Skip to main content

ITV kuonesha tuzo za muziki za Kili

WAKATI homa za wasanii mbalimbali juu ya shindano la Kilimanjaro Tanzania Music Awards (KTMA) zikizidi kupanda, wadhamini wa shindano hilo, Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia bia yake ya Kilimanjaro Premium Lager, imeandaa kipindi cha runinga kitakachozungumzia juu ya tuzo hizo.

Hayo yamesemwa Dar es Salaam na Meneja wa bia ya Kilimanajro Premium Lager, Pamela Kikuli, na kueleza kuwa kipindi hichi kitaitwa ‘Kili Chats.’

Alisema sio mara ya kwanza kwa bia hiyo kuandaa kipindi cha aina hii kwani mwaka jana kilirushwa wakati wa msimu wa ‘Nani Mtani Jembe’, kampeni inayowashirikisha wakongwe wa soka hapa nchini Simba na Yanga.

Meneja huyo alisema sasa hivi wameamua kujikita katika muziki kwani ndio msimu wa KTMA kwa hivyo wanataka kusikia kutoka kwa wananchi kuhusu maoni yao.

“Huu ni mwanzo mzuri kuelekea KTMA ambapo tutaalika wadau mbalimbali kwa mfano Ma DJ, wanamitindo, washiriki katika video mbalimbali na wengine,” alisema Pamela.

Alisema kipindi hicho kitarushwa na televisheni ya ITV kila Jumanne saa moja usiku hadi saa moja na nusu kuanzia Mei 12, mwaka huu.

Alisisitiza kuwa, wasanii hawatahusishwa katika kipindi hicho ili kuhakikisha wote wanapewa haki sawa kuelekea usiku wa tuzo.

“Wasanii hawatahusishwa kabisa kwa kuwa wao wanashindanishwa kwenye KTMA na wote tutajua matokeo usiku ule wa tuzo kwa hivyo hata kwenye kipindi hatutatoa maelezo yoyote kuhusu kura,” alisema.

Hata hivyo, kwa mujibu wa Pamela kipindi hicho kitatumika kutoa maelezo kuhusu namna ya kupiga kura.

Alisema hadhira (audience) itakayoshiriki katika kipindi hicho itapatikana kupitia ukurasa wa Kili wa facebook na kisha kupewa nafasi ya kushiriki wakati wa kuandaa show.

Fainali za Kili Music Awards 2015 zinatarajiwa kufanyika Dar es Salaam Juni 13 mwaka huu.

Bia ya Kilimanjaro Premium Lager imedhamini tuzo hizi tangu kuanzishwa kwake mwaka 1999 na ndio moja ya tuzo zilizodumu kwa muda na kujizolea umaarufu mkubwa katika ukanda wa Afrika Mashariki na ya Kati

Comments

Popular posts from this blog

Rais Wa Burundu "Apinduliwa"......Ndege Yake Jana Ilishindwa Kutua Burundi na Kuamua Kurudi Tanzania

Nchini Burundi, aliyekua mkuu wa majeshi Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza Jumatano Mei 13 kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza amepinduliwa madarakani. Meja Generali Niyombareh alisema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza. Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari alisema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa. Wakati  Mapinduzi  hayo  yakitangazwa, Rais Nkurunziza alikuwa  nchini Tanzania kujumuika na viongozi wa kanda  ya Afrika Mashariki kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi tangu Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu. Baada  ya  tangazo  la  kupindulikwa  kwake, Rais  huyo  alipanda  ndege  kurejea  nchini  kwake  licha  ya  tangazo  la  kufungwa  kwa  mipaka  yote  na  viwanja  vya...

Diamond Amuita Jokate Makombo...."Mwacheni Ali Kiba Ajilie Makombo"

Mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ amemuita mpenzi wake wa zamani Jokate Mwegelo kuwa ni makombo na kudai kama zilipendwa huyo anatembea na hasimu wake Ali Kiba, hakuna jipya kwani anakula makombo. Diamond ametoa kauli hiyo Jumatano iliyopita wakati mwanahabari wetu alipotaka kujua anajisikiaje kuona wapenzi wake wa zamani Jokate na Wema Sepetu ‘Madam’ wanamuunga mkono Ali Kiba. Pamoja na kudaiwa kuwa Jokate ana uhusiano wa ‘kimalovee’ na Ali Kiba na mwenyewe kutokubali, ameungana na Wema kuendesha kampeni ya nguvu kwenye mitandao ya kijamii kuhamasisha watu wampigie kura Kiba kwenye Tuzo za Kili 2015 kwa kile kinachoelezwa kuwa ni kampeni ya kuuangusha ufalme wa Diamond kimuziki. Baada ya mwanahabari wetu kuujua ‘mchezo huo’ uliopamba moto kama moto wa kifuu mitandaoni ndipo alipomuuliza Diamond anauzungumziaje ambapo kwanza alikiri kuufahamu na kudai ameudharau maana hauna jipya. “Hamna jipya waache waendelee kumpigia...

Gharama za kupima ardhi kupunguzwa

SERIKALI imesema katika mwaka ujao wa fedha itapunguza gharama za upimaji ardhi kwa zaidi ya nusu ili kuwawezesha wanachi kupima maeneo yao, hali ambayo inaonekana itapunguza migogoro ya ardhi. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi wakati wa ziara mkoani hapa kwa ajili ya kutatua migogoro ya ardhi ambayo imedumu kwa miaka mingi. Akizungumza na watendaji wa sekta mbalimbali wa mkoa wa Tabora, Waziri Lukuvi alisema Wizara itapunguza kwa zaidi ya nusu, gharama za upimaji ardhi ili kila mwananchi aweze kupima eneo lake na kupata hati ya umiliki. Lukuvi aliongeza kuwa serikali pia itaweza kukusanya kwa wingi kodi ya pango la ardhi, hivyo kuongeza mapato ambayo yataisaidia serikali katika kufanikisha shughuli za maendeleo. Pamoja na kupunguza gharama hizo, Lukuvi aliwaonya maofisa ardhi kuacha tabia ya kuendesha shughuli za serikali kwa kukiuka taratibu, akitolea mfano wa maofisa hao kupima viwanja juu ya viwanja suala ambalo limekuwa lina...