Skip to main content

Watendaji wala rushwa wanawaponza waadilifu

estus Kilufi

MBUNGE wa Mbarali, Modestus Kilufi (CCM), amesema watendaji wala rushwa na mafisadi wanasababisha mawaziri waadilifu walaumiwe bila sababu.

Ametangaza vita na watendaji hao na wawekezaji katika jimbo lake ambao wanadaiwa kutaka kuyumbisha uamuzi wa suala la mipaka kati ya wananchi na hifadhi ya Ihefu katika Hifadhi ya Ruaha mkoani Mbeya.

Hivi karibuni, Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu alitangaza kuwa wananchi wataendelea kuishi katika maeneo yao baada ya kutatuliwa kwa mgogoro wa mpaka ulikuwapo kwa muda mrefu.

Akichangia bajeti ya Wizara ya Maliasili na Utalii bungeni jana kwa ukali, Kilufi alisema wapo watendaji mafisadi na wala rushwa wanaojali maslahi yao, ambao wanasababisha watu waadilifu walaumiwe bila sababu.

“Hapa Waziri (Nyalandu) analaumiwa bila sababu. Haya ni maamuzi ya Rais Kikwete, alikuja na Waziri Mkuu, na vikao vikafanyika na kufikia uamuzi huu. “Sasa kwa nini watu wakweli na waadilifu wanalaumiwa bila sababu? Kuna watendaji wala rushwa na mafisadi, wanachukua fedha kwa Waarabu na kusababisha matatizo haya,” alisema mbunge huyo.

Alisema watu hao wanawafahamu na kwamba wananchi wa Mbarali hawatakubali kitu kingine chochote, kwani huko nyuma watendaji hao walipewa Sh bilioni saba za kulipa fidia wananchi, lakini zikalipwa Sh bilioni mbili.

“Hawa ni watendaji wabovu wala rushwa. Hizi fedha nyingine zimekwenda wapi? Wananchi wangu wanataka fidia yao na waliochukua fedha hizi wamechukuliwa hatua gani,” alihoji Kilufi.

Alisema suala la Ihefu lilikwisha siku nyingi na kwamba wanachotaka sasa ni wananchi kulipwa fidia hiyo.

“Hatutakubali hapa, hifadhi imetukuta wananchi, watu wanachukua fedha kwa maslahi binafsi. Mbarali tutakuwa mfano. Hata kama sikupewa ulinzi, kama nikiuawa, wananchi wangu watajua mbunge wao amekufa kwa sababu gani, sitakubali,” alisema kwa ukali.

Aliungwa mkono na Mbunge wa Viti Maalumu, Riziki Lulida (CCM), aliyesema kuna viongozi wanapokea rushwa na kusababisha matatizo katika jamii.

Alisema migogoro ya mipaka na maeneo ya uhifadhi inasababishwa na viongozi wasio waadilifu, na kuhoji watu wanaoingiza mifugo katika hifadhi huku wakiwa na silaha nzito, kuwa hao si wafugaji, bali majangili.

Mbunge wa Kuteuliwa, James Mbatia (NCCR-Mageuzi), alisema ipo haja ya kuweka mazingira mazuri, tulivu na kodi zisizobadilika, ili kuongeza mapato ya utalii.

Aidha, Mbunge wa Kuteuliwa, Zakia Meghji (CCM), alipendekeza kuwapo kwa mkataba wa kubadilishana nembo ya tembo yaliyohifadhiwa na mataifa ya nje, akisema zinatumika gharama kubwa kulinda ‘tembo waliokufa’ sawa na zile zinazotumika kulinda walio hai.

Waziri huyo wa zamani wa Maliasili na Utalii alisema yapo meno ya tembo tani 137 yaliyohifadhiwa ambayo yalikataliwa kuuzwa na taasisi ya kimataifa, na kuonesha hofu kuwa siku moja yanaweza kupotea na kusababisha mawaziri wafungwe.

