Skip to main content

Posts

Showing posts from June, 2015

Membe kupeleka nchi kwenye uchumi wa viwanda

WAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, ametangaza rasmi kuwania urais wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM}, huku akitamba ataipeleka nchi katika uchumi wa viwanda unaobebwa na kilimo na kuahidi kujenga serikali ya waadilifu. Licha ya Membe, wana CCM wengine wawili jana walitangaza pia kugombea urais nao ni Naibu Waziri wa Sayansi na Teknolojia Januari Makamba pamoja na Mbunge wa Nzega Dk Hamis Kigwangala. Membe alifichua kuwa alienda kuomba kwenye kaburi la Baba wa Taifa, hayati Mwalimu Julius Nyerere ili kupata ridhaa na kusisitiza kuwa urais si suala la kukurupuka na kwamba atahakikisha anasimamia utawala bora, huku akiongoza mapambano dhidi ya rushwa na kwa kubadili kipengele cha mtu atakayetoa rushwa na kutoa taarifa awe huru. Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika viwanja vya CCM Mkoa wa Lindi jana, Waziri Membe alisema kabla ya kuchukua uamuzi wa kufikiria urais alijipima na kuona anatosha kwa nafasi hiyo, pia baada ya kuwaangali...

Mama amchoma mikono mwanae kwa madai ya kuiba ugali

i Mponzi mkazi wa kijiji cha Ikule wilayani Kilombero,  mkoani Morogoro anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kumchoma mwanae na kumjeruhi mikono kwa madai ya kuiba ugali. Mama huyo alimuunguza mwanaye  Joseph Chawala, akimtuhumu Kuiba Ugali, kwa mujibu wa watendaji  mbalimbali wa kata ya Mng’eta. Wakizungumzia tukio hilo Jerome Chulu na Jeneth Hetela,  walisema unyanyasaji huo  ulishuhudiwa na majirani wa mwanamke huyo baada ya kusikia kelele za watoto ambao walimchukua mtoto huyo kumpeleka ofisi  ya mtendaji wa kata,polisi na baadaye hospitali. Walibainisha baadaye kuwa polisi  walikwenda kumkamata mwanamke huyo na mumewe Halidi Kiwenji ambaye  inadaiwa alikuwa karibu wakati wa tukio hilo ingawa baadaye baba huyo aliachiwa ili akawaangalie watoto wengine nyumbani. Polisi  walithibitisha tukio hilo ambalo uchuguzi wake unaendelea ili kumfikisha mahakamani mtuhumiwa huyo. Wananchi mbalimbali waliohojiwa wametaka hatua kuchukuliw...

Midahalo Watangaza Nia CCM Ruksa......Kinana Asema Nafasi Wanayoomba ni Kubwa, Ataka Wahojiwe wananchi Wawasikie

SIKU moja baada ya Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Mohamed Seif Khatib kupiga marufuku pamoja na mambo mengine makada wa chama hicho waliochukua fomu kuwania urais kushiriki midahalo, Katibu Mkuu wa chama hicho, Abdulrahman Kinana amepinga msimamo huo. Badala yake, Kinana ameruhusu makada hao wanaoomba ridhaa ya kupeperusha bendera ya chama hicho kwa nafasi ya urais kushiriki katika midahalo iliyoandaliwa na Umoja wa Watendaji wa Kampuni binafsi (Ceo's roundtable), huku akiwataka waandaaji wa midahalo hiyo kutenda haki ili kuepusha mifarakano. Akizungumza na waandishi wa habari mjini Bukoba jana, Kinana alisema midahalo hiyo inaweza kuwafanya wananchi kuwatambua wagombea wao na kuwapima kwa hoja kama wanaweza kuongoza nchi au la ili waweze kuwapigia kura. “Nimepigiwa simu na baadhi ya wagombea waliotangaza nia ya kuwania nafasi ya urais ndani ya chama, sasa nawaambia kuwa wana hiari ya kwenda au kutokwenda kwa sababu ni uamuzi wao binafsi na si suala la chama. ...

