Skip to main content

Posts

Showing posts from May, 2015

Gharama za kupima ardhi kupunguzwa

SERIKALI imesema katika mwaka ujao wa fedha itapunguza gharama za upimaji ardhi kwa zaidi ya nusu ili kuwawezesha wanachi kupima maeneo yao, hali ambayo inaonekana itapunguza migogoro ya ardhi. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi wakati wa ziara mkoani hapa kwa ajili ya kutatua migogoro ya ardhi ambayo imedumu kwa miaka mingi. Akizungumza na watendaji wa sekta mbalimbali wa mkoa wa Tabora, Waziri Lukuvi alisema Wizara itapunguza kwa zaidi ya nusu, gharama za upimaji ardhi ili kila mwananchi aweze kupima eneo lake na kupata hati ya umiliki. Lukuvi aliongeza kuwa serikali pia itaweza kukusanya kwa wingi kodi ya pango la ardhi, hivyo kuongeza mapato ambayo yataisaidia serikali katika kufanikisha shughuli za maendeleo. Pamoja na kupunguza gharama hizo, Lukuvi aliwaonya maofisa ardhi kuacha tabia ya kuendesha shughuli za serikali kwa kukiuka taratibu, akitolea mfano wa maofisa hao kupima viwanja juu ya viwanja suala ambalo limekuwa lina...

Hotuba ya Mh. Steven Wassira Aliyoitoa Leo Jijini Mwanza Wakati Akitangaza Nia ya Kugombea Urais wa Tanzania Kupitia CCM

Nianze kwa kutoa shukrani kwenu wote mlioacha shughuli zenu ili kuja hapa kunisikiliza. Kuja kwenu hapa kwa wingi ni ishara ya imani mliyonayo kwangu, Nawashukuru sana     Kwa zaidi ya mwaka mzima, kumekuwepo na miningo’no kuhusu uwezekano wangu kugombea urais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Aidha kutokana na mijadala ya wananchi au kupitia mitandao ya kijamii au vyombo rasmi vya habari, mining’ono hiyo imefanya baadhi ya watu wanifuate ili wanishauri nigombee na wengine wamenipigia simu kwa kunishawishi nisisite kugombea     Leo, nakuja hapa Mwanza kuvunja ukimya na kumaliza minong’ono kwa kutangaza rasmi kwamba nimekata shauri kugombea nafasi ya urais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania KWANINI NAGOMBEA Zikosababu kadhaa, ambazo zimenisukuma kugombea kufikia uamuzi huo     Haki yangu ya kikatiba. Hii ni sababu ya msingi lakini siyo yenye uzito, kwa vile ni haki ya kikatiba na ni kwa ajili ya watanzania wote. Hivyo...

Nancy Sumary na Dada Yako Nakaya Kunani ? Je ni Kweli Kuna Beef Kati ya Hawa Ndugu Wawili?

Nasikia Habari ya Mjini ni kuwa Hawa Ndugu wawili wa Damu Nancy Sumary na Dada yake Nakaya Kwa sasa Haziivi Hata Kidogo...Je Kunani Ama ni Uzushi tu ...Embu kwa Anaye jua A-Z atujuze....Maana Sitaki Kuamini Jinsi walivyokuwa wanapendana..eti sasa kila mtu kivyake.... Udaku Special Blog

Baada ya Jana Lowassa Kutangaza nia Urais 2015..January Makamba Nae Aja na Mpya

Tume ya taifa ya uchaguzi imeshatangaza kwamba uchaguzi mkuu utafanyika October 2015 ambapo sasa ni headlines zake zinachukua nafasi kwa watu mbalimbali kutangaza nia za kugombea nafasi ya juu ya Urais. Post hii inamilikiwa na January Makamba ambae ni Mbunge wa Bumbuli Tanga na anautaka Urais pia ambapo May 30 2015 aliandika :      ‘Wiki ijayo tutataarifu ni lini na kwa namna gani tutazungumza na Watanzania, kuchukua fomu, kuanza safari za mikoani kukutana na Watanzania‘ Udaku

Mrembo Jokate Amlipua Diamond, Ni Baada ya Kuitwa 'Makombo'

Jino kwa jino! Sexy lady anayefanya poa na ngoma yake ya Leo Leo, Jokate Mwegelo ‘Kidoti’, amemlipua aliyewahi kuwa mwandani wake, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ ambaye hivi karibuni alimwita makombo baada ya kusikia kwa sasa anatoka kimalovee na msanii Ali Kiba. Akizungumza na gazeti namba moja la mastaa Bongo, Ijumaa Wikienda, wikiendi iliyopita, Jokate alisema alishangazwa na maneno hayo ambayo hakustahili kuyatamka kwani kama ni ishu ya mtu kula makombo mbona hata yeye ni makombo na bado anakula makombo? “Sijapendezwa na kauli ya Diamond na namshangaa sana, sijajua nini kimemkuta maana mimi sijamtaka wala hakuna ambapo niliwahi kumwambia kuwa ninatoka  au ninamtaka Kiba, zaidi ya maneno ya watu kwenye mitandao ya kijamii. “Hata kama hilo lipo, bado sioni maana ya neno makombo kwani hata yeye ni makombo na anakula makombo kwa Zari (Zarinah Hassan) kwani nani asiyejua?” alihoji Jokate akionekana kuchukizwa na kauli hiyo ya Diamond na ...

