Skip to main content

16 waitwa Taifa Stars

KOCHA wa timu ya Taifa Tanzania ‘Taifa Stars’, Mart Nooij amewaita wachezaji 16 kuingia kambini leo kwa ajili ya maandalizi ya mchezo wa kufuzu fainali za Mataifa ya Afrika (Afcon) 2017 huku mchezaji wa Mgambo JKT, Malimi Busungu akiitwa kwa mara ya kwanza.

Busungu ni miongoni mwa washambuliaji waliofanya vizuri msimu uliopita katika Ligi Kuu Tanzania Bara iliyomalizika hivi karibuni akiwa na mabao tisa.

Amekuwa akihusishwa kutaka kusajiliwa na klabu za Yanga, Simba na Azam Fc.

Kwa mujibu wa Ofisa Habari na Mawasiliano wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Baraka Kizuguto, Kikosi hicho kilichoitwa na Nooij kitaingia kambini kwenye hoteli ya Tansoma kupimwa afya zao na kujua maendeleo yao kabla ya kujumuishwa na kikosi kilichoshiriki michuano ya Baraza la Vyama vya Soka Kusini mwa Afrika (Cosafa).

Wachezaji wanaoingia kambini kupimwa afya ni Mohamed Hussein, Peter Manyika, Hassan Isihaka, Jonas Mkude (Simba SC), Salum Telela, Juma Abdul, Nadir Haroub (Yanga ), Aishi Manula, Mudathir Yahya, Frank Domayo na Kelvin Friday (Azam FC).

Wengine ni Rashid Mandawa, Atupele Green (Kagera Sugar), Haroun Chanongo (Stand United), Malimi Busungu (Mgambo JKT) na Emmanuel Simwanda (African Lyon).

“Mara baada ya kurejea kutoka nchini Afrika Kusini, Nooij aliwapa mapumziko ya siku 10, wachezaji waliokuwa kwenye michuano ya Cosafa mpaka Juni Mosi ambapo ndipo watajumuika na wachezaji wengine waliopo kambini,” alisema.

Alisema wachezaji wote wataungana katika kambi ya pamoja Juni mosi 2015 kujiandaa na mechi hiyo itakayochezwa jijini Alexandria kwenye uwanja wa Borg El Arab, Juni 14, 2015.

Aidha, wachezaji wa Tanzania wanaocheza soka la kulipwa TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu pia watakuwepo kwenye kikosi kitakachokwenda Misri.

Kabla ya kuelekea nchini Misri, Taifa Stars inatarajiwa kuweka kambi jijini Addis Ababa, Ethiopia kuanzia Juni 4, mwaka huu kwa muda wa wiki moja kabla ya kwenda Misri kwenye mchezo huo dhidi ya Mafarao

Comments

Popular posts from this blog

Mnyukano urais chama cha walimu

a Gratian Mukoba. MCHUANO mkali umeibuka ndani ya Chama cha Walimu Nchini (CWT) baada ya wagombea 28 kujitosa kuwania Urais wa chama hicho chenye nguvu kutokana na kuundwa na idadi kubwa ya watumishi wa umma. Miongoni mwa wanaogombea ni rais wa sasa wa chama hicho, Gratian Mukoba ambaye pia Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Nchini (TUCTA). Uchaguzi huo unatarajiwa kufanyika Alhamisi wiki hii kwenye Ukumbi wa hoteli ya Ngurdoto, Arumeru mkoani Arusha siku ambayo itakuwa inahitimisha mkutano mkuu wa siku tatu wa chama hicho unaotarajiwa kufunguliwa kesho na Rais Jakata Kikwete. Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya chama hicho, Kanda ya Ziwa imeongoza kwa kutoa wagombea wengi wakiwemo wa mkoa wa Mwanza, Kaliyaya Masunga wa Ilemela, Magesa Kirati wa Kwimba, Marwa D. Marwa wa Nyamagana na Mashauri Benedict kutoka Sengerema. Wengine wa Kanda ya Ziwa ni Charles George wa Geita, Godi Kiduma, Lyangombe Dotto na Malimi Macheyeki kutoka Maswa mkoani Simiyu na Juma Boniface wa Bund...

Aunty Ezekiel ajifungua mtoto wa kike, amuita Cookie

Muigizaji wa filamu za Bongo, Aunty Ezekiel amejifungua mtoto wa kike siku ya Alhamis May 21. Mtoto huyo wa Aunty Ezekiel ambaye baba yake ni dancer wa Diamond aitwaye Mose Iyobo, amepewa jina la Cookie. Aunty ameshare habari hiyo na mashabiki wake wa Instagram: “Amin ktk Mungu ndio Mwisho wa Matatizo yote yaliyotuzunguka Hakuna mganga wala Mchawi pasipo Mungu. "Ahsante Mungu wang kwa kunikabidhi zawadi yang Asubuhi jana tar 21-05-2015 Muache yy atende kwani ndio nguzo yetu sote Nasema Ahsante tena Ahsante kwa zawadi hii kubwa ktk Maisha kwani ilikuwa ni kipindi kigumu chenye majaribu ya kila aina kupitia binaadamu wajizaniao wao ni miungu watu Bac endelea kunyoosha mkono wako ktk paji la kiumbe wako ukiwa kama kinga nami niwe kivuli tuu juu yake Amen Whn Jesus Say Yes Ni body can Say wht!!!!!!!Wlcm Baby Cookie wlcm 2 da world KIBOKO YANG…” Diamond ambaye ni uncle wa Cookie pia amempongeza Aunty na Mose kupitia Instagram: “Hongera sana @auntyezekiel na @...

Tanzanian Irene Kiwia Wins Woman of The Year Africa Award.

Africa Reconnect (http://www.africareconnect.com), a platform for women who have made remarkable contributions to the growth and development of the various nations in Africa has today awarded 11 Africans whose contributions to women empowerment in their countries is outstanding. The award ceremony, which took place in Polokwane, Limpopo South Africa, concluded a two day empowerment conference themed “ Accelerating Positive Change”. The 2015 awards recipient included; Seja Lorraine Semenya for best Cultural Developer in Africa, Dr. K. S Malukele for Best Community Developer in Africa, Mphatheleni Makaulele for Most Inspiring Woman in Africa, all from South Africa. The first lady of Akwibo State for Best Philanthropic in Africa and Irene Kiwia from Tanzania won Woman of the Year Africa award.