Polisi yakamata kontena la nyaya za milioni 150/-

Maalumu ya Dar es Salaam limekamata kontena likiwa na rola 15 za nyaya za umeme mali ya Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) zenye thamani ya Sh milioni 150. Akizungumza na waandishi wa habari jana, Kaimu Kamishna wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam Simon Sirro, alisema nyanya hizo ziliibwa Februari 26 zikiwa zinasafirishwa kuelekea mkoani Kagera kwa ajili ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA). Alisema baada ya wizi wa kontena hilo, kesi ilifunguliwa katika Kituo cha Polisi Buguruni na watuhumiwa watano kukamatwa na kufikishwa mahakamani. Aliongeza kuwa wakati upelelezi ukiendelea Mei 25 mwaka huu, polisi walipokea taarifa kutoka kwa msiri kwamba maeneo ya Kibamba mtaa wa Kibengewe kuna kontena katika kiwanda cha kutengenezea matofali. Alisema askari walifika eneo la tukio na kukuta kontena hilo lenye namba 00LU2876031 na kumhoji mlinzi wa eneo hilo ili kumpata mmiliki wa eneo na kontena hilo. “Tunashukuru ilipofika saa 5:00 usiku tulifanikiwa kumpata mmiliki wa eneo hilo, ...

Wananchi wanaopata maji wafikia 55%

Jumanne Maghembe. SERIKALI imesema kwamba sekta ya maji kwa kutumia mfumo wa Matokeo Makubwa Sasa (BRN) imeongeza wananchi wanaopata huduma ya maji kutoka milioni 15.2 Juni, 2013 hadi kufikia milioni 20.9 sawa na asilimia 55. Hata hivyo, baadhi ya wabunge na Kambi Rasmi ya Upinzani wamepinga takwimu hizo. Aidha wabunge waliozungumza baada ya bajeti kusomwa jana, wabunge hao walisema kwamba kuna udanganyifu mkubwa wa takwimu zilizowasilishwa ndani ya Bunge, huku Kambi ya Upinzani ikidiriki kusema kwamba mipango ya Serikali ya kuwapatia wananchi wake maji imeshindwa. Msemaji wa Kambi ya Upinzani wa Wizara ya Maji, Mohamed Rajab Mbarouk alisema kwamba takwimu za utafiti wa kitaifa katika eneo la maji, zinaonesha kwa sasa wananchi wanaopata maji safi na salama ni asilimia 40 tu na sio asilimia 57.8 kama ilivyorekodiwa katika taarifa za Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umasikini Tanzania (Mkukuta). Alisema takwimu nyingi pamoja na visima vinavyofanya kazi si sahihi, hali inayodhihi...

Msafara wa Makongoro Nyerere Wapata Ajali

MSAFARA wa Makongoro Nyerere, mtoto wa Baba wa Taifa, hayati Mwalimu Julius Nyerere, umepata ajali wakati mwanasiasa huyo akiwa katika harakati za kutimiza masharti ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya kutafuta wadhamini ili aweze kuwania nafasi ya urais. Ajali hiyo iliyojeruhi watu watano waliokuwa kwenye msafara huo, ilitokea jana katika eneo la Tekniko, Wilaya ya Kasulu, mkoani Kigoma baada ya gari aina ya Land Cruiser lenye namba T 188 BXG walilokuwamo kupinduka. Akithibitisha kutokea kwa ajali hiyo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kigoma, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Ferdinand Mtui, alisema ilitokea saa 10:30 asubuhi wakati msafara huo ukiongozwa na Makongoro ukielekea Kigoma mjini. Kamishna Mtui aliwataja waliojeruhiwa sehemu mbalimbali za mwili ikiwamo kichwani na mabegani  kuwa ni dereva wa gari hilo Julius Kambarage, ambaye ni mtoto wa Makongoro na mwandishi  Evans Magege. Wengine ni Katibu Mwenezi wa CCM, Musoma Mjini, Fikiri Marumba na Ally Tesha a...