Diamond awapa somo wenzake

NYOTA wa muziki wa bongo flava nchini, Diamond Platinumz amewataka wasanii wa Tanzania kusambaza nyimbo zao kwa njia ya teknolojia ili kunufaika na jasho lao. Diamond aliyasema hayo wakati akizindua teknolojia ya muziki ili kuziingiza sokoni kazi zake baada ya kushauriana na wadau anaoshirikiana nao kikazi ambayo pia yeye ni balozi anayeitangaza. Amesema sababu kubwa iliyomsukuma kufanya biashara ya muziki kupitia progamu hii ni kwamba nyimbo zake ziweze kuwafikia mashabiki wake popote na muda wowote kwa urahisi kupitia simu zao za mkononi na anakuwa na uhakika wa kupata mapato tofauti na zinavyosambazwa na wasambazaji wa mtaani. “Duniani kuna ushindani katika nyanja zote, hivyo sisi wanamuziki wa Tanzania tunapaswa kuhakikisha tunatoa muziki wa viwango vya juu kuhakikisha tunalenga zaidi katika masoko ya ndani na nje kama wenzetu wanavyofanya kusambaza kazi zao kupitia kampuni zinazotumia teknolojia ya kisasa na kumnufaisha msanii. “Kuna umuhimu mkubwa wa kujiamini, kuf...

Afungwa miaka 30 kwa kumbaka mtoto wa miaka tisa

Mkazi wa Malampaka mkoani Simiyu, Benedictor Bulobo (30) , ametupwa gerezani atakakotumikia kifungo kwa miaka 30 baada ya kupatikana na hatia ya kumbaka binti wa miaka tisa. Alihukumiwa  na Mahakama ya Wilaya ya Maswa juzi na Hakimu Mwandamizi Mfawidhi  Agatha Chigulu, baada ya kuridhishwa  na ushahidi uliotolewa na upande wa mashtaka. Akitoa hukumu hiyo hakimu huyo alisema kuwa anatoa adhabu hiyo ili kukomesha vitendo hivyo na kuwaonya wenye nia  mbaya ya kutaka kutenda kosa kama hilo wajifunze na kuacha mwenendo huo. Chigulu alieleza kuwa kosa hilo ni kinyume na kifungu cha 131 cha sheria ya kanuni ya adhabu sura ya 16 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2012. Awali mahakama iliambiwa na  Mwendesha Mashitaka wa Polisi, Nassibu Swedy kuwa mshitakiwa alitenda kosa hilo Februari 23 mwaka jana  saa 5:00 asubuhi. Alimnajisi mtoto huyo  maeneo ya nyumbani kwake baada ya kumkamata  kwa nguvu binti huyo mwanafunzi wa darasa la kwanza katika Shule ya M...

StarTimes kuonesha Kombe la Dunia U20

0 Written by Hellen Mlacky Hits: 6 WAPENZI wa soka nchini sasa watafaidi kwa kutazama michuano ya Kombe la Dunia chini ya miaka 20 mwaka 2015 moja kwa moja kwenye runinga zao kupitia ving’amuzi vya StarTimes. Michuano hiyo ambayo itaanza kutimua vumbi Mei 30 na kumalizika Juni 20 mwaka huu, itaoneshwa moja kwa moja kutoka nchini New Zealand, ambapo timu 24 za vijana kutoka mataifa mbalimbali duniani yatachuana kuwania ubingwa. Akizungumza baada ya kupata haki miliki kutoka kwa FIFA za kutangaza michuano hiyo maarufu duniani ambayo hubeba mastaa wa baadae kwa timu zao za taifa, Makamu wa Rais wa StarTimes Tanzania, Zuhura Hanif alisema kuwa wana furaha kubwa kuonesha michuano hiyo kwani soka ni mchezo unaopendwa zaidi duniani. Wapenzi wa soka wataweza kujionea mechi 52 kutoka timu 24 tofauti, ambapo mchezo wa kwanza utapigwa leo Mei 30 kwa kuwakutanisha wenyeji New Zealand na Ukraine.

Diamond awapa somo wenzake

Written by Rahel Pallangyo Hits: 32 NYOTA wa muziki wa bongo flava nchini, Diamond Platinumz amewataka wasanii wa Tanzania kusambaza nyimbo zao kwa njia ya teknolojia ili kunufaika na jasho lao. Diamond aliyasema hayo wakati akizindua teknolojia ya muziki ili kuziingiza sokoni kazi zake baada ya kushauriana na wadau anaoshirikiana nao kikazi ambayo pia yeye ni balozi anayeitangaza. Amesema sababu kubwa iliyomsukuma kufanya biashara ya muziki kupitia progamu hii ni kwamba nyimbo zake ziweze kuwafikia mashabiki wake popote na muda wowote kwa urahisi kupitia simu zao za mkononi na anakuwa na uhakika wa kupata mapato tofauti na zinavyosambazwa na wasambazaji wa mtaani. “Duniani kuna ushindani katika nyanja zote, hivyo sisi wanamuziki wa Tanzania tunapaswa kuhakikisha tunatoa muziki wa viwango vya juu kuhakikisha tunalenga zaidi katika masoko ya ndani na nje kama wenzetu wanavyofanya kusambaza kazi zao kupitia kampuni zinazotumia teknolojia ya kisasa na kumnufaisha msanii. ...

