Skip to main content

Serikali na wafanyabiashara wafikia mwafaka EFDs

SERIKALI na wafanyabiashara nchini wamefikia mwafaka juu ya matumizi ya mashine za kielektroniki (EFDs), kuendelea huku ikiendelea kuondoa vikwazo mbalimbali vilivyojitokeza, ikiwa ni pamoja na ukokotoaji wa gharama za mfanyabiashara.

Mwafaka huo ulifikiwa baada ya Kamati ya Kitaifa, iliyoundwa kwa ajili ya kupitia na kubainisha changamoto mbalimbali kuhusu mashine hizo.

Mapendekezo ya kamati yalihusu kuongeza uwazi katika mfumo mzima wa kodi kwa mizigo itokayo nje ya nchi, kuanzia mchakato wa uthaminishaji na uondoshaji wa mizigo bandarini, utambuzi wa gharama za manunuzi ndani ya nchi na gharama za uendeshaji zisizotambulika kisheria kwa kutokuwa na stakabadhi.

Akizungumza jana Dar es Salaam mbele ya Kamati na Viongozi wa Jumuiya ya Wafanyabiashara nchini, Waziri wa Fedha, Saada Mkuya alisema baada ya kuanzishwa, utaratibu wa kutumika kwa mashine hizo, ulikutana na changamoto mbalimbali zilizosababisha kuibuka kwa malalamiko na migogoro katika jamii.

Alisema chini ya mwafaka huo, utasaidia kukusanywa kwa kodi kwa ufanisi, ikiwa ni katika kuingizwa kwa gharama za wafanyabiashara katika mashine hizo.

Mkuya alisema mashine hizo hazikuwa na tatizo, lakini mfumo mzima wa utumikaji wake ndio uliokuwa na changamoto kwa wafanyabiashara, ambapo suala la ukadiriaji nalo linafanyiwa kazi.

Alisema baada ya kufikiwa kwa muafaka huo, matumizi ya mashine hizo utaanza kukokotoa gharama za mfanyabiashara huku kukiwa na bidhaa 150, ambazo zitaainishwa gharama halisi za bidhaa hizo.

“Kule bandarini kumekuwepo na baadhi ya wakala wa kupakua mizigo bandarini ambao sio waaminifu ambao hujikuta wakitoa viwango tofauti vya gharama kwa wafanyabiashara pindi wanapokuwa wakikomboa mizigo yao,” alisema Mkuya na kuongeza kuwa mfanyabiashara hujikuta akipatiwa risiti tofauti na kiwango halisi kinachotakiwa.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara, Johnson Minja alisema kupitia mwafaka huo, uwazi na uwajibikaji katika matumizi za mashine hizo, utawekwa wazi, lengo likiwa ni kuongeza ufanisi wa ukusanyaji wa kodi

Comments

Popular posts from this blog

Rais Wa Burundu "Apinduliwa"......Ndege Yake Jana Ilishindwa Kutua Burundi na Kuamua Kurudi Tanzania

Nchini Burundi, aliyekua mkuu wa majeshi Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza Jumatano Mei 13 kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza amepinduliwa madarakani. Meja Generali Niyombareh alisema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza. Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari alisema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa. Wakati  Mapinduzi  hayo  yakitangazwa, Rais Nkurunziza alikuwa  nchini Tanzania kujumuika na viongozi wa kanda  ya Afrika Mashariki kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi tangu Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu. Baada  ya  tangazo  la  kupindulikwa  kwake, Rais  huyo  alipanda  ndege  kurejea  nchini  kwake  licha  ya  tangazo  la  kufungwa  kwa  mipaka  yote  na  viwanja  vya...

Diamond Amuita Jokate Makombo...."Mwacheni Ali Kiba Ajilie Makombo"

Mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ amemuita mpenzi wake wa zamani Jokate Mwegelo kuwa ni makombo na kudai kama zilipendwa huyo anatembea na hasimu wake Ali Kiba, hakuna jipya kwani anakula makombo. Diamond ametoa kauli hiyo Jumatano iliyopita wakati mwanahabari wetu alipotaka kujua anajisikiaje kuona wapenzi wake wa zamani Jokate na Wema Sepetu ‘Madam’ wanamuunga mkono Ali Kiba. Pamoja na kudaiwa kuwa Jokate ana uhusiano wa ‘kimalovee’ na Ali Kiba na mwenyewe kutokubali, ameungana na Wema kuendesha kampeni ya nguvu kwenye mitandao ya kijamii kuhamasisha watu wampigie kura Kiba kwenye Tuzo za Kili 2015 kwa kile kinachoelezwa kuwa ni kampeni ya kuuangusha ufalme wa Diamond kimuziki. Baada ya mwanahabari wetu kuujua ‘mchezo huo’ uliopamba moto kama moto wa kifuu mitandaoni ndipo alipomuuliza Diamond anauzungumziaje ambapo kwanza alikiri kuufahamu na kudai ameudharau maana hauna jipya. “Hamna jipya waache waendelee kumpigia...

Gharama za kupima ardhi kupunguzwa

SERIKALI imesema katika mwaka ujao wa fedha itapunguza gharama za upimaji ardhi kwa zaidi ya nusu ili kuwawezesha wanachi kupima maeneo yao, hali ambayo inaonekana itapunguza migogoro ya ardhi. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi wakati wa ziara mkoani hapa kwa ajili ya kutatua migogoro ya ardhi ambayo imedumu kwa miaka mingi. Akizungumza na watendaji wa sekta mbalimbali wa mkoa wa Tabora, Waziri Lukuvi alisema Wizara itapunguza kwa zaidi ya nusu, gharama za upimaji ardhi ili kila mwananchi aweze kupima eneo lake na kupata hati ya umiliki. Lukuvi aliongeza kuwa serikali pia itaweza kukusanya kwa wingi kodi ya pango la ardhi, hivyo kuongeza mapato ambayo yataisaidia serikali katika kufanikisha shughuli za maendeleo. Pamoja na kupunguza gharama hizo, Lukuvi aliwaonya maofisa ardhi kuacha tabia ya kuendesha shughuli za serikali kwa kukiuka taratibu, akitolea mfano wa maofisa hao kupima viwanja juu ya viwanja suala ambalo limekuwa lina...