MSAFARA wa Makongoro Nyerere, mtoto wa Baba wa Taifa, hayati Mwalimu Julius Nyerere, umepata ajali wakati mwanasiasa huyo akiwa katika harakati za kutimiza masharti ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya kutafuta wadhamini ili aweze kuwania nafasi ya urais.
Ajali hiyo iliyojeruhi watu watano waliokuwa kwenye msafara huo, ilitokea jana katika eneo la Tekniko, Wilaya ya Kasulu, mkoani Kigoma baada ya gari aina ya Land Cruiser lenye namba T 188 BXG walilokuwamo kupinduka.
Akithibitisha kutokea kwa ajali hiyo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kigoma, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Ferdinand Mtui, alisema ilitokea saa 10:30 asubuhi wakati msafara huo ukiongozwa na Makongoro ukielekea Kigoma mjini.
Kamishna Mtui aliwataja waliojeruhiwa sehemu mbalimbali za mwili ikiwamo kichwani na mabegani kuwa ni dereva wa gari hilo Julius Kambarage, ambaye ni mtoto wa Makongoro na mwandishi Evans Magege.
Wengine ni Katibu Mwenezi wa CCM, Musoma Mjini, Fikiri Marumba na Ally Tesha ambao wote walipatiwa matibabu katika Hospitali ya Wilaya ya Kasulu na kuendelea na msafara.
Majeruhi mwingine ni Cyprian Msiba ambaye ni mwandishi wa kituo cha Televisheni cha Channel Ten ambaye alibaki hospitalini hapo kwa ajili ya huduma ya X-Ray kutokana na kuumia sehemu za bega.
Makongoro ambaye ni mbunge wa Afrika Mashariki, anazunguka mikoa mbalimbali nchini kwa nia ya kutafuta wadhamini ili kuomba ridhaa ya CCM kumpitisha kugombea nafasi ya urais.
a Gratian Mukoba. MCHUANO mkali umeibuka ndani ya Chama cha Walimu Nchini (CWT) baada ya wagombea 28 kujitosa kuwania Urais wa chama hicho chenye nguvu kutokana na kuundwa na idadi kubwa ya watumishi wa umma. Miongoni mwa wanaogombea ni rais wa sasa wa chama hicho, Gratian Mukoba ambaye pia Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Nchini (TUCTA). Uchaguzi huo unatarajiwa kufanyika Alhamisi wiki hii kwenye Ukumbi wa hoteli ya Ngurdoto, Arumeru mkoani Arusha siku ambayo itakuwa inahitimisha mkutano mkuu wa siku tatu wa chama hicho unaotarajiwa kufunguliwa kesho na Rais Jakata Kikwete. Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya chama hicho, Kanda ya Ziwa imeongoza kwa kutoa wagombea wengi wakiwemo wa mkoa wa Mwanza, Kaliyaya Masunga wa Ilemela, Magesa Kirati wa Kwimba, Marwa D. Marwa wa Nyamagana na Mashauri Benedict kutoka Sengerema. Wengine wa Kanda ya Ziwa ni Charles George wa Geita, Godi Kiduma, Lyangombe Dotto na Malimi Macheyeki kutoka Maswa mkoani Simiyu na Juma Boniface wa Bund...
Comments
Post a Comment