Watendaji wala rushwa wanawaponza waadilifu

estus Kilufi MBUNGE wa Mbarali, Modestus Kilufi (CCM), amesema watendaji wala rushwa na mafisadi wanasababisha mawaziri waadilifu walaumiwe bila sababu. Ametangaza vita na watendaji hao na wawekezaji katika jimbo lake ambao wanadaiwa kutaka kuyumbisha uamuzi wa suala la mipaka kati ya wananchi na hifadhi ya Ihefu katika Hifadhi ya Ruaha mkoani Mbeya. Hivi karibuni, Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu alitangaza kuwa wananchi wataendelea kuishi katika maeneo yao baada ya kutatuliwa kwa mgogoro wa mpaka ulikuwapo kwa muda mrefu. Akichangia bajeti ya Wizara ya Maliasili na Utalii bungeni jana kwa ukali, Kilufi alisema wapo watendaji mafisadi na wala rushwa wanaojali maslahi yao, ambao wanasababisha watu waadilifu walaumiwe bila sababu. “Hapa Waziri (Nyalandu) analaumiwa bila sababu. Haya ni maamuzi ya Rais Kikwete, alikuja na Waziri Mkuu, na vikao vikafanyika na kufikia uamuzi huu. “Sasa kwa nini watu wakweli na waadilifu wanalaumiwa bila sababu? Kuna watendaji ...

Safari Ya Matumaini ya Edward Lowassa Itaanza Rasmi Jumamosi Hii Jijini Arusha......Watanzania Wote Mnakaribishwa

Safari  Ya  Matumaini  ya  Edward  Lowassa  Itaanza  Rasmi   Jumamosi    Hii  Jijini  Arusha......Watanzania  Wote  Mnakaribishwa. Tarehe: 30.05.2015 Mahali:  Uwanja  wa  Sheikh  Amri  Abeid- Arusha Muda:   Kuanzia  Saa 8 Mchana  hadi  saa 11 Jion

Serikali kujenga barabara za mkoa mmoja mmoja

SERIKALI imesema baada ya kukamilisha ujenzi wa barabara zinazounganisha mikoa mbalimbali nchini, itashughulikia barabara za mkoa mmoja mmoja. Naibu Waziri wa Ujenzi, Gerson Lwenge alisema hayo jana wakati akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Liwale, Faith Mitambo (CCM). Lwenge alisema kwa sasa serikali imejikita katika kuhakikisha mikoa yote inaunganishwa kwa barabara za lami, na itakapokamilisha hilo, itazigeukia barabara za mkoa mmoja mmoja ili kuziweka katika hali bora. Awali, akijibu swali la msingi la Mitambo, alisema barabara ya Liwale-Nanguruku ni barabara ya mkoa yenye urefu wa kilometa 230. Naibu Waziri alisema katika mwaka wa fedha 2012/13, barabara hiyo ilitengewa jumla ya Sh milioni 1,066.92 na katika mwaka wa 2013/14, jumla ya Sh milioni 1,782.69 zilitengwa kwa ajili ya matengenezo mbalimbali. “Aidha, kufuatia mvua kubwa zilizonyesha katika kipindi cha mwaka wa fedha 2013/14 uharibifu mkubwa wa miundombinu ya barabara ulitokea na kusababisha uharibifu mkubwa. ...

Filamu ya Van Vicker na Wema Sepetu ‘Day After Death’ kuzinduliwa September, Dar

Filamu ya Wema Sepetu na muigizaji wa Ghana, Van Vicker ‘Day After Death’ inatarajiwa kuzinduliwa September mwaka huu jijini Dar es Salaam. Wema ameiambia Mpekuzi kuwa Van Vicker atakaa kwa wiki mbili zaidi kwaajili ya kufanya filamu nyingi na muigizaji huyo  aliyeibuka na tuzo ya muigizaji wa kike anayependwa kwenye tuzo za watu zilizotolewa Ijumaa iliyopita. “Tunaplan kuilaunch movie yetu mwezi wa tisa, kaniambia kwamba akija he is going to stay for another two weeks na anategemea tutafanya shoot nyingine huku huku,” amesema Wema. Wema amedai amefurahia kufanya kazi na Van Vicker ambaye jana alimpongeza kwa ushindi wake wa tuzo za watu. “Congrats @wemasepetu on your award for ‘Best & Loved’ Actress 2015. You deserve it. #DayAfterDeath our movie together should take you another notch higher. Thanks for trusting me. #HatsOff4U #TheYoungGodFather #TheEntrepreneur #TheVanVickerBrand,” aliandika Van kwenye Instagram

16 waitwa Taifa Stars

KOCHA wa timu ya Taifa Tanzania ‘Taifa Stars’, Mart Nooij amewaita wachezaji 16 kuingia kambini leo kwa ajili ya maandalizi ya mchezo wa kufuzu fainali za Mataifa ya Afrika (Afcon) 2017 huku mchezaji wa Mgambo JKT, Malimi Busungu akiitwa kwa mara ya kwanza. Busungu ni miongoni mwa washambuliaji waliofanya vizuri msimu uliopita katika Ligi Kuu Tanzania Bara iliyomalizika hivi karibuni akiwa na mabao tisa. Amekuwa akihusishwa kutaka kusajiliwa na klabu za Yanga, Simba na Azam Fc. Kwa mujibu wa Ofisa Habari na Mawasiliano wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Baraka Kizuguto, Kikosi hicho kilichoitwa na Nooij kitaingia kambini kwenye hoteli ya Tansoma kupimwa afya zao na kujua maendeleo yao kabla ya kujumuishwa na kikosi kilichoshiriki michuano ya Baraza la Vyama vya Soka Kusini mwa Afrika (Cosafa). Wachezaji wanaoingia kambini kupimwa afya ni Mohamed Hussein, Peter Manyika, Hassan Isihaka, Jonas Mkude (Simba SC), Salum Telela, Juma Abdul, Nadir Haroub (Yanga ), Aishi Manul...