Vijana watakiwa Kuwaepuka Wanasiasa Matapeli

VIJANA wilayani Tarime wametakiwa kuepuka baadhi ya wanasiasa wanaowatumia na kuwafanya kuwa daraja la kupandia ili kupata vyeo kwa maslahi yao binafsi. Kauli hiyo ilitolewa hivi karibuni na Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Mfaume Ally Kizigo, wakati wa ziara yake ya kuhamasisha uhai wa chama wilayani Tarime. Alisema kuna haja vijana kuepuka wanasiasa wanaowatumia kwa maslahi yao binafsi, huku wakiwaacha mitaani wakitaabika. Aliwatahadharisha kabla ya kujiunga na chama chochote cha siasa wafanye upembuzi wa kina kuangalia kitakachowavusha badala ya kukimbilia vyama kwa ushabiki. Alisema baadhi ya vijana wamekuwa wakikimbilia vyama vya upinzani kwa ushabiki, jambo ambalo huwarudisha nyuma kimaendeleo. “Fanyeni utafiti kabla ya kujiunga na chama chochote cha siasa, ukijiunga na chama kwa kufuata mkumbo mwisho wa siku utajutia,” alisema Kizigo

Padre na Wanafunzi sita Wateteketea Kwa Moto

WANAFUNZI sita wa Sekondari ya CTC Kigonsera inayomilikiwa na Misheni ya Mbinga mkoani Ruvuma na Mkuu wa Shule hiyo, Padre Yazint Kawonga, wamefariki dunia baada ya gari walilokuwa wakisafiria kutumbukia bondeni kisha kuwaka moto na kuiteketeza miili yao. Akizungumza na Mpekuzi jana shuhuda wa ajali hiyo, Makarius Nchimbi, alisema ilitokea juzi saa tisa alasiri katika mlima uliopo karibu na shule hiyo huku likiwa limewabeba wanafunzi waliokuwa wakitokea shambani kuvuna mahindi ya shule hiyo. Nchimbi ambaye ni mfanyakazi wa kitengo cha udereva katika misheni hiyo alidai yeye ndiye aliyekuwa dereva wa gari hilo kabla ya kupokelewa na Padre Kawonga aliyemtaka amsaidie kuliendesha kwa kuwarudisha shuleni wanafunzi waliokuwa shamba lililopo Kijiji cha Mkulumus kilichopo Kigonsera. Alisema gari hilo aina ya Land Rover 110 Station Wagon lenye namba T 306 AYM  lilipofika katika mlima huo lilimshinda Padre Kawonga wakati akitumia gia namba mbili na kuanza kurudi nyuma huku wanafunzi weng...

‘Sheria ya 1971 inachangia ndoa, mimba za utotoni’

SERIKALI imeombwa kuangalia upya Sheria ya mtoto ya mwaka 1971 kwani imebainika kuwa ndio chanzo kimojawapo kinachoruhusu na kuchangia ndoa za utotoni pamoja na mimba za utotoni. Akizungumza katika wa kongamano lililoandaliwa na Shirika la Intiative for Youth (INFOY), Mwenyekiti wa Baraza la Watoto Wilaya ya Arusha, Hassani Omary alisema ni wajibu wa serikali kuangalia upya sheria hiyo kwani sheria hii imekuwa ikiwaathiri watoto wengi hapa nchini. Alisema sheria hiyo imekuwa ikiruhusu watoto hata wenye umri chini ya miaka 18 kuolewa iwapo tu wazazi wake watakapokubali, kitu ambacho kinawaathiri watoto wengi katika masomo yao. Alisema ikitokea mtu mmoja kupeleka lalamiko lake katika vyombo vya sheria amekuwa akishindwa kutokana na sheria hiyo kuleta mkanganyiko kwani mtoto huyo hata awe mdogo kuolewa mradi tu familia yake iwe imeafiki. Aidha mbali na sheria hii pia Serikali inatakiwa kutilia mkazo katika mila mbalimbali na desturi kwani mila zingine zimekuwa zikichangia kwa kiasi ki...

