoni yao.

“Huu ni mwanzo mzuri kuelekea KTMA ambapo tutaalika wadau mbalimbali kwa mfano Ma DJ, wanamitindo, washiriki katika video mbalimbali na wengine,” alisema Pamela.

Alisema kipindi hicho kitarushwa na televisheni ya ITV kila Jumanne saa moja usiku hadi saa moja na nusu kuanzia Mei 12, mwaka huu.

Alisisitiza kuwa, wasanii hawatahusishwa katika kipindi hicho ili kuhakikisha wote wanapewa haki sawa kuelekea usiku wa tuzo.

“Wasanii hawatahusishwa kabisa kwa kuwa wao wanashindanishwa kwenye KTMA na wote tutajua matokeo usiku ule wa tuzo kwa hivyo hata kwenye kipindi hatutatoa maelezo yoyote kuhusu kura,” alisema.

Hata hivyo, kwa mujibu wa Pamela kipindi hicho kitatumika kutoa maelezo kuhusu namna ya kupiga kura.

Alisema hadhira (audience) itakayoshiriki katika kipindi hicho itapatikana kupitia ukurasa wa Kili wa facebook na kisha kupewa nafasi ya kushiriki wakati wa kuandaa show.

Fainali za Kili Music Awards 2015 zinatarajiwa kufanyika Dar es Salaam Juni 13 mwaka huu.

Bia ya Kilimanjaro Premium Lager imedhamini tuzo hizi tangu kuanzishwa kwake mwaka 1999 na ndio moja ya tuzo zilizodumu kwa muda na kujizolea umaarufu mkubwa katika ukanda wa Afrika Mashariki na ya Kati

Comments

Popular posts from this blog

Mnyukano urais chama cha walimu

a Gratian Mukoba. MCHUANO mkali umeibuka ndani ya Chama cha Walimu Nchini (CWT) baada ya wagombea 28 kujitosa kuwania Urais wa chama hicho chenye nguvu kutokana na kuundwa na idadi kubwa ya watumishi wa umma. Miongoni mwa wanaogombea ni rais wa sasa wa chama hicho, Gratian Mukoba ambaye pia Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Nchini (TUCTA). Uchaguzi huo unatarajiwa kufanyika Alhamisi wiki hii kwenye Ukumbi wa hoteli ya Ngurdoto, Arumeru mkoani Arusha siku ambayo itakuwa inahitimisha mkutano mkuu wa siku tatu wa chama hicho unaotarajiwa kufunguliwa kesho na Rais Jakata Kikwete. Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya chama hicho, Kanda ya Ziwa imeongoza kwa kutoa wagombea wengi wakiwemo wa mkoa wa Mwanza, Kaliyaya Masunga wa Ilemela, Magesa Kirati wa Kwimba, Marwa D. Marwa wa Nyamagana na Mashauri Benedict kutoka Sengerema. Wengine wa Kanda ya Ziwa ni Charles George wa Geita, Godi Kiduma, Lyangombe Dotto na Malimi Macheyeki kutoka Maswa mkoani Simiyu na Juma Boniface wa Bund...

Aunty Ezekiel ajifungua mtoto wa kike, amuita Cookie

Muigizaji wa filamu za Bongo, Aunty Ezekiel amejifungua mtoto wa kike siku ya Alhamis May 21. Mtoto huyo wa Aunty Ezekiel ambaye baba yake ni dancer wa Diamond aitwaye Mose Iyobo, amepewa jina la Cookie. Aunty ameshare habari hiyo na mashabiki wake wa Instagram: “Amin ktk Mungu ndio Mwisho wa Matatizo yote yaliyotuzunguka Hakuna mganga wala Mchawi pasipo Mungu. "Ahsante Mungu wang kwa kunikabidhi zawadi yang Asubuhi jana tar 21-05-2015 Muache yy atende kwani ndio nguzo yetu sote Nasema Ahsante tena Ahsante kwa zawadi hii kubwa ktk Maisha kwani ilikuwa ni kipindi kigumu chenye majaribu ya kila aina kupitia binaadamu wajizaniao wao ni miungu watu Bac endelea kunyoosha mkono wako ktk paji la kiumbe wako ukiwa kama kinga nami niwe kivuli tuu juu yake Amen Whn Jesus Say Yes Ni body can Say wht!!!!!!!Wlcm Baby Cookie wlcm 2 da world KIBOKO YANG…” Diamond ambaye ni uncle wa Cookie pia amempongeza Aunty na Mose kupitia Instagram: “Hongera sana @auntyezekiel na @...

Tanzanian Irene Kiwia Wins Woman of The Year Africa Award.

Africa Reconnect (http://www.africareconnect.com), a platform for women who have made remarkable contributions to the growth and development of the various nations in Africa has today awarded 11 Africans whose contributions to women empowerment in their countries is outstanding. The award ceremony, which took place in Polokwane, Limpopo South Africa, concluded a two day empowerment conference themed “ Accelerating Positive Change”. The 2015 awards recipient included; Seja Lorraine Semenya for best Cultural Developer in Africa, Dr. K. S Malukele for Best Community Developer in Africa, Mphatheleni Makaulele for Most Inspiring Woman in Africa, all from South Africa. The first lady of Akwibo State for Best Philanthropic in Africa and Irene Kiwia from Tanzania won Woman of the Year Africa award.