Kocha Simba Sc kutangazwa leo

KITENDAWILI cha kocha atakayeifundisha Simba msimu ujao kinatarajiwa kuteguliwa leo, wakati jina litakapowekwa hadharani. Simba ilishindwana na kocha wake Mserbia Goran Kopunovic, aliyeiongoza timu hiyo kumaliza ya tatu katika msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliomalizika hivi karibuni. Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya timu hiyo, Zacharia Hanspoppe alisema jana kuwa, leo wanatarajia kutangaza jina la kocha huyo baada ya kushindwana na yule wa awali. Ilidaiwa kuwa Kopunovic alikuwa akitaka kiasi kikubwa cha fedha ili kusaini mkataba mpya wa miaka miwili na Simba ilikuwa ikimtaka kocha huyo kwa miezi tisa. Awali, kocha huyo alikuwa na mkataba wa miezi sita, uliomalizika Jumapili ya wiki iliyopita baada ya ligi kufikia tamati. Awali, Simba ilisema kuwa kulikuwa na majina ya makocha sita waliojitokeza kujaza nafasi ya kocha huyo Mserbia aliyetaka kiasi cha dola za Marekani 50,000 (ambazo ni sawa na Sh milioni 100) kwa ajili ya kusaini mkataba. Pia, kocha huyo inadaiwa alihitaji ki...

Oman yaikabidhi SMZ bil. 12.3/-

Published on Wednesday, 27 May 2015 00:29 Written by Khatib Suleiman, Zanzibar Hits: 72 SERIKALI ya Oman imeikabidhi Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) hundi ya Sh bil 12.3 kwa ajili ya kiwanda cha uchapishaji, pamoja na nyaraka za magari 10 ya msaada, yaliyotolewa yatumiwe na viongozi. Wakati akikabidhi hundi na nyaraka hizo kwa Rais wa Zanzibar, Dk Mohammed Shein, Ikulu mjini hapa jana, Balozi wa Oman nchini, Saoud Ali Mohamed Al Ruqaishi alisema fedha hizo ni kwa ajili ya kununua mashine za kuchapisha magazeti na vitabu. Akitoa shukrani, Dk Shein aliipongeza Serikali ya Oman. Alisema, msaada huo utaiwezesha Serikali yake kufikia malengo ya kuwa na kiwanda cha kisasa cha upigaji chapa, na kwamba, hautatumika kwa malengo tofauti. Alisema, “Msaada huu unathibitisha ushirikiano mzuri wa muda mrefu kati ya Serikali hizi mbili”. Inaelezwa kuwa, Serikali ya Oman imekwisha toa misaada mingi kwa Zanzibar, ikiwemo kujenga Chuo cha Afya kilichopo Mbweni, nje kidogo ya mji ...

Mtanzania ateuliwa Mkurugenzi Mkuu Msaidizi WHO

MKURUGENZI Mkuu wa Shirika la Afya Duniani (WHO), Dk Margaret Chan amemteua Mtanzania, Dk Winnie Mpanju- Shumbusho kuwa Mkurugenzi Mkuu Msaidizi wa shirika hilo. Uteuzi huo wa Dk Mpanju unaanza Juni mosi, mwaka huu na ulitangazwa wakati wa kikao cha Baraza la WHO lililofanyika Mei 18 hadi Mei 26, mwaka huu Geneva, Uswisi. Kutokana na uteuzi huo, Dk Mpanju sasa ataongoza Kitengo cha WHO kinachoshughulikia Ukimwi, kifua kikuu, malaria na magonjwa yasiyopewa kipaumbele. Atafanya kazi hiyo kwa kushirikiana na nchi husika katika kudhibiti magonjwa hayo, hivyo kutoa mchango katika maendeleo na mafanikio ya Malengo ya Milenia na Malengo Endelevu ya Maendeleo. Dk Mpanju ana uzoefu wa zaidi ya miaka 30 katika nafasi za juu za uongozi wa masuala ya afya, afya ya jamii, ushirikiano wa kimataifa na elimu kwa ujumla. Kabla ya uteuzi huo, Mpanju alikuwa Mkurugenzi katika ofisi ya Mkurugenzi Msaidizi wa WHO anayeshughulikia Ukimwi, kifua kikuu, malaria na magonjwa yasiyopewa kipaumbele Chini ya ...