Bunge kukaa hadi Jumapili

MKUTANO wa 20 wa Bunge la Bajeti kwa mwaka wa fedha 2015/16, umelazimika kupanga kikao chake kufanyika keshokutwa Jumapili ili kwenda na ratiba. Kwa mujibu wa ratiba mpya ya Mkutano huo iliyotolewa jana na Ofisi ya Bunge, keshokutwa Wizara ya Fedha itawasilisha bajeti yake kuanzia saa tano asubuhi. Awali, Wizara ya Fedha ilipangwa kuwasilisha bajeti yake kesho, lakini ratiba ilivurugika Jumanne wiki hii baada ya kifo cha ghafla cha Mbunge wa Jimbo la Ukonga mkoani Dar es Salaam, Eugen Mwaiposa (CCM). Kutokana na kifo hicho, Bunge liliahirishwa Jumanne mchana ikiwa ni saa chache baada ya kuwasilishwa kwa Bajeti ya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii. Bunge lilirejea jana kwa kipindi cha Maswali ya Kawaida asubuhi bila kuwapo kwa Maswali ya Papo kwa Hapo kwa Waziri Mkuu na baadaye mjadala wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii uliendelea hadi jioni. Leo itakuwa zamu ya Wizara ya Maji na kesho itakuwa Wizara ya Nishati na Madini, wizara mbili ambazo hotuba zao zilitakiwa kuwasilishwa Jum...

Zatumwa bil 10/- kulipa walimu wapya

SERIKALI imetuma Sh bilioni 10 katika mikoa mbalimbali nchini kwa ajili ya kuwalipa walimu wapya ambao wameripoti kazini mapema mwezi uliopita. Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba alisema hayo bungeni jana, alipotoa ufafanuzi kwa Mwongozo kwa Spika ulioombwa na Mbunge wa Tabora Mjini, Ismail Aden Rage (CCM). Rage katika Mwongozo wake huo, alitaka kusikia kauli ya Serikali kuhusu walimu wapya ambao wamepangwa katika Manispaa ya Tabora na sehemu nyingine nchini kuwa hawajapewa fedha zao na wanaishi katika hali ngumu kwa sasa. Naibu Waziri alikiri kuwa ni kweli wapo walimu katika baadhi ya halmashauri nchini, hawajalipwa fedha zao baada ya kuripoti kazini kutokana na sababu mbalimbali. “Ni kweli wapo walimu hawajalipwa fedha zao kama alivyoeleza Mheshimiwa Rage. Yapo maeneo kadhaa nchini na hii imetokana na matatizo kati ya wizara husika na hazina,” alisema Mwigulu na kuongeza: “Ni kama nilivyoeleza hapa juzi kuwa watumishi wanapopangwa ni lazima kila kitu kikamili...

Nooij asema Stars itang’ara

KOCHA wa timu ya soka Taifa, ‘Taifa Stars’, Mart Nooij amesema watajitahidi kuhakikisha wanafanya vyema katika michuano yote iliyoko mbele yao. Taifa Stars ipo kwenye harakati za kuwania kufuzu michuano ya Kombe la Mataifa Afrika (AFCON) na ile ya Kombe la Afrika kwa wachezaji wa ndani (CHAN). Kwa sasa timu hiyo ipo kambini ikitarajiwa kucheza na Misri Juni 14 katika mechi ya kuwania kufuzu Afcon. Akizungumza jana kwenye hafla fupi ya uzinduzi wa jezi na utoaji wa tuzo kwa waliotoa mchango kwenye soka ya Tanzania, Nooij alisema wana kikosi cha wachezaji 41 kambini ambapo baadhi wataondoka leo na wengine watabaki kujiandaa na michuano ya Chan. “Tutajaribu kufanya vizuri, tuna Afcon na Chan yote ina umuhimu mkubwa kwetu, watakaobaki wataenda Zanzibar kwa maandalizi ya mchezo dhidi ya Uganda,” alisema. Kwa upande wake nahodha wa Stars, Nadir Haroub alisema uzinduzi wa jezi mpya utawasaidia wao kuzivaa na kwenda kupambana kwa juhudi ili kupata ushindi. Kocha Noo...

