Skip to main content

Watendaji wala rushwa wanawaponza waadilifu

estus Kilufi

MBUNGE wa Mbarali, Modestus Kilufi (CCM), amesema watendaji wala rushwa na mafisadi wanasababisha mawaziri waadilifu walaumiwe bila sababu.

Ametangaza vita na watendaji hao na wawekezaji katika jimbo lake ambao wanadaiwa kutaka kuyumbisha uamuzi wa suala la mipaka kati ya wananchi na hifadhi ya Ihefu katika Hifadhi ya Ruaha mkoani Mbeya.

Hivi karibuni, Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu alitangaza kuwa wananchi wataendelea kuishi katika maeneo yao baada ya kutatuliwa kwa mgogoro wa mpaka ulikuwapo kwa muda mrefu.

Akichangia bajeti ya Wizara ya Maliasili na Utalii bungeni jana kwa ukali, Kilufi alisema wapo watendaji mafisadi na wala rushwa wanaojali maslahi yao, ambao wanasababisha watu waadilifu walaumiwe bila sababu.

“Hapa Waziri (Nyalandu) analaumiwa bila sababu. Haya ni maamuzi ya Rais Kikwete, alikuja na Waziri Mkuu, na vikao vikafanyika na kufikia uamuzi huu. “Sasa kwa nini watu wakweli na waadilifu wanalaumiwa bila sababu? Kuna watendaji wala rushwa na mafisadi, wanachukua fedha kwa Waarabu na kusababisha matatizo haya,” alisema mbunge huyo.

Alisema watu hao wanawafahamu na kwamba wananchi wa Mbarali hawatakubali kitu kingine chochote, kwani huko nyuma watendaji hao walipewa Sh bilioni saba za kulipa fidia wananchi, lakini zikalipwa Sh bilioni mbili.

“Hawa ni watendaji wabovu wala rushwa. Hizi fedha nyingine zimekwenda wapi? Wananchi wangu wanataka fidia yao na waliochukua fedha hizi wamechukuliwa hatua gani,” alihoji Kilufi.

Alisema suala la Ihefu lilikwisha siku nyingi na kwamba wanachotaka sasa ni wananchi kulipwa fidia hiyo.

“Hatutakubali hapa, hifadhi imetukuta wananchi, watu wanachukua fedha kwa maslahi binafsi. Mbarali tutakuwa mfano. Hata kama sikupewa ulinzi, kama nikiuawa, wananchi wangu watajua mbunge wao amekufa kwa sababu gani, sitakubali,” alisema kwa ukali.

Aliungwa mkono na Mbunge wa Viti Maalumu, Riziki Lulida (CCM), aliyesema kuna viongozi wanapokea rushwa na kusababisha matatizo katika jamii.

Alisema migogoro ya mipaka na maeneo ya uhifadhi inasababishwa na viongozi wasio waadilifu, na kuhoji watu wanaoingiza mifugo katika hifadhi huku wakiwa na silaha nzito, kuwa hao si wafugaji, bali majangili.

Mbunge wa Kuteuliwa, James Mbatia (NCCR-Mageuzi), alisema ipo haja ya kuweka mazingira mazuri, tulivu na kodi zisizobadilika, ili kuongeza mapato ya utalii.

Aidha, Mbunge wa Kuteuliwa, Zakia Meghji (CCM), alipendekeza kuwapo kwa mkataba wa kubadilishana nembo ya tembo yaliyohifadhiwa na mataifa ya nje, akisema zinatumika gharama kubwa kulinda ‘tembo waliokufa’ sawa na zile zinazotumika kulinda walio hai.

Waziri huyo wa zamani wa Maliasili na Utalii alisema yapo meno ya tembo tani 137 yaliyohifadhiwa ambayo yalikataliwa kuuzwa na taasisi ya kimataifa, na kuonesha hofu kuwa siku moja yanaweza kupotea na kusababisha mawaziri wafungwe.

Naye Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa (Chadema), aliunga mkono hoja ya Meghji akisema meno hayo yanaweza kupigwa ‘dili’ kama yataendelea kuhifadhiwa

Comments

Popular posts from this blog

Rais Wa Burundu "Apinduliwa"......Ndege Yake Jana Ilishindwa Kutua Burundi na Kuamua Kurudi Tanzania

Nchini Burundi, aliyekua mkuu wa majeshi Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza Jumatano Mei 13 kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza amepinduliwa madarakani. Meja Generali Niyombareh alisema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza. Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari alisema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa. Wakati  Mapinduzi  hayo  yakitangazwa, Rais Nkurunziza alikuwa  nchini Tanzania kujumuika na viongozi wa kanda  ya Afrika Mashariki kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi tangu Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu. Baada  ya  tangazo  la  kupindulikwa  kwake, Rais  huyo  alipanda  ndege  kurejea  nchini  kwake  licha  ya  tangazo  la  kufungwa  kwa  mipaka  yote  na  viwanja  vya...

Gharama za kupima ardhi kupunguzwa

SERIKALI imesema katika mwaka ujao wa fedha itapunguza gharama za upimaji ardhi kwa zaidi ya nusu ili kuwawezesha wanachi kupima maeneo yao, hali ambayo inaonekana itapunguza migogoro ya ardhi. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi wakati wa ziara mkoani hapa kwa ajili ya kutatua migogoro ya ardhi ambayo imedumu kwa miaka mingi. Akizungumza na watendaji wa sekta mbalimbali wa mkoa wa Tabora, Waziri Lukuvi alisema Wizara itapunguza kwa zaidi ya nusu, gharama za upimaji ardhi ili kila mwananchi aweze kupima eneo lake na kupata hati ya umiliki. Lukuvi aliongeza kuwa serikali pia itaweza kukusanya kwa wingi kodi ya pango la ardhi, hivyo kuongeza mapato ambayo yataisaidia serikali katika kufanikisha shughuli za maendeleo. Pamoja na kupunguza gharama hizo, Lukuvi aliwaonya maofisa ardhi kuacha tabia ya kuendesha shughuli za serikali kwa kukiuka taratibu, akitolea mfano wa maofisa hao kupima viwanja juu ya viwanja suala ambalo limekuwa lina...

Frola Mbasha Ajiunga CHADEMA

MWIMBAJI maarufu wa nyimbo za injili nchini, Frola Mbasha ameijunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema). Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika viwanja vya Tanganyika Packers mjini Dar es Salaam jana, Mbunge wa Kawe, Halima Mdee (Chadema), alisema kuijunga kwa Mbasha katika chama hicho kutasaidia kuhamasisha wasanii wengine ambao wamekuwa wakitumiwa na Chama Chama Mapinduzi (CCM), bila kupata mafanikio. ” Idadi kubwa ya wasanii nchini, wanateseka bila ya kujijua, hii inatokana na kutumiwa na CCM bila kupata mafanikio ya aina yoyote…Frola inabidi uwaelimishe ili waweze kujiunga na chama chetu,”alisema Mdee. Naye Mwenyekiti wa Chadema,Freeman Mbowe alisema siku Serikali itakapowasilisha muswada wa Sheria wa Vyombo vya Habari bungeni, wabunge wa chama hicho na wale wanauounda Umoja wa Katiba ya Wananchi ( Ukawa) watafanya vurugu ili kuhakikisha haupiti. Alisema baadhi ya vipengele vya muswada huo vinakandamiza waandishi na wananchi kupata...