Naye Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa (Chadema), aliunga mkono hoja ya Meghji akisema meno hayo yanaweza kupigwa ‘dili’ kama yataendelea kuhifadhiwa

Comments

Popular posts from this blog

Mnyukano urais chama cha walimu

a Gratian Mukoba. MCHUANO mkali umeibuka ndani ya Chama cha Walimu Nchini (CWT) baada ya wagombea 28 kujitosa kuwania Urais wa chama hicho chenye nguvu kutokana na kuundwa na idadi kubwa ya watumishi wa umma. Miongoni mwa wanaogombea ni rais wa sasa wa chama hicho, Gratian Mukoba ambaye pia Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Nchini (TUCTA). Uchaguzi huo unatarajiwa kufanyika Alhamisi wiki hii kwenye Ukumbi wa hoteli ya Ngurdoto, Arumeru mkoani Arusha siku ambayo itakuwa inahitimisha mkutano mkuu wa siku tatu wa chama hicho unaotarajiwa kufunguliwa kesho na Rais Jakata Kikwete. Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya chama hicho, Kanda ya Ziwa imeongoza kwa kutoa wagombea wengi wakiwemo wa mkoa wa Mwanza, Kaliyaya Masunga wa Ilemela, Magesa Kirati wa Kwimba, Marwa D. Marwa wa Nyamagana na Mashauri Benedict kutoka Sengerema. Wengine wa Kanda ya Ziwa ni Charles George wa Geita, Godi Kiduma, Lyangombe Dotto na Malimi Macheyeki kutoka Maswa mkoani Simiyu na Juma Boniface wa Bund...

Aunty Ezekiel ajifungua mtoto wa kike, amuita Cookie

Muigizaji wa filamu za Bongo, Aunty Ezekiel amejifungua mtoto wa kike siku ya Alhamis May 21. Mtoto huyo wa Aunty Ezekiel ambaye baba yake ni dancer wa Diamond aitwaye Mose Iyobo, amepewa jina la Cookie. Aunty ameshare habari hiyo na mashabiki wake wa Instagram: “Amin ktk Mungu ndio Mwisho wa Matatizo yote yaliyotuzunguka Hakuna mganga wala Mchawi pasipo Mungu. "Ahsante Mungu wang kwa kunikabidhi zawadi yang Asubuhi jana tar 21-05-2015 Muache yy atende kwani ndio nguzo yetu sote Nasema Ahsante tena Ahsante kwa zawadi hii kubwa ktk Maisha kwani ilikuwa ni kipindi kigumu chenye majaribu ya kila aina kupitia binaadamu wajizaniao wao ni miungu watu Bac endelea kunyoosha mkono wako ktk paji la kiumbe wako ukiwa kama kinga nami niwe kivuli tuu juu yake Amen Whn Jesus Say Yes Ni body can Say wht!!!!!!!Wlcm Baby Cookie wlcm 2 da world KIBOKO YANG…” Diamond ambaye ni uncle wa Cookie pia amempongeza Aunty na Mose kupitia Instagram: “Hongera sana @auntyezekiel na @...

Tanzanian Irene Kiwia Wins Woman of The Year Africa Award.

Africa Reconnect (http://www.africareconnect.com), a platform for women who have made remarkable contributions to the growth and development of the various nations in Africa has today awarded 11 Africans whose contributions to women empowerment in their countries is outstanding. The award ceremony, which took place in Polokwane, Limpopo South Africa, concluded a two day empowerment conference themed “ Accelerating Positive Change”. The 2015 awards recipient included; Seja Lorraine Semenya for best Cultural Developer in Africa, Dr. K. S Malukele for Best Community Developer in Africa, Mphatheleni Makaulele for Most Inspiring Woman in Africa, all from South Africa. The first lady of Akwibo State for Best Philanthropic in Africa and Irene Kiwia from Tanzania won Woman of the Year Africa award.