Mpinzani wa Lipumba afukuzwa uanachama

BARAZA Kuu la Uongozi la Chama cha Wananchi (CUF), limemvua uanachama mjumbe wake kutoka Mkoa wa Shinyanga, Chifu Lutayosa Yemba. Chifu Yemba ambaye pia alikuwa ni mpinzani wa Profesa Ibrahim Lipumba katika kuwania uenyekiti wa CUF kwenye uchaguzi uliofanyika mwaka jana, alivuliwa uanachama kwa tuhuma za ubadhirifu wa fedha za chama pamoja na kutumia vibaya jina la mwenyekiti wa chama hicho. Chanzo cha kuaminika kutoka ndani ya kikao hicho cha Baraza Kuu kilichoanza vikao vyake jana jijini Dar es Salaam, kimesema kuwa tuhuma za mjumbe huyo zilifikishwa mbele ya kikao hicho na kufikiwa uamuzi huo. “Kikao cha Baraza Kuu bado kinaendelea hapa na ajenda kubwa ilikuwa ni tuhuma dhidi ya Chifu Yemba ambaye anadaiwa kutumia jina la Mwenyekiti wa chama kuanzisha Saccos na hata kusababisha chama kudaiwa shilingi milioni 12. “Lakini pia amekuwa akitumia jina la Mwenyekiti wa chama, Profesa Lipumba katika mradi wake huo binafsi ambao anauendesha na hata kusababisha chama ku...

Mwakyembe Akana kutumia Richmond Kumchafua Lowassa...... Umoja wa Ulaya nao wakana kuhusika Kumchafua.

WAZIRI wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk. Harrison Mwakyembe, ameibuka na kusema hajawahi kumshambulia kwenye mitandao Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa kuhusu sakata la Richmond. Kauli hiyo ya Dk. Mwakyembe imekuja siku chache baada ya kusambazwa kwa waraka unaodaiwa kuandikwa naye, ukimuhusisha na tuhuma za kumshambulia Lowassa, jambo ambalo amelifananisha kuwa ni sawa na siasa za kitoto. Akizungumza jana katika kipindi cha Power Breakfast kinachorushwa na kituo cha redio Clouds FM, alisema kutokana na kusambazwa kwa waraka ambao umeandikwa nyadhifa zake za ubunge na uwaziri, hivi sasa ameshaanza kuchukua hatua za kisheria dhidi ya watu waliokuwa wakiusambaza. Waziri Mwakyembe ambaye kitaaluma ni mwanasheria na mwanahabari, alisema anapata shaka hata na baadhi ya vyombo vya habari pamoja na mitandao hiyo na kudai kuwa anamshambulia Lowassa. “Ninashangazwa sana na hii mitandao ya kijamii na baadhi ya vyombo vya habari (magazeti), vimekuwa vikiandika vitu viba...

Nyumba Anayoishi Ali Kiba Yazua Utata..Yadaiwa si yake Bali Kapewa Kuishi tu na Mrembo Amazing Anayeishi Singapore