JK akerwa vijana nchini kutumika na wazee

TABIA ya vijana wa sasa ya kuchukua fedha kutoka kwa wazee na kuwagawia vijana wenzao ili kurahisisha mambo kwa wazee hao, imeonesha kumkera Rais Jakaya Kikwete. Akizungumza na vijana mjini hapa alisema vijana wa zamani walikuwa tofauti na wa sasa, wakati vijana wakihakikisha mambo yanakwenda vyema na hawatumiki vibaya, wa sasa ndio wanachukua fedha na kuwagawia wenzao. Alisema tabia ya baadhi ya viongozi wa vijana kutumika kugawa fedha za wazee inaua demokrasia na maadili na kuingiza utamaduni wa hovyo katika siasa. “Kama ukiwa na viongozi wa vijana unapojihusisha na kugawa fedha, vijana hamuwezi kugeuka makuwadi, hamuwezi kugeuka kuwa mawakala wa kuhonga vijana wenzenu mtakuwa mmetoka kabisa kwenye mstari,” alisema Rais Kikwete. Alikuwa akifungua mkutano mkuu wa kwanza wa Shirikisho la Wanafunzi wa Vyuo vya Elimu ya Juu jana huku akitamba kuwa CCM itaendelea kuongoza na wataisoma namba. Aliwaasa vijana kuwa hatima ya CCM iko mikononi mwao na hivyo ni vyema wakajiepush...

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetoa Ratiba rasmi kuelekea Uchaguzi Mkuu Mwaka huu. Kampeni zitaanza Agosti 22 na Upigaji Kura kufanyika Oktoba 25.

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetoa ratiba rasmi kwa vyama vya Siasa na wananchi wote itakayotumika katika Uchaguzi Mkuu wa Serikali  unaotarajia kufanyika Oktoba mwaka huu. Kwa mujibu wa taarifa iliyosainiwa na Mwenyekiti wa Tume hiyo  Jaji wa Rufaa (Mst.) Damian Lubuva imesema kuwa kwa Mamlaka waliyopewa kwa mujibu wa vifungu vya 35B(1), (3) (a), 37 (1) (a) na 46 (1) vya Sheria ya Taifa ya Uchaguzi,  Sura ya 343, shughuli za uchaguzi zinatarajia kuanza hivi karibuni. Taarifa hiyo imefafanua kuwa  Uteuzi wa wagombea Urais, Ubunge na Udiwani unatarajia kufanyika Agosti 21, 2015, na  kampeni za Uchaguzi kwa wagombea hao zitatarajia kuanza Agosti 22 mpaka - Oktoba 24 mwaka huu. Halikadhalika siku ya kupiga kura kwa wananchi wote inatarajiwa kuwa Oktoba 25, 2015 kwa wale waliojitokeza kujiandikisha kwenye daftari la wapiga kura.

Frola Mbasha Ajiunga CHADEMA

MWIMBAJI maarufu wa nyimbo za injili nchini, Frola Mbasha ameijunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema). Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika viwanja vya Tanganyika Packers mjini Dar es Salaam jana, Mbunge wa Kawe, Halima Mdee (Chadema), alisema kuijunga kwa Mbasha katika chama hicho kutasaidia kuhamasisha wasanii wengine ambao wamekuwa wakitumiwa na Chama Chama Mapinduzi (CCM), bila kupata mafanikio. ” Idadi kubwa ya wasanii nchini, wanateseka bila ya kujijua, hii inatokana na kutumiwa na CCM bila kupata mafanikio ya aina yoyote…Frola inabidi uwaelimishe ili waweze kujiunga na chama chetu,”alisema Mdee. Naye Mwenyekiti wa Chadema,Freeman Mbowe alisema siku Serikali itakapowasilisha muswada wa Sheria wa Vyombo vya Habari bungeni, wabunge wa chama hicho na wale wanauounda Umoja wa Katiba ya Wananchi ( Ukawa) watafanya vurugu ili kuhakikisha haupiti. Alisema baadhi ya vipengele vya muswada huo vinakandamiza waandishi na wananchi kupata...

Madiwani Walia Na Ndoa FEKI Za Walimu......Wadai Upungufu Wa Walimu Vijijini Unasababishwa Na Walimu Wa Kike Kughushi Vyeti Vya Ndoa

BAADHI ya Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Muheza, mkoani Tanga, wamesema tatizo la upungufu wa walimu kwenye shule za msingi zilizopo vijijini kunachangiwa na walimu hasa wa kike kutaka kufundisha mjini. Walisema baadhi ya walimu wa kike wamekuwa wakighushi vyeti vya ndoa ili kuonesha wameolewa na kuwafuata waume zao mijini jambo linalozorotesha jitihada za Serikali kumaliza tatizo la walimu kwani baadhi ya shule za vijijini zina walimu hadi wawili. Madiwani hao waliyasema hayo mwishoni mwa wiki kwenye Kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo Diwani wa Kata ya Lusanga, Sesiwa Mhando, alidai halmashauri ilitenga sh. milioni 30 kwa ajili ya walimu kupelekwa shule za vijijini; lakini hadi sasa hajui mchakato huo umekwamia wapi. "Tatizo la walimu kwenye shule za msingi linatokana na walimu kujazana mijini hasa wa kike wakiwa na ndoa   bandia, madiwani tulitenga sh. milioni 30 ili zitumike kupeleka walimu vijijini lakini sijui mchakato huo umeishia wapi," al...

