Skip to main content

Yanga yaenda Tunisia na matumaini kibao

MSAFARA wa watu 50 wa timu ya Yanga umeondoka nchini jana saa 5 usiku kwenda Tunisia kwa ajili ya mchezo wa hatua ya 16 bora wa michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Etoile du Sahel uliopangwa kupigwa Jumamosi usiku kwenye mji wa Sousse.

Katika msafara huo, Yanga imeondoka na kikosi cha wachezaji 20 kwa kutumia ndege ya Shirika la Ndege la Emirates kupitia Dubai kabla ya kwenda Tunisia, ambako ndipo yalipo makazi ya wapinzani wao Etoile.

Akizungumza na gazeti hili, kocha wa Yanga Hans van der Pluijm alisema wanakwenda Tunisia wakiwa na matumaini makubwa ya kupata ushindi kutokana na maandalizi mazuri waliyoyafanya hapa nchini ambayo anaamini yatawasaidia katika mchezo huo.

“Ni mchezo mgumu kutokana na ubora wa wapinzani wetu, lakini hilo haliwezi kututisha na kukubali kirahisi tumejizatiti kuhakikisha tunapambana na kupata ushindi kama ambavyo wao walipata sare nyumbani,” alisema Pluijm.

Pluijm alisema watahakikisha wanatumia mfumo wao waliozoea kucheza siku zote kwa kucheza kwa kasi na kutumia mawinga ili waweze kuwakimbiza mabeki wao ambao amegundua siyo wazuri hawana spidi kama ilivyo kwa wachezaji wake Mrisho Ngassa na Simon Msuva.

“Tunataka kutengeneza mashambulizi mengi kwenye lango lao ili kupata bao moja ambalo litawapa mshtuko kwa sababu ya presha kutoka kwa mashabiki wao na baada ya hapo kazi yetu itakuwa nyepesi ya kuwadhibiti washambuliaji wao ambao ni hatari kwa mipira ya krosi,” alisema Pluijm.

Katika hatua nyingine, Mkuu wa Idara ya Habari wa klabu ya hiyo, Jerry Muro aliwatoa hofu mashabiki wao na kuwataka kuwa na matumaini na kuendelea kuiombea timu yao ili waweke rekodi nyingine kwa kuwatoa mabingwa wa Afrika wa mwaka 2007 Etoile du Sahel.

Muro alisema kiwango cha timu yao kimewapa matumaini ya kuwatoa Etoile na wanakwenda Tunisia wakiwa na uhakika wa kuweka rekodi nyingine ya pili kwa mwaka huu baada ya ile waliyoiweka Jumatatu kwa kutwaa ubingwa wa Ligi ya Tanzania Bara kwa mara 25 huku wakiwa wamebakiwa na mechi mbili mkononi.

“Mashabiki wa Yanga wanapaswa kutokuwa na hofu na badala yake kuiombea timu yao iweze kufanikisha malengo yao ya kucheza hatua ya makundi mwaka huu na kuendelea kufurahi kama walivyo furahia ubingwa wa Tanzania Bara Jumatatu wiki hii pale Uwanja wa Taifa,” alisema Muro.

Kikosi cha Yanga ambacho kimeondoka jana ni Deogratius Munishi, Ally Mustapha, Oscar Joshua, Juma Abduli, Kelvin Yondan, Nadir Haroub, Mbuyu Twite, Rajab Zahiri, Said Juma, Haruna Niyonzima, Simon Msuva, Mrisho Ngassa, Amissi Tambwe, Kpah Sherman, Edward Charles, Danny Mrwanda, Hussein Javu, Nizar Khalfan, Andrey Coutinho na Pato Ngonyani.

Yanga, inahitaji ushindi wa aina yoyote au sare ya kuanzia mabao 2-2 ili iweze kusonga mbele katika hatua ya makundi katika michuano hiyo ya Kombe la Shirikisho kufuatia sare ya 1-1 katika mchezo wa kwanza uliofanyika Aprili 18 Dar es Salaam.

Comments

Popular posts from this blog

Mnyukano urais chama cha walimu

a Gratian Mukoba. MCHUANO mkali umeibuka ndani ya Chama cha Walimu Nchini (CWT) baada ya wagombea 28 kujitosa kuwania Urais wa chama hicho chenye nguvu kutokana na kuundwa na idadi kubwa ya watumishi wa umma. Miongoni mwa wanaogombea ni rais wa sasa wa chama hicho, Gratian Mukoba ambaye pia Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Nchini (TUCTA). Uchaguzi huo unatarajiwa kufanyika Alhamisi wiki hii kwenye Ukumbi wa hoteli ya Ngurdoto, Arumeru mkoani Arusha siku ambayo itakuwa inahitimisha mkutano mkuu wa siku tatu wa chama hicho unaotarajiwa kufunguliwa kesho na Rais Jakata Kikwete. Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya chama hicho, Kanda ya Ziwa imeongoza kwa kutoa wagombea wengi wakiwemo wa mkoa wa Mwanza, Kaliyaya Masunga wa Ilemela, Magesa Kirati wa Kwimba, Marwa D. Marwa wa Nyamagana na Mashauri Benedict kutoka Sengerema. Wengine wa Kanda ya Ziwa ni Charles George wa Geita, Godi Kiduma, Lyangombe Dotto na Malimi Macheyeki kutoka Maswa mkoani Simiyu na Juma Boniface wa Bund...

Aunty Ezekiel ajifungua mtoto wa kike, amuita Cookie

Muigizaji wa filamu za Bongo, Aunty Ezekiel amejifungua mtoto wa kike siku ya Alhamis May 21. Mtoto huyo wa Aunty Ezekiel ambaye baba yake ni dancer wa Diamond aitwaye Mose Iyobo, amepewa jina la Cookie. Aunty ameshare habari hiyo na mashabiki wake wa Instagram: “Amin ktk Mungu ndio Mwisho wa Matatizo yote yaliyotuzunguka Hakuna mganga wala Mchawi pasipo Mungu. "Ahsante Mungu wang kwa kunikabidhi zawadi yang Asubuhi jana tar 21-05-2015 Muache yy atende kwani ndio nguzo yetu sote Nasema Ahsante tena Ahsante kwa zawadi hii kubwa ktk Maisha kwani ilikuwa ni kipindi kigumu chenye majaribu ya kila aina kupitia binaadamu wajizaniao wao ni miungu watu Bac endelea kunyoosha mkono wako ktk paji la kiumbe wako ukiwa kama kinga nami niwe kivuli tuu juu yake Amen Whn Jesus Say Yes Ni body can Say wht!!!!!!!Wlcm Baby Cookie wlcm 2 da world KIBOKO YANG…” Diamond ambaye ni uncle wa Cookie pia amempongeza Aunty na Mose kupitia Instagram: “Hongera sana @auntyezekiel na @...

Tanzanian Irene Kiwia Wins Woman of The Year Africa Award.

Africa Reconnect (http://www.africareconnect.com), a platform for women who have made remarkable contributions to the growth and development of the various nations in Africa has today awarded 11 Africans whose contributions to women empowerment in their countries is outstanding. The award ceremony, which took place in Polokwane, Limpopo South Africa, concluded a two day empowerment conference themed “ Accelerating Positive Change”. The 2015 awards recipient included; Seja Lorraine Semenya for best Cultural Developer in Africa, Dr. K. S Malukele for Best Community Developer in Africa, Mphatheleni Makaulele for Most Inspiring Woman in Africa, all from South Africa. The first lady of Akwibo State for Best Philanthropic in Africa and Irene Kiwia from Tanzania won Woman of the Year Africa award.