Musa Mateja Mjengo anaoishi mkali wa Bongo Fleva anayetamba na ngoma yake ya Chekecha Cheketua, Ali Saleh Kiba uliopo Kunduchi-Mbezi Beach jijini Dar, unadaiwa kuzua utata mkubwa hivyo kulilazimu Risasi Jumamosi kuchimba na kubaini kuwa nyumba hiyo si ya msanii huyo bali amepangisha. Awali, Kiba alikaririwa akisema kuwa, mjengo huo wa kifahari ni wa ndugu yake aliyepo nje ya nchi ambaye alimpa ili aishi na ndugu zake (wa Kiba) wakati yeye (mmiliki) akiwa hayupo.Siku kadhaa mbele, baada ya Kiba kuvamiwa nyumbani hapo na watu kupora vitu huku akinusurika kuuawa, jamaa huyo alikaririwa redioni na kwenye mitandao ya kijamii akisema kuwa nyumba hiyo ni yake. Ilidaiwa kwamba, mara tu baada ya Kiba kutangaza kumiliki nyumba hiyo, ilidaiwa kuwa aliibuka mwanamke aliyetajwa kwa jina moja la Mariana ikisemekana eti ndiye mmiliki halali wa nyumba hiyo.Madai mazito yaliendelea kushushwa kwamba, Mariana, akiwa mwandani wa Kiba ndiye aliyemuweka Kiba aishi kwenye nyumba hiyo wakati yeye (Mariana)...

mashabiki Alikiba asema vurugu zilizotokea Afrika Kusini zimesababisha video ya ‘Chekecha’ ichelewe, awaomba msamaha mashabiki

Staa wa muziki Alikiba amesema kuwa video shooting ya wimbo wake ‘Chekecha’ ambayo imepangwa kufanyika Afrika Kusini, imechelewa kutokana na vurugu dhidi ya raia wa kigeni (Xenophobia) zilizoibuka hivi karibuni nchini humo. “Tayari tulikuwa tumeplan kila kitu unajua kunakuwa kuna zile dancing, choreographer wangu alikuwa ameshacreate kila kitu amewatumia dancers wa South Africa, lakini kilichotufelisha ni hii Xenophobia iliyokuwa imetokea,” alisema Alikiba kupitia Ubaoni ya E-Fm. “Vile vile unajua vifaa kule wanakuwa wanaazima kwahiyo imekuwa ni sheria ambayo imepitishwa hairuhusiwi kufanya hivyo mpaka patulie.” Hata hivyo Alikiba amesema mipango yote inaenda vizuri na siku si nyingi atasafiri kuelekea Afrika Kusini kwaajili ya kulipa deni la video alilonalo kwa mashabiki wake. “Kwahiyo tumefanya tena opportunity nyingine tumepata tayari namshukuru Mungu tumeshapanga kila kitu.” Kwa kuonesha kuwa anawajali na kuwaheshimu mashabiki, Kin...

WEMA SEPETU Awashukia na Kuwapa Vidonge vyao Waandaji wa Instagram Kwa Kutokumlipa Mzee Majuto

Wema Sepetu Amefunguka kwenye Ukurasa wake wa Instagram akiwachana waandaji wa Instagram Parties Kwa Kutokumlipa Mzee Majuto Pesa zake baaada ya Wema Kuwaunganishia Mzee Huyo ili Aje kwenye Party yao iliyofanyika week end iliyopita Hapa Dar es Salaaam.....Ameandika Hivi:     Waandaaji wa Instagram party sijawapenda kiukweli... Mpaka nimefkia hatua ya kuandika basi mjue kuwa mmenikwaza... Mlikuja kwangu na mkaniomba niwatafutie Huyu Mzee wa watu... Kwa moyo mmoja nilifanya hivyo, Iweje leo hii kashamaliza kazi msitake kumlipa hela yake... Baba wa watu katoka Tanga na nauli yake, mpaka hotel kajilipia mwenyewe.... Mimi sipendi lawama jamani... Sana sana ikiwa ni kwa wasanii wenzangu... Sasa hivi naonekana mbaya mimi maana mimi ndo niliewaunganisha na huyu Baba wa watu... Hawawajui nyie ananijua mimi..... Na kaja kwa heshima yangu.... Hizo ni dhulma na sio vizuri kumfanyia hivyo Mzee wa watu... Namuheshimu sana na siwezi kumkosea heshima kiasi hicho... Ila hakuna neno tumwa...