Edward Lowassa Aongea na Vyombo vya Habari LEO....... Adai hahusiki na Kashfa ya Richmond, Hana Mpango wa Kuhama CCM na Yupo Tayari Kupima Afya

Waziri Mkuu mstaafu  Edward Lowassa leo amefanya  mkutano maalum nyumbani kwake mjini Dodoma  na  wahariri  wakuu  wa  vyombo  mbalimbali  vya  habari  hapa  nchini. Katika mkutano huo kwa ufupi Lowassa amesema yafuatayo; 1. Amesema Hahusiki lolote na sakata la Richmond na ndio sababu hata kamati ya Mwakyembe haikuona sababu ya kumhoji. Amesisitiza kuwa cheo cha uwaziri mkuu ndio ilikuwa lengo la kamati ya mwakyembe na spika wa bunge kipindi hicho Samwel Sitta. Amesisitiza hicho sio kikwazo kwake katika kuingia Ikulu kwani sakata la Richmond lilipikwa kumchafua. Amechukua muda mrefu kuzungumzia hili la Richmond na amesema atalisema zaidi Arusha wikendi hii.(Jumamosi) 2. Anaamini kila mtangaza nia ana makundi ya kumuunga mkono. Yeye katika mkutano huu na wahariri leo ameambatana na Nazir Karamagi, Peter serukamba, Diana chilolo, Hussein Bashe na wengineo . Pia aliyekuwa mkurugenzi wa HakiElimu Elizabeti Misoki ametan...

Mnyukano urais chama cha walimu

a Gratian Mukoba. MCHUANO mkali umeibuka ndani ya Chama cha Walimu Nchini (CWT) baada ya wagombea 28 kujitosa kuwania Urais wa chama hicho chenye nguvu kutokana na kuundwa na idadi kubwa ya watumishi wa umma. Miongoni mwa wanaogombea ni rais wa sasa wa chama hicho, Gratian Mukoba ambaye pia Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Nchini (TUCTA). Uchaguzi huo unatarajiwa kufanyika Alhamisi wiki hii kwenye Ukumbi wa hoteli ya Ngurdoto, Arumeru mkoani Arusha siku ambayo itakuwa inahitimisha mkutano mkuu wa siku tatu wa chama hicho unaotarajiwa kufunguliwa kesho na Rais Jakata Kikwete. Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya chama hicho, Kanda ya Ziwa imeongoza kwa kutoa wagombea wengi wakiwemo wa mkoa wa Mwanza, Kaliyaya Masunga wa Ilemela, Magesa Kirati wa Kwimba, Marwa D. Marwa wa Nyamagana na Mashauri Benedict kutoka Sengerema. Wengine wa Kanda ya Ziwa ni Charles George wa Geita, Godi Kiduma, Lyangombe Dotto na Malimi Macheyeki kutoka Maswa mkoani Simiyu na Juma Boniface wa Bund...

ikwete: CCM chagueni mtu anayeuzika na kukubalika, Mkicheza Itakula Kwenu!!!

Hatimaye Rais Jakaya Kikwete amemtaja mrithi wake baada ya kuwataka wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM kumchagua mgombea urais anayekubalika ndani na nje ya chama hicho. Kikwete alisema hayo jana wakati akifungua kikao cha Halmashauri Kuu kwenye ukumbi wa ofisi ya makao makuu ya chama hicho mjini Dodoma, unaojulikana kwa jina la White House. Kauli hiyo imekuja wakati chama hicho kikiwa kwenye wakati mgumu kupata mgombea mpya baada ya Rais Kikwete kumaliza muda wake wa vipindi viwili vinavyokubalika kikatiba, huku kukiwa na ongezeko kubwa la nguvu ya upinzani. Juzi, Kamati Kuu ya CCM iliwaachia huru makada wake sita waliotumikia adhabu ya miezi 17 ya kuzuiwa kujishughulisha na shughuli za uchaguzi baada ya kubainika kukiuka sheria za uchaguzi za chama hicho kutokana na kuanza kampeni mapema. Miongoni mwa makada hao, wamo wanaopewa nafasi kubwa ya kupitishwa na chama hicho na ambao kambi zao zimekuwa zikipambana vikali na kuweka wasiwasi wa kuivuruga CCM. Lakini Kikwete, am...

Walimu 1,200 kukutana na JK

wanatarajiwa kukutana na Rais Jakaya Kikwete mjini Arusha, wiki ijayo wakati kiongozi huyo wa nchi atakapokuwa akifungua rasmi mkutano wao mkuu wa mwaka kitaifa. “Tunatarajia kuwa walimu wapatao 1,200 kutoka mikoa 25 na wilaya 153 za Tanzania Bara watakutana na Rais Kikwete katika eneo la Ngurdoto, wilayani Meru, mkoani Arusha. Mkutano huo Mkuu wa Chama cha Walimu Taifa (CWT) utafanyika kati ya Mei 26 hadi 28, mwaka huu,” alisema Mwenyekiti wa chama hicho mkoani Arusha, Juvin Buruya na kuongeza: “Walimu wote Tanzania watawakilishwa vema kwenye mkutano huo ambapo tutatumia fursa ya uwepo wa Rais Kikwete kumuomba amalizie ahadi zake kadhaa alizowaahidi wakufunzi hao kabla hajastaafu rasmi,” alisema. Kwa mujibu wa mwenyekiti huyo wa CWT mkoani Arusha, walimu watakaojumuika kwenye mkutano mkuu, watatumia fursa hiyo kumuaga rasmi mke wa Rais, Mama Salma Kikwete ambaye pia ni mwalimu. Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu wa CWT, Ezekiah Oluoch alisema chama hicho kim...

