Skip to main content

Posts

Showing posts from April, 2015

ITV kuonesha tuzo za muziki za Kili

WAKATI homa za wasanii mbalimbali juu ya shindano la Kilimanjaro Tanzania Music Awards (KTMA) zikizidi kupanda, wadhamini wa shindano hilo, Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia bia yake ya Kilimanjaro Premium Lager, imeandaa kipindi cha runinga kitakachozungumzia juu ya tuzo hizo. Hayo yamesemwa Dar es Salaam na Meneja wa bia ya Kilimanajro Premium Lager, Pamela Kikuli, na kueleza kuwa kipindi hichi kitaitwa ‘Kili Chats.’ Alisema sio mara ya kwanza kwa bia hiyo kuandaa kipindi cha aina hii kwani mwaka jana kilirushwa wakati wa msimu wa ‘Nani Mtani Jembe’, kampeni inayowashirikisha wakongwe wa soka hapa nchini Simba na Yanga. Meneja huyo alisema sasa hivi wameamua kujikita katika muziki kwani ndio msimu wa KTMA kwa hivyo wanataka kusikia kutoka kwa wananchi kuhusu maoni yao. “Huu ni mwanzo mzuri kuelekea KTMA ambapo tutaalika wadau mbalimbali kwa mfano Ma DJ, wanamitindo, washiriki katika video mbalimbali na wengine,” alisema Pamela. Alisema kipi...

Maandamano mapya Baltimore Marekani

Kumetokea maandamano mapya nchini Marekani katika mji wa Baltimore kufuatia kifo cha kijana mweusi Freddie Gray aliyekufa kutokana na majeraha akiwa mikononi mwa polisi. Mamia ya watu wameandamana katika mitaa, wakionyesha ujasiri licha ya hali mbaya ya hewa iliyokuwepo. Matokeo ya mwanzo ya uchunguzi wa polisi wa jinsi kijana wa miaka ishirini na mitano mwenye asili ya weusi alivyouawa bado hayajawekwa hadharani. Maandamano

Vyama vyakataa msajili kusuluhisha migogoro

vimeiomba Ofisi ya Msajili wa Vyama isihusike kutatua migogoro ya ndani ya vyama kwa kuwa jukumu hilo ni la ndani ya vyama husika vyenye miongozo ya kuitatua. Badala yake, wameitaka ofisi hiyo ishughulike na utatuzi wa migogoro ya vyama inayohusisha chama kimoja na kingine, kwa sababu ndio wanayoamini kuwa inahitaji mtu wa pembeni wa kusimamia na kuongoza utatuzi. Akizungumza katika mkutano wa mashaurino ya wadau wa vyama vya siasa na ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, uliodhaminiwa na Shirika la Kimataifa la Maendeleo (UNDP), kwa lengo la kutafuta njia ya kufikia uchaguzi mkuu wa amani, Mwenyekiti wa chama cha Alliance for Tanzania Farmers (AFP), Said Sudi Said alisema. Katika hatua nyingine Serikali imeombwa iiwezeshe ofisi hiyo kwa kuitengea bajeti ya kutosha isikwame kuendeleza jukumu lake la kuvipa vyama vya siasa uwezo wa kuendelea kuishi, kwa kuwa ndio mlezi anayetegemewa. Kaimu Katibu Mkuu wa UDP, Isaack Cheyo alisema Ofisi ya Msajili ikiwezeshwa kifedha na kupatiwa watum...

Yanga yaenda Tunisia na matumaini kibao

MSAFARA wa watu 50 wa timu ya Yanga umeondoka nchini jana saa 5 usiku kwenda Tunisia kwa ajili ya mchezo wa hatua ya 16 bora wa michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Etoile du Sahel uliopangwa kupigwa Jumamosi usiku kwenye mji wa Sousse. Katika msafara huo, Yanga imeondoka na kikosi cha wachezaji 20 kwa kutumia ndege ya Shirika la Ndege la Emirates kupitia Dubai kabla ya kwenda Tunisia, ambako ndipo yalipo makazi ya wapinzani wao Etoile. Akizungumza na gazeti hili, kocha wa Yanga Hans van der Pluijm alisema wanakwenda Tunisia wakiwa na matumaini makubwa ya kupata ushindi kutokana na maandalizi mazuri waliyoyafanya hapa nchini ambayo anaamini yatawasaidia katika mchezo huo. “Ni mchezo mgumu kutokana na ubora wa wapinzani wetu, lakini hilo haliwezi kututisha na kukubali kirahisi tumejizatiti kuhakikisha tunapambana na kupata ushindi kama ambavyo wao walipata sare nyumbani,” alisema Pluijm. Pluijm alisema watahakikisha wanatumia mfumo wao waliozoea kucheza siku zo...