Serikali na wafanyabiashara wafikia mwafaka EFDs

SERIKALI na wafanyabiashara nchini wamefikia mwafaka juu ya matumizi ya mashine za kielektroniki (EFDs), kuendelea huku ikiendelea kuondoa vikwazo mbalimbali vilivyojitokeza, ikiwa ni pamoja na ukokotoaji wa gharama za mfanyabiashara. Mwafaka huo ulifikiwa baada ya Kamati ya Kitaifa, iliyoundwa kwa ajili ya kupitia na kubainisha changamoto mbalimbali kuhusu mashine hizo. Mapendekezo ya kamati yalihusu kuongeza uwazi katika mfumo mzima wa kodi kwa mizigo itokayo nje ya nchi, kuanzia mchakato wa uthaminishaji na uondoshaji wa mizigo bandarini, utambuzi wa gharama za manunuzi ndani ya nchi na gharama za uendeshaji zisizotambulika kisheria kwa kutokuwa na stakabadhi. Akizungumza jana Dar es Salaam mbele ya Kamati na Viongozi wa Jumuiya ya Wafanyabiashara nchini, Waziri wa Fedha, Saada Mkuya alisema baada ya kuanzishwa, utaratibu wa kutumika kwa mashine hizo, ulikutana na changamoto mbalimbali zilizosababisha kuibuka kwa malalamiko na migogoro katika jamii. Alisema chini ya mwafaka huo,...

Serikali yaandaa programu kunufaisha wasanii

Published on Wednesday, 03 June 2015 00:07 Written by Mgaya Kingoba, Dodoma Hits: 72 SERIKALI inaandaa programu maalumu ya kunasa kazi za wasanii zinazochezwa redioni, kwenye televisheni na katika simu kufahamu kiasi gani kinastahili kulipwa kwa kutumia kazi hizo ili kuongeza mapato ya wasanii na ya serikali. Aidha, tangu kuanza kwa urasimishaji wa kazi za sanaa, hadi kufikia Mei mwaka huu, CD na DVD 30,984 zimekamatwa kwa kazi za ndani na 45,166 kwa kazi za nje. Pia Serikali imesema maandalizi ya kurekebisha Sheria ya Hakimiliki na Hakishiriki Namba 7 ya Mwaka 1999 imeanza na rasimu ya kwanza imeshaandaliwa. Akizungumzia kifaa hicho, Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Janet Mbene alisema imetangazwa zabuni ya kutafuta programu hiyo ya kunasa kazi hizo kwa nia ya kujua kiasi gani anastahili kulipwa msanii na serikali. Alisema stempu zilizotolewa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) tangu urasimishaji wa sanaa uanze ni 45,570,000 kwa muziki na 18,420,000 kwa filamu, na taarifa k...

Lowassa aahirisha Kuchukua fomu ya Kugombea Urais

Mbunge wa Monduli ambaye aliwahi kuwa Waziri mkuu wa Tanzania Edward Lowassa amaeahirisha kuchukua fomu ya kugombea urais kwa tiketi ya chama cha Mapinduzi hadi siku ya kesho ambayo ni alhamisi. Hadi sasa mwanasiasa  aliyefungua dimba la kuchukua fomu ya urais  ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Kazi Maalumu), Profesa Mark Mwandosya pamoja na Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika Stephen Wassira. Mwanasiasa anayefuata  mchana huu ni Amina Salum Ali.

Wednesday, June 3, 2015 Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya Tarehe 3 Juni 2015

BRN yapaisha sekta ya elimu

SEKTA ya Elimu imefanikiwa kwa asilimia 81 na kushika nafasi ya kwanza katika utekelezaji wa awamu ya kwanza ya Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (BRN). Matokeo ya utekelezaji wa mikakati iliyowekwa na BRN ni kupanda kwa ufaulu wa mtihani wa kumaliza Elimu ya Msingi (Darasa la Saba) na kupanda ufaulu wa mtihani wa kumaliza Elimu ya Sekondari (Kidato cha Nne). Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa aliyasema hayo bungeni jana wakati alipowasilisha Bajeti ya Mwaka 2015/16. Dk Kawambwa alisema, “Kwa mujibu wa taarifa ya mwaka mmoja (2013/14) sekta ya elimu imefanikiwa kwa asilimia 81 na kushika nafasi ya kwanza katika utekelezaji wa awamu ya kwanza ya mikakati hiyo.” Aliyajata baadhi ya mafanikio ambayo yamehakikiwa na ‘Presidential Delivery Bureau’ ni kutoa tuzo kwa shule na wanafunzi waliofanya vizuri kwenye matokeo ya darasa la saba na kidato cha nne. Alisema jumla ya tuzo 3,044 zilitolewa kwa shule zilizopata ufaulu uliotukuka na zile zilizo...