Wema Sepetu, Ray , Hemedy PHD Wanyakua Tuzo Za ‘Tuzo Za Watu2015’

Mastaa wa Bongo Movies, Wema Sepetu, Vicent Kugosi ‘Ray’ na Hemmedy PHD wameshinda tuzo za TUZO ZA WATU za mwaka huu zilizofanyika usiku wa jana. Wema sepetu ameshinda tuzo ya muigizaji wa kike anayependwa  wakati Ray ameshinda tuzo ya muongozaji  wa filamu anayependwa huku Hemmed PHD ameibuka mshindi wa wa tuzo ya muigizaji wakiume anayependwa na filamu ya Kigodoro imeibuka kuwa ni filamu inayopendwa.

Comoro yahitaji Msaada wa Ndege Tanzania

SERIKALI ya Comoro imeiomba Serikali ya Tanzania iisaidie kutatua changamoto ya uhaba wa ndege zinazotua nchini humo hali iliyosababishwa na kusitishwa kwa huduma za safari za shirika la ndege la Yemen. Akizungumza na waandishi wa habari jana katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julias Nyerere jijini Dar es Salaam, Waziri wa Uchukuzi wa Comoro,  Bahia Masoundi, alisema Shirika la Ndege la Yemen lilisitisha huduma zake kufuatia machafuko yanayoendelea nchini Yemen. “Mchafuko ya nchini Yemen yalipelekea shirika lao la ndege kusitisha huduma zake na kutokana na kwamba ndilo shirika tulilokuwa tukilitegemea kwa kiasi kikubwa ndio maana uhaba umejitokeza baada ya kufunga huduma zao,” alisema Massoundi. Alisema kwa sasa kuna mashirika manne tu yanayofanya kazi nchini humo na ndege zinazotua ni chache na kwamba serikali ya nchi hiyo haimiliki shirika hata moja hivyo kulazimika kuomba msaada nchini Tanzania. Naye Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Anga Tanzania (...

Mwalimu na Wenzake Watano Wakamatwa na Mifupa ya Albino

WATU sita, akiwemo Mwalimu wa Shule ya Msingi Katunguru iliyoko Kata ya Wendele, Tarafa ya Msalala wilayani Kahama, wamekamatwa mjini hapa wakiwa na vipande sita vya mifupa inayodhaniwa kuwa ya albino. Taarifa zilizopatikana mjini hapa zimeeleza kwamba, mwalimu huyo Bahati Kilungu Maziku (56), Msukuma na mkazi wa Mtaa wa Mbulu katika Halmashauri ya Mji wa Kahama, amekamatwa akiwa na watu watano, wakiwemo waganga wa jadi watatu, katika harakati za kuuziana mifupa hiyo. Wengine waliokamatwa ni mganga wa jadi Bi. Elizabeth au Shija Makandi Sweya (42), mkazi wa Busongwahala, Wilaya ya Nzega mkoani  Tabora, Bilia Masanja Mhalala (39), Msukuma, mkulima na mkazi wa Mogwa wilayani Nzega, mke wa Biria ambaye ni mganga wa jadi Regina au Tatu Kashinje Nhende (40), Msukuma na mkazi wa Mogwa. Aidha, watuhumiwa wengine waliokamatwa ni Muhoja John Shija (24), Mnyamwezi na mkazi wa Isagenhe wilayani Nzega pamoja na mganga wa jadi na mfanyabiashara Abubakar Ally Magazi (25), Mrundi na mkaz...

Urais 2015: Mwanamke wa kwanza CCM ajitokeza kutangaza nia

Mwanamke wa Kwanza ndani ya chama cha Mapinduzi (CCM) Amina Salum Ali, amevunja ukimya na kuamua kuweka wazi nia yake ya  kutaka kugombea urais katika uchaguzi mkuu utakaofanyika mwezi oktoba. Akizungumzia uamuzi huo, mwanasiasa huyo ambaye pia ni Balozi wa Kudumu wa Umoja wa Afrika (AU) katika Umoja wa Mataifa (UN), amesema wanawake wamekuwa wanyonge kugombea nafasi za juu za uongozi kwa kukosa fedha, lakini sasa ni wakati mwafaka kwao kujiamini katika jamii kwani uongozi siyo fedha bali ni uzalendo, kujikubali na kujiamini. “Nimeona nina uzalendo, ninajiamini na ninaweza kuifikisha nchi yangu katika uchumi wa kwanza kwa kutumia rasilimali zetu zikiwamo gesi, mafuta, kilimo na utalii. Ninajiamini kwamba wakati wangu umefika kuwaongoza Watanzania.” amesema Amina Amina  aliwahi kushika nafasi za juu za uongozi Zanzibar na Tanzania Bara, ukiwamo uwaziri wa fedha Zanzibar. Ameongeza kuwa wanawake wengi wanaogopa kujitokeza wakihofia kugombea nafasi za juu ...