Mwenyekiti aliyefungwa miaka 15 aachiwa

KIJIJI cha Msitu wa Mbogo wilayani Arumeru mkoani Arusha, jana kililipuka kwa furaha baada ya viongozi wanne wa kijiji hicho, akiwemo mwenyekiti, kuachiwa huru kwa dhamana na Mahakama. Waliachiwa baada ya siku 20 za vilio, simanzi na majonzi za wakazi wa kijiji hicho kuhusu suala la viongozi hao. Viongozi hao, Mwenyekiti wa Kijiji, Ernest Mkilanyi na wajumbe wake wanne, walihukumiwa jumla ya miaka 75 jela hivi karibuni kwa unyang’anyi wa Sh 780,000. Kila mtu alihukumiwa miaka 15 jela. Kuachiwa kwa dhamana kwa viongozi hao kunatokana na juhudi za Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Husna Mwilima na Kamati yake ya Ulinzi na Usalama katika kushughulikia rufaa dhidi ya hukumu hiyo, iliyotolewa na Hakimu John Mwita wa Mahakama ya Mwanzoya Mbuguni/Maji ya Chai . Mwilima aliwaahidi wananchi hao, walipoandamana hadi ofisini kwake Aprili 10 mwaka huu kupinga hukumu hiyo na kumuomba kuwapatia tena viongozi wao kwa kuwarejesha uraiani. Akizungumza jana katika mkutano wa hadhara na mapokezi ya mwe...

Mahakama yamkamua mbunge matunzo ya mtoto

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imemuamuru Mbunge wa Jimbo la Dimani Zanzibar, Abdallah Sharia Ameir (CCM) kutoa Sh 200,000 kila mwezi kwa ajili ya matunzo ya mtoto wake wa kiume, mwenye umri wa miaka mitatu na nusu, anayedaiwa kumtelekeza. Pamoja na amri hiyo, Hakimu Mkazi, Hellen Liwa alisema mbunge huyo atatoa kiasi hicho cha fedha kuanzia siku alipokoma kutoa matunzo na matibabu kwa mtoto huyo, anayetajwa kuwa ni mlemavu. Pia, aliamuru mtoto huyo kulelewa na wazazi wake na siyo bibi yake, kama alivyokuwa akitaka mbunge huyo. Hivyo ataendelea kukaa na mama yake. Kwa upande wake, Wakili Gideon Mandes aliyekuwa akimtetea Hawa Deus aliyekuwa mke wa mbunge huyo, alisema kupitia hukumu hiyo Mahakama imetoa uamuzi wa haki. “Kupitia hukumu hii nimebaini wazazi wanawajibu wa kumtunza mtoto wanayemzaa bila ya kujali hali yake hata kama ni ya ulemavu asitelekezwe na imedhihirisha hakuna mtu aliye juu ya sheria na kwamba sheria ipo sawa kwa kila mtu,”alisema wakili huyo. Wakili...