Rais Kikwete ziarani Ulaya

Hits: 215 Rais Jakaya KikweteRais Jakaya Kikwete RAIS Jakaya Kikwete jana alianza ziara rasmi ya wiki moja katika nchi tatu za Ulaya kwa mwaliko wa viongozi wa nchi hizo. Rais Kikwete ambaye aliondoka nchini usiku wa kuamkia jana baada ya kumaliza kuendesha Mkutano wa Wakuu wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kuhusu Burundi, ameanzia ziara yake katika Finland ambako atakaa kwa siku tatu. Baadaye, Rais Kikwete atatembelea nchi za Sweden na Uholanzi kabla ya kurejea nyumbani. Akiwa Finland, Rais Kikwete miongoni mwa mambo mengine leo atafanya mazungumzo rasmi ya Kiserikali na Rais wa nchi hiyo na baadaye atatembelea Bunge.

Maelfu ya wananchi kumsindikiza Lowassa kuchukua fomu ya Urais

Waziri Mkuu Wa zamani Edward Lowassa  anatarajia kwenda makao makuu ya chama cha Mapinduzi maarufu kama White House mkoani Dodoma  june 3 akisindikizwa na maelfu ya wananchi. Kwa  mujibu wa  Mnyetishaji  wetu  aliyezungumza  na mtandao  huu,  amearifu  kuwa wakazi wa Manispaa ya Dodoma watakwenda  kumpokea  Mbunge wa   Monduli   Edward   katika   wilaya  ya Manyoni   akitokea  mkoani  Arusha  kwenda mkoani Dodoma kuchukua fomu ya kugombea Urais kwa tiketi ya chama  cha Mapinduzi (CCM). Aidha, wagombea wote  wanaotaka kuwania urais kupitia chama cha Mapinduzi wanatakiwa kuchukua  fomu  ifikapo tarehe  3/6/2015  na  kurudisha  2/7/2015. Kutafuta  wadhamini  mikoani ni 3/6/2015 hadi 2/7/2015. Kamati  ya usalama na maadili itakutana 8/7/2015 ikifuatiwa na kamati ya Halmashauri kuu ya Taifa 9/7/2015. Uteuzi...

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya Tarehe 2 Juni 2015

Gwajima: Asiyempenda Lowassa Akale Limao!!!

Mchungaji wa Kanisa la Ufufuo na Uzima Askofu Josephati Gwajima amesema kwamba mwananchi  au mwanasiasa  yeyote asiyempenda Mbunge wa Monduli Edward Lowassa akale limao Askofu Gwajima alisema hayo juzi  mara baada ya Edward Lowassa kumaliza hatuba yake wakati akitangaza  nia ya kutaka kugombea  urais katika uchaguzi mkuukwa  tiketi  ya  Chama cha Mapinduzi, CCM. Kabla ya kumaliza hotuba yake wananchi walimshinikiza Edward Lowassa amsimamishe Askofu Gwajima  ndipo Lowassa alimuita na kumpa maiki aongee na wananchi waliofurika katika viwanja vya Sheikh Amri Abeid  jijini Arusha. Askofu Gwajima  alianza kwa kuomba mwenyezi Mungu aibariki safari ya Matumaini ya Mbunge wa Monduli Edward Lowassa na mwisho kabisa kuwapa mjumbe mzito wananchi kuwa mwenye Chuki na Lowassa akale limao.

Monday, June 1, 2015 Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya June 1, 2015