Aunty Ezekiel ajifungua mtoto wa kike, amuita Cookie

Muigizaji wa filamu za Bongo, Aunty Ezekiel amejifungua mtoto wa kike siku ya Alhamis May 21. Mtoto huyo wa Aunty Ezekiel ambaye baba yake ni dancer wa Diamond aitwaye Mose Iyobo, amepewa jina la Cookie. Aunty ameshare habari hiyo na mashabiki wake wa Instagram: “Amin ktk Mungu ndio Mwisho wa Matatizo yote yaliyotuzunguka Hakuna mganga wala Mchawi pasipo Mungu. "Ahsante Mungu wang kwa kunikabidhi zawadi yang Asubuhi jana tar 21-05-2015 Muache yy atende kwani ndio nguzo yetu sote Nasema Ahsante tena Ahsante kwa zawadi hii kubwa ktk Maisha kwani ilikuwa ni kipindi kigumu chenye majaribu ya kila aina kupitia binaadamu wajizaniao wao ni miungu watu Bac endelea kunyoosha mkono wako ktk paji la kiumbe wako ukiwa kama kinga nami niwe kivuli tuu juu yake Amen Whn Jesus Say Yes Ni body can Say wht!!!!!!!Wlcm Baby Cookie wlcm 2 da world KIBOKO YANG…” Diamond ambaye ni uncle wa Cookie pia amempongeza Aunty na Mose kupitia Instagram: “Hongera sana @auntyezekiel na @...

Malinzi: Kocha hang’oki

RAIS wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi amesema kuwa hana mpango wa kumfukuza Kocha Mkuu wa timu ya taifa, Taifa Stars, Mart Nooij. Kwa sasa wadau mbalimbali wa soka wamependekeza kufukuzwa kwa kocha huyo hasa kutokana na kufanya vibaya kwa timu hiyo katika michuano ya Cosafa inayoendelea nchini Afrika Kusini. Timu hiyo inashiriki michuano hiyo kama mgeni mwalikwa ikiwa pamoja na Ghana, ilifungwa na Madagascar mabao 2-0 katika mchezo wake wa pili wa Kundi B uliofanyika kwenye Uwanja wa Royal Bafokeng mjini Rustenburg. Awali, Jumatatu wiki hii ilifungwa bao 1-0 na Swaziland katika mechi ya kwanza, hali ambayo inamaanisha kuwa timu hiyo haikupata hata bao moja, kitu ambacho kimewakera mashabiki wengi wa soka. Lakini wakati Nooij akicheza mechi yake ya 15 juzi na kufungwa sita, kutoka sare sita na kushinda mechi tatu tu tangu Aprili mwaka jana alipoanza kazi, Malinzi anasema licha ya matokeo hayo, haoni sababu ya kumfukuza Mholanzi huyo. Katika mahojiano na ...

Tuhuma za wanaume Rombo zamfadhaisha mbunge wao

lasini. MADAI ya wanawake wa wilaya ya Rombo, Kilimanjaro, kukodi wanaume kutoka nchini Kenya, baada ya kukosa huduma za ndoa kutoka kwa waume zao kwa muda mrefu, kutokana na ulevi wa gongo uliopindukia, zimemfadhaisha Mbunge wao, Joseph Selasini (Chadema). Mbunge huyo amefikia hatua ya kusema kuwa familia yake na wananchi wa huko, wamefadhaika na kuingiwa na wasiwasi kuwa huenda wenzi wao katika ndoa zao ikiwemo ya mbunge, si waaminifu. Selasini alisema hayo jana, alipokuwa akiuliza swali kwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ambapo alisema ingawa hali hiyo imewafadhaisha, lakini alitetea utengenezaji wa pombe za kienyeji, ikiwemo pombe haramu ya gongo. Katika utetezi huo, Selasini alitaka Serikali iangalie namna ya kusaidia uboreshwaji wa pombe za kienyeji, kwa kuwa kipato chake kimekuwa kikisaidia ada za watoto, kujikimu na kuongeza kipato cha familia. Akijibu swali hilo, Pinda alisema kwa namna Selasini anavyozungumza, huenda anatetea suala la kuhalalisha pombe haramu aina ya gongo, ...

Vikao vizito vya CCM kuanza leo

na CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimejigamba kitatoka katika vikao vyake muhimu vya Kamati Kuu (CCM) na Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) vinavyoanza mjini hapa leo kikiwa imara kuliko hapo awali. Kauli hiyo imetolewa na Katibu wa Itikadi na Uenezi Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Nape Nnauye wakati akijibu swali kuhusiana na vikao vizito vya chama hicho vinavyoanza leo. Nnauye alikuwa anaelezea maandalizi ya vikao vya kamati kuu kinachotarajia kuanza leo na halmashauri kuu ambayo itaanza kikao chake cha siku mbili kesho. Katibu huyo amesema wajumbe wa vikao hivyo ambavyo vitatoa mwelekeo wa sura ya uchaguzi itakavyokuwa ndani na nje ya chama hicho wameshaanza kuwasili mjini hapa. Ajenda muhimu katika mikutano hiyo ni ratiba ya uchaguzi pamoja na kuwapata wagombea wa chama hicho ngazi zote. Ajenda nyingine ni hali ya kisiasa nchini na kutolewa kwa ratiba ya uchaguzi. Pia vikao hivyo vinatarajia kutoa ratiba ya mchakato wa uchaguzi wa Urais na wagombea wengine, kutengeneza kanuni za kuwap...

Magazeti ya leo tar 22/5/2015

Magazeti ya leo