Sumatra kiini cha ajali barabarani

WAZIRI wa Uchukuzi, Samuel Sitta amesema ajali za barabarani zinachangiwa na uzembe wa taasisi inayosimamia sekta ya usafiri jambo linalogharimu maisha ya watu wasio na hatia, na kuitaka taasisi hiyo kuchukua hatua na kuhakikisha nidhamu inarejea kwenye sekta hiyo. Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA) ndiyo yenye dhamana ya kusimamia na udhibiti wa sekta ya usafiri katika nchi kavu na majini. Sitta aliyasema hayo jana jijini Dar es Salaam alipozungumza na waandishi wa habari wakati Kamati ya Bunge ya Miundombinu ilipokuwa ikizungumza na viongozi wa wizara hiyo. Sitta alisema “Hakuna kitu kinachoniuma kama ajali za barabarani ambazo nyingi zinasababishwa na uzembe, ubovu wa magari na matairi ya mtumba, halafu baya zaidi ni kwamba Mamlaka husika ya kudhibiti vyombo hivyo ipo, inaona na kuwasamehe makosa,” alisema Sitta. Aliongeza, mamlaka husika zina wajibu wa kusimamia vyombo hivyo na kuhakikisha vile vinavyofanya makosa vinachukuliwa hatua ikiw...

Kili Music Award 2015

Tanroads yaagizwa kukabidhi barabara kwa DART

Magufuli ameagiza Wakala wa Barabara nchini (TANROADS) kukabidhi maeneo ya barabara yaliyokamilika ya mradi wa barabara wa mabasi yaendayo kasi kwa Wakala wa Usafiri Haraka wa Mabasi(DART) ili yaanze kutumiwa na wananchi. Aidha ameiagiza kampuni inayojenga mradi huo ya Strabag kufanya kazi usiku na mchana ili kukamilisha mradi huo haraka ambapo hadi sasa umekamilika kwa asilimia 90. Dk Magufuli aliyasema hayo jana Dar es Salaam baada ya kukagua ujenzi wa miundombinu ya mabasi yaendayo haraka (BRT) kutoka Morocco - Magomeni - Fire hadi Kariakoo na kuweka jiwe la msingi katika Barabara ya Uhuru. Pia aliiagiza DART kuhakikisha mchakato wa kupata magari ili wanapokabidhiwa barabara hizo magari yaanze kufanya safari badala ya kupoteza muda mwingine wa kusubiri mabasi. Alisema Dar es Salaam ni Mkoa ambao unatekeleza miradi mingi ya miundombinu ambapo kwa miradi inayotekelezwa kwa sasa na inayotarajiwa kujengwa inakaribia thamani ya Sh trilioni nne. Alisema katika mradi wa barabara za ju...

Chelsea yaichapa Leicester City 3 -1

Vigogo watumia Fedha za Kulipia Madeni ya Walimu Kujenga Maabara kutimiza Agizo la Rais Kikwete Posted

Askari shupavu wa kike atunukiwa nishani.

Sumatra wasitisha nauli mpya kwa siku 14

Mwanafunzi auawa baada ya kukutwa na barua ya mapenzi

Serikali yatangaza mikakati ya kuimarisha shilingi

Majambazi Matatu (3) Yauawa na Jeshi la Polisi Mkoani Kigoma

Majambazi Matatu (3) Yauawa na Jeshi la Polisi Mkoani Kigoma

Waganga wajitolea kumtibu Wema

Waganga wajitolea kumtibu Wema Sepetu

Escrow yampa tuzo Kafulila

Escrow yampa tuzo Kafulila >Sakata la uchotwaji wa fedha katika Akaunti ya Tegeta Escrow limemng’arisha Mbunge wa Kigoma Mbunge wa Kigoma Kusini (NCCR Mageuzi), David Kafulila akikabidhiwa Tuzo ya utetezi wa haki za binadamu ya mwaka 2014, Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Tom Nyanduga, Dar es Salaam jana.  Kulia ni Mwenyekiti wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu nchini, Martina Kabisama. Picha na Kelvin Matandiko ADVERTISEMENT Dar es Salaam. Sakata la uchotwaji wa fedha katika Akaunti ya Tegeta Escrow limemng’arisha Mbunge wa Kigoma Kusini (NCCR- Mageuzi),  David Kafulila baada ya kutunukiwa tuzo ya kutambua mchango wake katika kufichua ufisadi huo uliohusisha uchotwaji wa Sh306 bilioni kutoka Benki Kuu ya Tanzania (BoT). Katika sakata hilo, mawaziri wawili walipoteza nyadhifa zao pamoja na Mwanasheria Mkuu wa Serikali baada ya Ripoti ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali kuwahusisha na sakata hilo. Maofisa wengine kadhaa wa S...